Wanawake nao wanataka kujua kama mwanaume anaweza kazi!

TANMO

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
11,513
11,274
Jamani hii nimeikuta kwenye Blog ya Dina Marios wa Clouds Fm.

Kuna dada mmoja ameolewa mwaka jana tena mke wa pili harusi ya kiislamu tumemchangia vizuri jamani kuanzia kitchen party,send off,harusi...sasa juzijuzi nikakutana nae nikawa namuuliza habari za maisha ya ndoa maana nikitambo hatujaonana,akaniambia alishaachana na yule mwanaume(mumewe),nikamuuliza kwanini ndio akaanza kunipa mchapo kama ifuatavyo.


Yeye katika maisha ya uchumba na bwana walikuwa hawajawahi kufanya tendo la ndoa,alikutana nae akawa anampa mahitaji yake muhimu lakini hakuwahi kumuomba tendo la ngono hata siku moja shost akashukuru mungu kwamba ni wanaume wachache utakutana nao katika maisha haya mkawa wapenzi na asikuombe naniliu..sasa baada ya mwaka kupita bwana akamwambia anataka kumuoa lakini mke wa pili.Mwanadashosti akaona si mbaya bahati ilioje akakubali kuolewa ndio na sisi tukashereheka....sasa wakiwa ndoani akawa anaona mbona bwana haniombi unyumba jamani!!!ikabidi yeye aanzishe michezo ili hatimae mchezo kamili uchezwe, baadae anakuja kugundua jamaa jogoo hawiki wala hasimami kujitutumua kuwika.


Akaendelea kuniambia kuwa alivumilia lakini kiukweli alishindwa akajikuta anaanzisha mahusiano na kijana mwingine akahakikisha yule mume anajua ili ampe talaka na kweli alijua na talaka akapewa ndoa ilidumu miezi 10 tu.Nikampa pole sana na tukaendelea na story zingine


Sasa nauliza tufanyeje?tukubali kuonja kwanza ili tujue kabisa mwanaume anaekuoa jogoo wake anawika na ngoma yake inakesha si ya kitoto au tuendelee na ule msemo wa kusubiri mpaka ndoa?

Mwisho wa kunukuu.
Chanzo Dina Marios Blog

Kwa mtazamo wangu nadhani ni vyema wanawake wakamfahamu mapema mwanaume kabla ya kukubali kufunga naye pingu za maisha manake tendo la ndoa ni haki ya kila mwanandoa ati!
 
Hiyo poa,

Lakini mimi nitasema kabisa naonja tu, kuoa sioi, hapo vipi?

Na vipi mmshashi akija na gia ya kuoa, akaonja, halafu kuingia mitini?

Tatizo ni kwamba, society yetu inamuangalia fuska wa kiume kama rijali na fuska wa kike kama malaya.Kwa hiyo wanawake wakitaka kudai usawa katika hili katika society yetu wataumia wenyewe.
 
Hapo mwanangu kama ni kuonjeshwa kama wauza njugu wa baa, mbona tutamega hadi zitukome hizo 'naniliu'
 
Kama suala ni kuonja onja tu kabla ya ndoa; basi, hutakoma hata ukioa. Maana tabia ya kuonja onja mboga mbali mbali itaendelea tu. Na ishu ya Ngoma ilivyokomaa siku hizi! We acha tu. Utaonja hata visivyoonjeka. Utashangaa umeshaoa lakini bado unavitolea mimacho vibinti vya watu. Maana unatamani kuonja. Teh teh teh teh tih tih tih tih
 
Sasa nauliza tufanyeje?tukubali kuonja kwanza ili tujue kabisa mwanaume anaekuoa jogoo wake anawika na ngoma yake inakesha si ya kitoto au tuendelee na ule msemo wa kusubiri mpaka ndoa?

jibu sahihi ndio hilo, pigia tu mstari.
na kuongezea hata wanaume tunahitaji 'kuonja' kidogo kama 'asali' tamu au chungu, heehehe teeh hahahaaaa.
 
Kuonja ni muhimu sana ukiona mtu anachumbia hata kwa miezi miwili bila kuomba ngoma ujue huyo si riziki.
 
Kwa maadili ya kidini inatakiwa mtu asionje mpaka atakapofunga ndoa. Ingawaje hii imekuwa ngumu kwa watu wengi sana, ndio maana kuonja onja kunakuwa kwingi sana.

Lakini mwamamke anaweza kumuuliza mume mtarajiwa mwaswali fulani fulani ambayo yatamfanya ajue kama jamaa sio riski (Jogoo hawiki)
 
Hakuna sababu ya kuonjaonja!

Hali hiyo aliyokutana nayo huyo mdada, sijui mshostito,..ni surprise ya ndoa, na ni kesi `rare sana kukutana nayo, hivyo wanajamii msiifanye kama ndo sababu ya kumess out!
 
haifai kuonja kabla ya ndoa,kwani itakuwa ni sawa na kuhalalisha uchafu wa zinaa.
kumbuka kuzini kumekatawa katika imani ya dini, zinaa inaleta ujinga na umasikini katika jamii hivyo haina budi kuepukwa.
 
Kwakweli huo ndo mtihani wenyewe unapokuja hapo,mana kwa sisi wakristo ukikutana na kaka kabla ya ndoa ni dhambi mana unakuwa umezini na ukisema usubiri hadi ndoa ndo hiyo kasheshe unakumbana nayo,ila nadhani ni muhimu wakati wa uchumba ukamdodosa huyo mwenzi wako utajua tu wangu hata katika touching jamani utashindwa?mana wengine wanakuwa na maumbile makubwa nk hivyo hata amabao jogoo haliwiki basi we siku tu mjaribu kuwa unamhitaji ukiona anakwepa sana hapo jua kuna jambo mana ndoa sio ya kukurupukia coz huyo mtu anakuwa ni wako wa maisha vingnevyo utaishia kutoka nje ya ndoa kila siku that is not gud.
 
Kwakweli huo ndo mtihani wenyewe unapokuja hapo,mana kwa sisi wakristo ukikutana na kaka kabla ya ndoa ni dhambi mana unakuwa umezini na ukisema usubiri hadi ndoa ndo hiyo kasheshe unakumbana nayo,ila nadhani ni muhimu wakati wa uchumba ukamdodosa huyo mwenzi wako utajua tu wangu hata katika touching jamani utashindwa?mana wengine wanakuwa na maumbile makubwa nk hivyo hata amabao jogoo haliwiki basi we siku tu mjaribu kuwa unamhitaji ukiona anakwepa sana hapo jua kuna jambo mana ndoa sio ya kukurupukia coz huyo mtu anakuwa ni wako wa maisha vingnevyo utaishia kutoka nje ya ndoa kila siku that is not gud.
 
Kuhusu huku kuonja mi naona kwaweza zua balaa,sababu wapo wanaume wengine dada zangu mkijaribu kuonja tuu,hamta tamani ndoa tena maishani mwenu,wapo wanaume wenye maumbile na kasi ya ajabu,hivyo basi sio kila kitu huonjwa,mtakuja onja sumu iwadhuru maishani!!
 
Kama suala ni kuonja onja tu kabla ya ndoa; basi, hutakoma hata ukioa. Maana tabia ya kuonja onja mboga mbali mbali itaendelea tu. Na ishu ya Ngoma ilivyokomaa siku hizi! We acha tu. Utaonja hata visivyoonjeka. Utashangaa umeshaoa lakini bado unavitolea mimacho vibinti vya watu. Maana unatamani kuonja. Teh teh teh teh tih tih tih tih

Cool! sio hivyo unavyodai wewe kuonjaonja kila mtu, bali ku-test yule ambaye unamuona atakuwa ubavu wako. Let say kama hao walikaa kwenye mahusiano mwaka mzima na mpaka wakafikia hatua ya uchumba na mwisho kuona ina maana walikuwa wameshafika mbali.
 
Kwakweli huo ndo mtihani wenyewe unapokuja hapo,mana kwa sisi wakristo ukikutana na kaka kabla ya ndoa ni dhambi mana unakuwa umezini na ukisema usubiri hadi ndoa ndo hiyo kasheshe unakumbana nayo,ila nadhani ni muhimu wakati wa uchumba ukamdodosa huyo mwenzi wako utajua tu wangu hata katika touching jamani utashindwa?mana wengine wanakuwa na maumbile makubwa nk hivyo hata amabao jogoo haliwiki basi we siku tu mjaribu kuwa unamhitaji ukiona anakwepa sana hapo jua kuna jambo mana ndoa sio ya kukurupukia coz huyo mtu anakuwa ni wako wa maisha vingnevyo utaishia kutoka nje ya ndoa kila siku that is not gud.


Kwa kweli kwa sisi wanawake inakuwa ngumu sana kuanza kumwambia mshikaji kwamba leo tukananihii ukizingatia kama ndo kwanza mnaanza mahusiano afadhali kama ingekuwa ni mtu wako hii inawezekana wanawake tumeumbwa na aibu babu!!
 
Ninavyojua kulingana na Biblia, hapo hakukuwa na ndoa. Ndoa maana yake halisi ni tupu ya mbele ya mwanaume iingie ndani ya tupu ya mbele ya mwanamke.Bila kitendo hicho hakuna ndoa na ndio maana nashangaa mtu kudai talaka; labda kwa vile ilikuwa ya Kiislamu nami uuslamu siujui unadai nini ktk hali kama hiyo.

Ila napenda kufahamu: Je kama watu wamefanikiwaa kimaisha kupitia ujambazi ndio watu wote tuwe majambazi? Mliouunga mkono uzinzi fikirieni upya.
 
Kwakweli huo ndo mtihani wenyewe unapokuja hapo,mana kwa sisi wakristo ukikutana na kaka kabla ya ndoa ni dhambi .

Hapana sio dhambi si kuna kitubio?
Kumega muhimu kuna wengine tunajiexpress sasa ni lazima ujue mapema usije ukaanza kukimbia Ndoa ooh mimi mme wangu anakunjuka kunako ukiwaambia mashostino wako watakucheka.
 
Kwa kweli kwa sisi wanawake inakuwa ngumu sana kuanza kumwambia mshikaji kwamba leo tukananihii!

Teh teh teh utakufa njaa Safina shauri yako si unamwambia tu mzee vp mambo flani hufeel? utaona respond yake.
 
amekoma kuolewa kwenye ndoa ya watu wengi. hayo ndo matunda yake. Mungu anataka mme mmoja mke mmoja, yeye anaenda kushare. mwacheni ajifunze na ndo atajua kuwa,.....sitaki kumalizia nisije nikakashifu faith fulani.
 
Mi naona kwamba ni bora wangeendelea na ndoa yao kwan maana nzima ya ndoa sio kundoana tu bali pia kuna mambo mengine ya kusaidiana. kwa mfano siku bwana angekuwa mzima alafu sku wametoka kufunga ndoa wakapata ajali iliyopelekea bwana kuumia vibaya ivyo kushindindwa tena kufanya mambo ytu je angemuacha, je na kma yeye mwanamke ni mgumba aachwe?
 
Hapana sio dhambi si kuna kitubio?
Kumega muhimu kuna wengine tunajiexpress sasa ni lazima ujue mapema usije ukaanza kukimbia Ndoa ooh mimi mme wangu anakunjuka kunako ukiwaambia mashostino wako watakucheka.


Fidel unajua ukweli ni kwamba dunia ya sasa tunayoishi sie ni tofauti na zamani ambako hizi sheria zilikuwa zinaaply. mfano

Wazazi wetu walikuwa wanajua kabisa mchumba flani anatoka ukoo flani, wana matatizo flani either ya kurithi au hata kama mchumba ana matatizo ya utu uzima ilikuwa rahisi kujua lakini si saa hivi ambako mtu wa mashariki anaendaoa mtu wa magharibi akiwa na magonjwa ya kurithi basi mnagawana umasikini huo wa magonjwa (na ndio maana tumekuwa tukishuhudia milipuko ya magonjwa ambayo zamani hayakuwepo)

Pili katika dunia ya sasa ya utandawazi na effects zake ni wazi kuwa hata maadili ya watoto wa kike yamepotea (hata wa kiume) sasa hivi ni rahisi sana kwa binti wa kike kuwa ameshamaliza kila kitu na hata kizazi tena hakifanyi kazi maana kuna wanaoanza wakiwa shule ya msingi hata anapofikia muda wa kuolewa mh amekubuhu sasa atakapokutana na mwenzi mtarajiwa kujizuia hataweza. Matokeo yake wanajikuta mambo yameharibika (wamebarikiwa ujauzito kabla ya ndoa)

Tatu kwa dunia ya sasa usipojaribu unawezajikuta unaolewa na mwanamke mwenzio ati au mchicha mwiba (dume lakini pia jike)

Sihalalishi uzinzi but ninaamini kama tungewezarudisha siku nyuma enzi za mababu basi tungewezazuia kuonjana!
 
Back
Top Bottom