Wanawake 38 wakamatwa kwa kukeketa wasichana wadogo

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,303
000_Par1114351.jpg


Polisi wilayani Same imewakamata wanawake 38 kwa tuhuma za kukeketa wasichana wadogo. Wanawake hao walikamatwa juzi Jumapili wakati wakicheza dansi ya kitamaduni ya kuzunguka nyumba iliyokuwa na wasichana 21 wenye umri kati ya miaka 3 na 15 ambao tayari walikuwa wameshakeketwa.

Akiongea na vyombo vya habari, Meya wa wilaya ya Same, Mh. Herman Kapufi, alisema kuwa aliwafahamisha polisi mara tuu baada ya kusikia habari hizo za ukeketaji. Kapufi amesema baadhi ya wasichana hao bado walikuwa wanavuja damu sehemu zao za siri huku majeraha ya engine yakiendelea kupona.

Tanzania imepiga marufuku ukeketaji tokea mwaka 1998 ambapo mtu anayekutwa hatiani kwa kosa la ukeketaji anaweza kuhukumiwa hadi kifungo cha miaka 15. Hata hivyo, ukeketaji bado unafanywa kwenye baadhi ya jamii. Tafiti zinaonyesha kuwa asilimia 15 ya wanawake na wasichana wamekeketwa huku vinembe vyao vikiwa vimekatwa na kuondolewa kabisa kwenye sehemu zao za siri.

Mara nyingi ukeketaji huo hufanywa kwa kutumia kisu, wembe au kitu kingine chenye nja kali bila ganzi au taratibu zozote za kiafya. Baadhi ya wasichana hupoteza maisha yao kutokana na majereha makubwa yatokanayo na ukeketaji. Pia kuna jamii nyingine ambazo zinawatenga wanawake ambao hawajakeketwa.

Baadhi ya watafiti wa mambo wanadai kuwa baadhi ya watu wanaamini kuwa mwanamke aliyekeketwa anakuwa mwaminifu zaidi kwa mume wake.

Habari kwa hisani ya AFP
 
Afisaa mmoja wa serikali kaskazini mwa Tanzania ameambia BBC kuwa kikundi kikubwa cha watu waliokamatwa kwa kuhusika na ukeketaji wa wasichana mjini Moshi watafikishwa mahakamani Jumatano. Kamishna wa wilaya katika eneo la Kilimanjaro (Herman Kapufi,) amesema kuwa watu 38 waliokamatwa Jumatatu miongoni mwao ni wazazi wa wasichana waliokuwa wanakeketwa. Alisema kuwa wasichana waliokeketwa wanapokea matibabu.

Maafisa wakuu mjini Moshi Tanzania, waliwakamata wanawake 38 mnamo siku ya Jumatatu waliopatikana wakiwakeketa wasichana katika eneo hilo. Haijulikani idadi ya wasichana walioathirika. Lakini ripoti zinasema kuwa walikuwa kati ya umri wa miaka 3 na 16. Ingawa ukeketaji ambao umeharamishwa huendelezwa katika sehemu nyingi za Mara na Dodoma nchini Tanzania , hilo sio jambo la kawaida kutokea mjini Moshi.

Inaarifiwa wanawake hao walikamatwa walipokuwa wanacheza dansi ya kitamaduni wakiwazingira wasichana ambao ndio walikuwa wamekeketwa tu. Baadhi ya wasichana inaarifiwa bado walikuwa wanavuja damu na wengine wakiwa wanauguza majeraha. Ukeketaji umeharamishwa nchini Tanzania tangu mwaka 1998 ingawa bado unaendelezwa katika baadhi ya sehemu za nchi hiyo. Inakisiwa asilimia 15 ya wasichana pamoja na wanawake wamekeketwa nchini humo.

Sosi: BBC: Mangariba 38 matatani Moshi Tanzania - BBC Swahili - Habari
 
HAFU UTASIKIA WATU NA NGO ZAO UKEKETAJI USHAMIRI SANA MKOA WA MARA HASWA TARIME, kisa viongozi wengi kwenye hzo NGOs ni WACHAGA na WAPARE
Navyofahamu ukeketaji umeshamiri sana Uchagani, Upareni, Umasaini, kwa wambulu na Wairaki aka wabagdadi
 
HAFU UTASIKIA WATU NA NGO ZAO UKEKETAJI USHAMIRI SANA MKOA WA MARA HASWA TARIME, kisa viongozi wengi kwenye hzo NGOs ni WACHAGA na WAPARE. Navyofahamu ukeketaji umeshamiri sana Uchagani, Upareni, Umasaini, kwa wambulu na Wairaki aka wabagdadi

Umeona eh? Ukeketaji upo maeneo mengi tuu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom