Wanawake mnakwama wapi?

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Dec 13, 2014
3,900
6,658
Wanawake wawili walikuwa wakisimulia kilichotokea usiku baada ya waume zao kurejea nyumbani kutoka kazini.

Mwanamke 1
Shoga yangu, jana ilikuwa siku mbaya kwangu mume aliporudi kutoka kazini alifika nikamuwekea maji bafuni alipomaliza kuoga nikapakuwa chakula tukala nikitegemea kuwa akimaliza kula atanitoa aut, alipomaliza kula akaelekea chumbani na kulala nami ikabidi tu nimfate tukalale.

Mwanamke 2
Mimi sijui niseme nini kifupi Mungu kanipatia anipendaye, yaani alipofika nikamwabia tutoke muda huo huo tuliondoka sikupata hata tabu maana ameenda kuoga huko huko na tulikula hotelini,
Wakati wa kurudi sasa hatukuchukua hata taxii tulirudi kwa mguu akiwa ananikumbatia na kunipa maneno ya mahaba.

Upande wa pili waume za wanawake hao wakiwa kazini walikuwa wakiongea:

Mume wa mwanamke 1:
Rafiki yangu, mke wangu ni zaidi ya malikia yaani ananijari kwa kila hali, jana nimekuta katayarisha kila kitu, nilioga maji mazuri na alikuwa kapika chakula kitamu kifupi nampenda sana siwezi kumsariti.

Mume wa mwanamke 2
Rafiki yangu, nakuonea wivu mimi nimerudi sijakuta chakula hata maji tu ya kuoga ikabidi tu nimchukue nitoke nae aut, bahati mbaya sikuwa na pesa ya kutosha baada ya matumizi hela yote iliisha nikakosa hata ya nauli ya kuturudisha nyumbani, ilibidi kutembea nikajifanya nampenda nikawa namkumbatia na kumpumbaza kwa maneno ya mahaba. tulitembea kwa mguu hadi nyumbani.

Wanaume anahita utulivu na moyo wa faraja hasa anaporudi na stress za kazini.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom