Wanawake mnavopenda kuhudumiwa na wanaume hivi kuna mvuto gani?

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
Habari za mchana wana MMU,

Kama title inavosema hapo juu.

Mara nyingi katika huduma tofauti wanawake wanapenda na kufurahia sana wahudumiwe na wanaume. Ikiwa ni restaurant au bar kama kuna wahudumu wa kike utaskia lawama 'basi wahudumu wa kike wa hii bar wanajivuuta sana' au 'wanaringa sana'. Utashangaa hata fundi wa kushona nguo za kike wapo radhi kum support kwanza fundi mwanaume kuliko mwanamke mwenzao.

Juzi uliletwa uzi humu kuhusu waosha miguu wanaume na mtazamo wa jamii. Ninahakika hata wakitokea waosha miguu wa kike, wengi katika wanawake watapendelea zaidi kusuguliwa miguu na kuoshwa kucha na wanaume.

Kwenye huduma za afya napo hasa katika matibabu yanayohitaji madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake ( gynecologists) wanawake always watapendelea kuhudumiwa na madaktari wanaume.

Yupo dada mmoja alikua anamtafuta Gyno akaelekezwa kwa Doctor Bingwa anaitwa Thomas(ni jina lake la ubini wake maana yeye anaitwa Angela) basi yule dada hakuingia kuhudumiwa na Dr Angela.

Ingawa yawezekana hii ni case ya mtu mmoja lakini in most cases wanawake huhitaji huduma ya mwanaume zaidi (fanya tafiti kwa wajawazito wanaokaribia kujifungua) na kama kuna mwanamke inakua ni second option.

Nauliza wakuu hii ni kasumba, kutojiamini kwa jinsia hii au ni kweli wanaume wanatoa huduma nzuri kwenye kila sekta?
 
Kuhudumiwa na mwanamke mwenzako inataka moyo.
Miaka fulani, iliyopita nilikuwa na tafuta kazi kampuni Fulani, kumbe general Meneja ni mke wa kwenye kampuni, kila kitu ni yeye, Mara chache sana kumkuta mmewe ofisini.

Huyooo nikaelekea town hiyo ofisi sikujua sehemu ilipo, ilibidi niulize duka Fulani wanielekeze, nikamuuliza mkaka Fulani anauza duka anielekeze,samahani kaka ofisi ya ....... Iko wapi ? Akanitazama akacheka, akaniuliza kwani una shida gani? Nikajikanyaga baadae nikamwambia na tafuta kazi, alicheka kwa nguvu akanambia " ofisi ile pale ila hupati kazi pale kwa kukuona tu"

Nikaenda kufika reception on kauliza kwa hr wakanielekeza kwa mama, duh kufika salama anaitikia kama anataka kutapika ananiona juu chini, nikamwambia shida yangu, akajibu sasa wewe hapa tutakupa kazi gani? Kwanza kazi hakuna, umesomea nini? Maskini vyeti anavyo mkononi shule hana. Kibongeee kama nini kajaa kwenye kiti kabinua midomo, nikawaza mda wa kubinuliwa wageni midomo si aende hata Jim ??? nikaondoka sikurudi tena.

Alieniambia niende pale ni Rafiki wa mkurugenzi ingawa mm mkurugenzi simjui najua jina la kampuni, alifatilia kwa nn sikupewa kazi akapiga simu wakamwambia sijafika.pale ahaaa kazi za watu.
 
Kuhudumiwa na mwanamke mwenzako inataka moyo.
Miaka fulani, iliyopita nilikuwa na tafuta kazi kampuni Fulani, kumbe general Meneja ni mke wa kwenye kampuni, kila kitu ni yeye, Mara chache sana kumkuta mmewe ofisini.

Huyooo nikaelekea town hiyo ofisi sikujua sehemu ilipo, ilibidi niulize duka Fulani wanielekeze, nikamuuliza mkaka Fulani anauza duka anielekeze,samahani kaka ofisi ya ....... Iko wapi ? Akanitazama akacheka, akaniuliza kwani una shida gani? Nikajikanyaga baadae nikamwambia na tafuta kazi, alicheka kwa nguvu akanambia " ofisi ile pale ila hupati kazi pale kwa kukuona tu"

Nikaenda kufika reception on kauliza kwa hr wakanielekeza kwa mama, duh kufika salama anaitikia kama anataka kutapika ananiona juu chini, nikamwambia shida yangu, akajibu sasa wewe hapa tutakupa kazi gani? Kwanza kazi hakuna, umesomea nini? Maskini vyeti anavyo mkononi shule hana. Kibongeee kama nini kajaa kwenye kiti kabinua midomo, nikawaza mda wa kubinuliwa wageni midomo si aende hata Jim ??? nikaondoka sikurudi tena.

Alieniambia niende pale ni Rafiki wa mkurugenzi ingawa mm mkurugenzi simjui najua jina la kampuni, alifatilia kwa nn sikupewa kazi akapiga simu wakamwambia sijafika.pale ahaaa kazi za watu.
Mifano kama hii ipo miiingi sana, sasa sijui kuna siri gani ndani yake
 
Back
Top Bottom