Wanaume wanaooa au wanaopenda kuoa wanawake wa kijijini ndo waharibifu wakubwa

inawahusu hata nyinyi wa kijijini, msikabidhi dada zenu kwa mabazazi wa mjini
Haswaaaa.... Na pia Kama mmewakabidhi Basi waambieni kabisa hao binti zenu kama wanateseka waseme wasiogope kusema
 
Ni wengi tu mbona. Mwingine yupo afande mmoja hivi naye kaoa kijiji cha Salong'we huko Magu Mwanza. Jamaa anapiga, kwanza jamaa mruka njia tu. Anakuja na kahaba hadi nyumbani. Mwishowe kabint kameamua kutoroka na kurud kwao kijijini.

Sababu ni kipondo na umalaya wa huyo mura
Bora na huyo anayejua njia hata akatoroka.... Huyu hata stand ilipo hajui ..... Yaan kanaishia dukani tuu sokoni mwanaume ndo anaenda yeye
 
Yaani wakiona MTU anatoka mjini ameulamba kila MTU anatabasamu na kusema mambo yameiva kumbe wanakuwa wameficha mambo mengi
Saaana..... Hapo wazazi wake wanajua mtoto wao huku mjini anakula good time kumbe Cha Moto anakiona....
Na uyu mwanaume sio kwamba hata Ni Mambo Safi Sana Wala mfano mzuri juzi hapa kwenye sikukuu ya idi msichana Dada ake alimwambia wachange ela elfu kumi kumi watume nyumbani kwao kwa ajili ya sikukuu msichana akawa anaogopa kumuambia mme wake kwamba anaomba elfu kumi ya kumpa mzazi wake kijijin.....
Na hapo alikua anaongea na cm nipo jikoni napika Cha jioni nikasikia maongezi nikajiambia elfu tuuu jamanii mmhh....
 
Kuna falla mmoja alikuwa na hii tabia,siku moja nikamuita.

Nikamwambia arifu eh,siku moja nitakutandika nikupeleke mwenyewe polisi,hunishindi kabisa wewe.
Huyo mtu ana kwao,kama harekebishiki mrudishe.

Siku moja nikampanga binti akasepa,na jamaa akahama kabisa mtaa huo.
Mimi uyu binti natamani awaambie wazazi wake huko kijijin kweli kabisaa
 
Yaan sijui hata nimsaidiaje.... Nlimwambia awaambie nyumbani kwao akaniambia cm yake Haina ela nikampa ela akaweke vocha sijui hata Kama alisema......

Kenyewe kanasema nyumbani kwao wamemuambia ndoa Ni kuvumilia.... Aliniambia ivyo mtoto mwenzie ambao wanashinda wote..... Alaf Sasa saa zingine kanapigwa alaf kanatoka nje kanacheka na kuongea hata hakanuni jamani..... Nyie wanaume nyieee na nyinyi mtazaa tuu watoto wa kike
Mpaka nimelia aisee inaumiza sana

Wanaume mkituoa wadogo mjue na kutulea jamani khaaa!!!

Anamtengenezea tatizo baya mno la kisaikolojia huyo binti, saiv akipigwa hanuni sababu bado mchanga lakini siku akichoka huyo mwanaume ajiandae kwa rangi zote atakazopewa

Hebu msaidie kabla hajaambukizwa ukimwi huyo binti

Hizo ndoa za utotoni na za wazazi hizi ni zigo la misumari kichwani
 
Anamuonea kwa vile mtoto jamani, lakini sio vizuri hata kwa bed nahisi hakaandaliwi kanashtukia mashine inazama tu duh.
Hayo Ni ya ndani siwezi kujua ila Kuna Yale yanayo jionesha kabisa yaani inatia huzuni
 
Si wote bhana, usituaribie wengine mimi ndiyo kwanza naenda kuchumbia lushoto,
Hizi za mjini na wameshajua utamu wa umbea wa instagram huwa zinakuwa ngumu kumeza!
Na huyu ametokea vijiji vya huko huko TANGA ila sio lushoto...... Kenyewe kanasema kalikua kanafanya kazi za ndani wazazi wake wakakaita ili kaje kaolewe
 
Usisahau kurecord ushahidi maana unaweza kwenda kushtaki kwa kumsaidia huyo binti lkn akiitwa akakataa kwamba anapigwa kwa uwoga na familia za vijijini nyingi haziwaskilizi Ke kwaiyo hata akiwaambia ukute hawana msaada wowote,these monsters
Sasa na record ushahidi gani jamaniiii.....

