Wanawake mnavumilia mengi sana, hongera kwenu

vposterior

JF-Expert Member
Jul 19, 2018
732
1,231
Wadau leo nilienda kuswali basi tayari nimejipanga katika safu kusubiri imamu atuongoze kuswali mara kaingia jamaa akasimama pembeni yangu na yeye amekuja kufanya ibada. Lahaula jamaa ananuka harufu mbaya sana ya sigara yaani hadi kero, kwa kweli ilibidi nikatishe ibada na nikachomoka kwenye ile safu nikajiunga upande wa pili.

Sasa nimejiuliza sana mbaba huyu ana mke na wanalala kitanda kimoja hali inakuwaje kwa huyo mama na wengine wanakuwa walevi pia basi ni vundo juu ya vundo.

Duuh poleni sana wanawake ambao sio walevi wala wavutaji lakini mmeolewa au mnaishi na hao watu.
 
Mlevi mmoja samahani sana kama nimekugusa. Maana wanaongelewa wavutaji na walevi na wewe ni miongoni mwao.
Wala usiwaze mkuu mi sina wa kumbuguza kama hao wengine wenye familia na wala sihitaji nimekuwa committed na pombe tuu sina female companion wakuvumilia maswaibu yangu dhaidi ya pombe


Note : sio walevi wote wananuka uvundo wengine tunalewa kistaarabu
 
Wala usiwaze mkuu mi sina wa kumbuguza kama hao wengine wenye familia na wala sihitaji nimekuwa committed na pombe tuu sina female companion wakuvumilia maswaibu yangu dhaidi ya pombe


Note : sio walevi wote wananuka uvundo wengine tunalewa kistaarabu
Sawa mkuu kila la kheri na partner wako pombe.
 
Ungemtimua akaondoe harufu, Muda wa swala hata ukiwa na harufu ya vitunguu mdomoni unatakiwa kuiondoa ili usiwakere wengine ibadani....


Pole yako tumeipokea,, asante sana
 
Kuna siku tulikuwa tuna-compete na msela mmoja kwa demu flani mrembo kiasi, ila tulikuwa hatufahamiani na jamaa. Na demu alijua kabisa kama tunamtaka sote.

Kiukweli nilikuwa na asilimia chache za kumpata, maana jamaa alionekana matawi ya juu na alikuwa na gari nzuri pia.

Jamaa na rafiki yake wakawasha sigara.

Kitendo cha kuwasha masigara yao kilinipa credits kwa mrembo. Na demu alinambia kabisa hapendi harufu za sigara.
 

Similar Discussions

15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom