kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,307
- 12,602
Polepole na Musukuma ni watu wanaopingana na Rais Mama Samia kwenye kila kitu. Wanabweka kwenye mitandao kupinga maamuzi ya Rais.
Walipinga chanjoweeeeee lakini mwishowe nadhani na wawo walichanja kimyakimya.
Sasa hivi wanapinga uwamuzi wa mama Samia wa kuisafisha miji, eti miji isisafishwe eti kuwatetea wavamizi na wachafuzi wa maeneo wasiondolewe mitaani.
Kwenye awamu ya Tano hawakuwa hivyo hata kidogo, kule barabara ya ubungo kimara maelelfu ya watu wakiwemo wamachinga waliondolewa kinyama kabisa kupisha upanuzi wa barabara tena walivunjia hata kule ambako barabara haitafika lakini Polepole na Musukuma hawakunyanyua midomo Yao hata millimeter moja kupinga na kutetea.
Leo hii eti miji isisafishwe ili watembea kwa miguu wawatunze wamachinga kwa kuwaachia njia zao za kukwepea magari kuepuka ajali. Kwa akili za Polepole na Musukuma wamachinga Wana haki kuliko watanzania waliozibiwa njia zao za kutembelea na kuchafuliwa mazingira yao.
Hizi ni Chuki za wazi ambazo ni kiongozi mkomavu TU ndiye anaeweza kuzivumilia.
Wamachinga ni sehemu ya jamii yetu, hawako pale kwa msingi ya dini, kabila Wala mkoa. Ni WA dini zote, makabila yote na kutoka mikoa yote ya bara na visiwani, hakuna mwenye Chuki nao binafsi, lakini huwezi kuchukua haki za watanzania wengine ukawapa wamachinga eti kwakuwa wanatafuta riziki. Lazima tuanzie pahala katika kutatua kero za makundi yote bila upendeleo.
Polepole na Musukuma hawatoi njia mbadala ya kuhakikisha usalama wa watembea kwa miguu, mitaro iliyozibwa, vibanda vya wamachinga wanamokimbilia vibaka kukwepa kukamatwa wanapowaibia watanzania wenzao au maji yanaotuama na kufurika nyakati za mvua kwa njia za maji kuzibwa.
Hizi ni siasa uchwara kabisa, Maana haki yako lazima ikomee pale inapoanza haki ya mwenzio. Kwanini haki ya mmachinga isikomee pale haki ya mtembea kwa miguu inapoanzia?
Heshima ni kujiheshimu, Mama Samia kaletwa na Mungu kwetu hakupiga kampeni ya kuwa Rais, kila mtu analifahamu hilo, tumheshimu, wacha atengeneze pale wenzake waliposhindwa. Mama Samia ni mwanamke, na tabia ya akinamama ni usafi, Wacha asafishe maana hakuna sheria yoyote anayokiuka kwa kuwaondoa, huwezi kuendesha nchi kwakutumia moyo badala ya akili/ubongo.
Rais Samia atapigiwa kura za kishindo na wale watanzania ambao:
1. Wanaopenda utaratibu kwenye kila jambo. Nchi ilikosa utaratibu, jogoo wa sh.15,000 alinunuliwa kwa sh.100,000, Waziri alitumbuliwa mbele ya kadamnasi na matusi juu na yeye mwenyewe, mkewe na watoto wakiwepo.
2. Wanaopenda uhuru wa kutoa mawazo bila kubugudhiwa.
3. Wanaoamini kwenye haki za binadamu bila kujali jinsia yake.
4 wanaopenda usafi na miji safi
5. Unaopenda utawala wa sheria.
6. Wanaopenda kuona mihili yote inafanyakazi kazi zake bila kuingiliwa.
Walipinga chanjoweeeeee lakini mwishowe nadhani na wawo walichanja kimyakimya.
Sasa hivi wanapinga uwamuzi wa mama Samia wa kuisafisha miji, eti miji isisafishwe eti kuwatetea wavamizi na wachafuzi wa maeneo wasiondolewe mitaani.
Kwenye awamu ya Tano hawakuwa hivyo hata kidogo, kule barabara ya ubungo kimara maelelfu ya watu wakiwemo wamachinga waliondolewa kinyama kabisa kupisha upanuzi wa barabara tena walivunjia hata kule ambako barabara haitafika lakini Polepole na Musukuma hawakunyanyua midomo Yao hata millimeter moja kupinga na kutetea.
Leo hii eti miji isisafishwe ili watembea kwa miguu wawatunze wamachinga kwa kuwaachia njia zao za kukwepea magari kuepuka ajali. Kwa akili za Polepole na Musukuma wamachinga Wana haki kuliko watanzania waliozibiwa njia zao za kutembelea na kuchafuliwa mazingira yao.
Hizi ni Chuki za wazi ambazo ni kiongozi mkomavu TU ndiye anaeweza kuzivumilia.
Wamachinga ni sehemu ya jamii yetu, hawako pale kwa msingi ya dini, kabila Wala mkoa. Ni WA dini zote, makabila yote na kutoka mikoa yote ya bara na visiwani, hakuna mwenye Chuki nao binafsi, lakini huwezi kuchukua haki za watanzania wengine ukawapa wamachinga eti kwakuwa wanatafuta riziki. Lazima tuanzie pahala katika kutatua kero za makundi yote bila upendeleo.
Polepole na Musukuma hawatoi njia mbadala ya kuhakikisha usalama wa watembea kwa miguu, mitaro iliyozibwa, vibanda vya wamachinga wanamokimbilia vibaka kukwepa kukamatwa wanapowaibia watanzania wenzao au maji yanaotuama na kufurika nyakati za mvua kwa njia za maji kuzibwa.
Hizi ni siasa uchwara kabisa, Maana haki yako lazima ikomee pale inapoanza haki ya mwenzio. Kwanini haki ya mmachinga isikomee pale haki ya mtembea kwa miguu inapoanzia?
Heshima ni kujiheshimu, Mama Samia kaletwa na Mungu kwetu hakupiga kampeni ya kuwa Rais, kila mtu analifahamu hilo, tumheshimu, wacha atengeneze pale wenzake waliposhindwa. Mama Samia ni mwanamke, na tabia ya akinamama ni usafi, Wacha asafishe maana hakuna sheria yoyote anayokiuka kwa kuwaondoa, huwezi kuendesha nchi kwakutumia moyo badala ya akili/ubongo.
Rais Samia atapigiwa kura za kishindo na wale watanzania ambao:
1. Wanaopenda utaratibu kwenye kila jambo. Nchi ilikosa utaratibu, jogoo wa sh.15,000 alinunuliwa kwa sh.100,000, Waziri alitumbuliwa mbele ya kadamnasi na matusi juu na yeye mwenyewe, mkewe na watoto wakiwepo.
2. Wanaopenda uhuru wa kutoa mawazo bila kubugudhiwa.
3. Wanaoamini kwenye haki za binadamu bila kujali jinsia yake.
4 wanaopenda usafi na miji safi
5. Unaopenda utawala wa sheria.
6. Wanaopenda kuona mihili yote inafanyakazi kazi zake bila kuingiliwa.