Mungu amsaidie tuu maskini
 
Yuko mafunzoni huyo binti atakuwa binti wa kikurya amekuwa huku akishuhudia vipigo kwa ***** sasa kwa nini yeye asipigwe,
Mhimu kama yuko hapa town fanya juu chini nipate namba yake ili tumzibue masikio,baada ya hapo mmewe lazima ataomba poor
Wala sio mkurya.... Alaf Nia yangu sio azibuliwe masikio Nia yangu Ni asiteseke kwa ndoa yake
 
Mpaka nimelia aisee inaumiza sana

Wanaume mkituoa wadogo mjue na kutulea jamani khaaa!!!

Anamtengenezea tatizo baya mno la kisaikolojia huyo binti, saiv akipigwa hanuni sababu bado mchanga lakini siku akichoka huyo mwanaume ajiandae kwa rangi zote atakazopewa

Hebu msaidie kabla hajaambukizwa ukimwi huyo binti

Hizo ndoa za utotoni na za wazazi hizi ni zigo la misumari kichwani
Ila Kuna mtu kanipa ushauri mzuri Sana pm nitaufanyia kazi..... Mungu akubariki this may work hakika.... Leo jioni nikirudi kutoka kwa shughuli zangu ntafanya Kama ulivyoniagiza Mungu akubariki aisee mkuu
 
Wewe jirani weweeee may thunder strike you.... Shenzi kabisaaa.....

Ipo ivi hapa nnapokaa nna jirani yangu Ni mwanaume alioa mwezi uliopita zile ndoa za ramadhani zile... Sasa kilichonifanya nianzishe Uzi Ni jinsi anavo mtreat mkewe yaan sio sawa kabisa , kwanza binti wa watu ana miaka kumi na Tisa tuu kametolewa kijijini kuletwa mjini Kuja kuteseka kabinti kawatu kanapigwa na ndo kwanza ndoa Haina hata miezi mitatu.... Mwanaume Ni Malaya huyuuu kila nikirudi kutoka kwenye mizunguko yangu namfuma maeneo ya hatari ila najikausha tuu Leo nimeshindea kuvumilia kwakweli maana leo tena kampiga vibao mtoto wa watu kwa kosa la kijinga kabisa.....

Swali langu kwa wanaume wa huku jf wenye tabia Kama hi kwanini ukaoe mtoto wa watu mdogo anaesalimia kwa kupiga goti uje umtese???? SI Bora utafute gume gume za huku mjini tuuu.....

Wito kwa wazazi na wale wenye ndugu zao vijijin msiozeshe mabinti zenu wadogo kwa mwanaume ambae hajajuana nae yaan amekuja tuu kijijin kwa ajil ya kutaftiwa mke tuuu wanakuja kuteseka huku jamani...

Uyu msichana anapenda kajifunika funika kumbe anaficha alama za alipopigwa
Wewe mwanaume wewe naomba Mungu uwe tuu jf uje usome hapa ili angalau uache ujirekebishe
Acha apigwe tu akome kuparamia mjini
 
Kila la heri utuletee mrejesho wa yatakayojiri
Ila Kuna mtu kanipa ushauri mzuri Sana pm nitaufanyia kazi..... Mungu akubariki this may work hakika.... Leo jioni nikirudi kutoka kwa shughuli zangu ntafanya Kama ulivyoniagiza Mungu akubariki aisee mkuu
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom