Lizarazu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2015
- 6,334
- 7,868
Habarini za jumamosi wana MMU?
Katika maisha ya kimahusiano wanaume tumekuwa tukifanya mambo mengi sana kwa ajili ya wanawake tuwapendao ikiwemo kupigana na mwanaume mwenzio na chanzo ikiwa ni yeye.
Na mara nyingi huwa tunafanya hivi pasipo kushurutishwa na mtu yeyote, bali huwa tunasukumwa tu na ego zetu za kiume hili kutaka kumuhakikishia tu kwamba wewe ni kidume haswa(zagamba).
Bahati mbaya unaweza ukapigana mpaka ukatolewa jicho ukiamini kwamba unapigania penzi lakini yeye kwa upande wake asishtuke kabisa na akakuacha mchana kweupeee!! Ukabaki unajilaumu tu na kuonekana mjinga.
HIKI NI KISA CHANGU KILICHOTOKEA MIAKA KADHAA ILIYOPITA.
Nilipokuwa form one kuna mtoto mmoja wa kihaya mashalah alikujaga second-selection na mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kumzoea pale shuleni kwa maana nyingine mimi ndie nilikuwa mwenyeji wake.
Yule mtoto kiukweli alitokea kunielewa sana na hata mimi mwenyewe pia nilimwelewa vilivyo na mwisho wa siku nilimtongoza lakini hakunipa jibu.
Sasa wakati bado nipo nasubiri jibu, akatokea jamaa mmoja wa Form-three akamtongoza na ndani ya muda mfupi tu yeye akakubaliwa akaanza na kumla kabisa na mbaya zaidi demu akaanza kunipotezea mimi, kiukweli niliumia sana na nikatokea kumchukia yule jamaa.
Nakumbuka ilikuwa ni siku ya Ijumaa siku hiyo sikwenda shuleni na madaftari nilienda kwa kazi moja tu, kumshikisha adabu mtu ambaye nilimuona kama ameninyang'anya demu wangu....
Yule demu nakumbuka mara nyingi muda wa kutoka shule alikuwa anaongozana na mshikaji, sasa mimi siku hiyo niliwavizia sehemu ambayo wako wenyewe wawili tu njia nzima na bahati nzuri ikawa hivyo kweli.
Nilipowafikia nikawasimamisha yule demu akanipuuza, lakini jamaa yake akasimama tena kwa kujiamini kabisa halafu akaanza kunipiga beat eti nisimzoee kabisa demu wake, nami sikukaa kimya nikaanza kumjibu...jamaa alivyojiroga si akanikwida kisa tu yeye ni mrefu basi acha iwe varangati hapo!
Nakumbuka yule jamaa nilimpiga kabari moja matata hadi akaanza kupiga kelele za kuomba msaada na hapo ni baada ya kuwa ameshaning'ata lakini akaona simwachii maana nilikuwa nna hasira nae vibaya mno.
Jumatatu iliyofuata nilikutana na yule demu wake ambaye ndio alikuwa chanzo cha ugomvi, alinitukana sana akisema kwamba eti nilitaka kumuua mtoto wa watu(bwana yake) bila kosa lolote na kamwe hawezi kuwa na mimi, baada ya hapo hatukuwahi kuongea tena mpaka ana hama shule form-two.
Niliumia sana kumkosa yule demu maana mbali tu na kupigana kwa ajili yake pia mimi ndio nilikuwaga namfundisha, alikujaga kuanza shule hajui chochote hata pre-form one alikuwa hajasoma, nilijitoa Sana kwa yule binti wakati yule jamaa mwingine aliyempata alitumia status ya "u-form three tu.
Kwangu Mimi hiki ni kisa ambacho nakikumbuka kwa ukaribu, unaweza na wewe uka-share kisa chako hapa!
Je umewahi kupigana kwa ajili ya mwanamke na bado mwanamke huyo ukamkosa!??
Karibu.
Katika maisha ya kimahusiano wanaume tumekuwa tukifanya mambo mengi sana kwa ajili ya wanawake tuwapendao ikiwemo kupigana na mwanaume mwenzio na chanzo ikiwa ni yeye.
Na mara nyingi huwa tunafanya hivi pasipo kushurutishwa na mtu yeyote, bali huwa tunasukumwa tu na ego zetu za kiume hili kutaka kumuhakikishia tu kwamba wewe ni kidume haswa(zagamba).
Bahati mbaya unaweza ukapigana mpaka ukatolewa jicho ukiamini kwamba unapigania penzi lakini yeye kwa upande wake asishtuke kabisa na akakuacha mchana kweupeee!! Ukabaki unajilaumu tu na kuonekana mjinga.
HIKI NI KISA CHANGU KILICHOTOKEA MIAKA KADHAA ILIYOPITA.
Nilipokuwa form one kuna mtoto mmoja wa kihaya mashalah alikujaga second-selection na mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kumzoea pale shuleni kwa maana nyingine mimi ndie nilikuwa mwenyeji wake.
Yule mtoto kiukweli alitokea kunielewa sana na hata mimi mwenyewe pia nilimwelewa vilivyo na mwisho wa siku nilimtongoza lakini hakunipa jibu.
Sasa wakati bado nipo nasubiri jibu, akatokea jamaa mmoja wa Form-three akamtongoza na ndani ya muda mfupi tu yeye akakubaliwa akaanza na kumla kabisa na mbaya zaidi demu akaanza kunipotezea mimi, kiukweli niliumia sana na nikatokea kumchukia yule jamaa.
Nakumbuka ilikuwa ni siku ya Ijumaa siku hiyo sikwenda shuleni na madaftari nilienda kwa kazi moja tu, kumshikisha adabu mtu ambaye nilimuona kama ameninyang'anya demu wangu....
Yule demu nakumbuka mara nyingi muda wa kutoka shule alikuwa anaongozana na mshikaji, sasa mimi siku hiyo niliwavizia sehemu ambayo wako wenyewe wawili tu njia nzima na bahati nzuri ikawa hivyo kweli.
Nilipowafikia nikawasimamisha yule demu akanipuuza, lakini jamaa yake akasimama tena kwa kujiamini kabisa halafu akaanza kunipiga beat eti nisimzoee kabisa demu wake, nami sikukaa kimya nikaanza kumjibu...jamaa alivyojiroga si akanikwida kisa tu yeye ni mrefu basi acha iwe varangati hapo!
Nakumbuka yule jamaa nilimpiga kabari moja matata hadi akaanza kupiga kelele za kuomba msaada na hapo ni baada ya kuwa ameshaning'ata lakini akaona simwachii maana nilikuwa nna hasira nae vibaya mno.
Jumatatu iliyofuata nilikutana na yule demu wake ambaye ndio alikuwa chanzo cha ugomvi, alinitukana sana akisema kwamba eti nilitaka kumuua mtoto wa watu(bwana yake) bila kosa lolote na kamwe hawezi kuwa na mimi, baada ya hapo hatukuwahi kuongea tena mpaka ana hama shule form-two.
Niliumia sana kumkosa yule demu maana mbali tu na kupigana kwa ajili yake pia mimi ndio nilikuwaga namfundisha, alikujaga kuanza shule hajui chochote hata pre-form one alikuwa hajasoma, nilijitoa Sana kwa yule binti wakati yule jamaa mwingine aliyempata alitumia status ya "u-form three tu.
Kwangu Mimi hiki ni kisa ambacho nakikumbuka kwa ukaribu, unaweza na wewe uka-share kisa chako hapa!
Je umewahi kupigana kwa ajili ya mwanamke na bado mwanamke huyo ukamkosa!??
Karibu.