Wanawake hasa wa miaka hii ya utandawazi wakifanikiwa kama wapo kwenye uchumba au ndoa lazima iteteleke (asilimia kubwa sio wote)ipo

Mzee wa old school

JF-Expert Member
May 16, 2021
504
830
Habari zenu wandugu..

Nimependa nilete hii mada. Hivi ni kwanini wanawake wanashindwa kumudu mafanikio hasa wa miaka hii ya utandawazi.

Mfano wa kweli kuna watu wengi nawafahamu wanawake zao baada ya kufanikiwa wakavunja mahusiano.. Pia hata Mimi ishawahi nitokea kuna binti nilikuwa nae kwenye mahusiano.

Wote tulikua tuna "haso" mwenzangu bana Mungu akamnyooshea kwa kiasi akatoboa kiaina. Eeh! Nilijuta kila mara nategwa nikosee tu iwe sababu niachwe nikashtukia nikawa najitahidi kukwepa. Hahaha akaona chuma akitegwi ikabidi anichane live tu nikae mbali nae.

Basi nikawa mpole nikakubali. Lakini miaka imepita akayumba simu zikaanza na akaniomba sana msamaha. Nikakubali lakini nikawa naishi naye kwa machale.

Mungu akampa tena heeeeh! Kama kawaida kanitafutia sababu kanipiga tofali sehemu zote ili nisimtafute.

Sasa najiuliza hawa wenzetu vipi? Afu eti haki sawa.. Ndio IPO hivyo kweli?
 
Tatuta chako afu tuone ukipata naww unakuwaje..!!!
Daah! Kweli wanawake mmeisha.. Kwahiyo hivyo ndo mnavyofundishwaga huko haki sawa, sasa Vyangu ninavyo vingi tu... Na havinipagawishi maana vinatafutwa.... Nyinyi badae mtaleta kizazi ambacho hakijielewi na hakijui dhamani ya maisha iko wapi
 
Ni kweli kabisa,mwanamke nikishika mpini wewe makali navuta upanga kimakusudi ili ukutoe vimikono hivyo uache kunitomasatomasa.
 
Back
Top Bottom