Wanaume wanaooa au wanaopenda kuoa wanawake wa kijijini ndo waharibifu wakubwa

Wewe jirani weweeee may thunder strike you.... Shenzi kabisaaa.....

Ipo ivi hapa nnapokaa nna jirani yangu Ni mwanaume alioa mwezi uliopita zile ndoa za ramadhani zile... Sasa kilichonifanya nianzishe Uzi Ni jinsi anavo mtreat mkewe yaan sio sawa kabisa , kwanza binti wa watu ana miaka kumi na Tisa tuu kametolewa kijijini kuletwa mjini Kuja kuteseka kabinti kawatu kanapigwa na ndo kwanza ndoa Haina hata miezi mitatu.... Mwanaume Ni Malaya huyuuu kila nikirudi kutoka kwenye mizunguko yangu namfuma maeneo ya hatari ila najikausha tuu Leo nimeshindea kuvumilia kwakweli maana leo tena kampiga vibao mtoto wa watu kwa kosa la kijinga kabisa.....

Swali langu kwa wanaume wa huku jf wenye tabia Kama hi kwanini ukaoe mtoto wa watu mdogo anaesalimia kwa kupiga goti uje umtese???? SI Bora utafute gume gume za huku mjini tuuu.....

Wito kwa wazazi na wale wenye ndugu zao vijijin msiozeshe mabinti zenu wadogo kwa mwanaume ambae hajajuana nae yaan amekuja tuu kijijin kwa ajil ya kutaftiwa mke tuuu wanakuja kuteseka huku jamani...

Uyu msichana anapenda kajifunika funika kumbe anaficha alama za alipopigwa
Wewe mwanaume wewe naomba Mungu uwe tuu jf uje usome hapa ili angalau uache ujirekebishe
Wivu umekujaa mpaka umeota makunyanzi usoni
 
Dada naomba, naomba sana ulifanye hili kwa ajili yangu, iko siku utanielewa. Zungumza vizuri na huyo binti kama mzazi wake, bado ni binti mdogo mno! Ongea nae uangalie namna ya kumsaidia mpaka Ustawi wa Jamii, usiangalie mambo ya kuvunja ndoa ya watu, ni bora ivunjike tu huyo binti abaki salama. Unaweza ukawa unasita kumsaidia hivyo, likampata kubwa zaidi hata kupoteza maisha yake kitu kitakachokutesa maisha yako yote. Msaidie huyu binti dada tafadhali sana
 
Wanawake wengi tu wanapigwa sana na waume zao, only that its not easy to open up.
 
Wewe jirani weweeee may thunder strike you.... Shenzi kabisaaa.....

Ipo ivi hapa nnapokaa nna jirani yangu Ni mwanaume alioa mwezi uliopita zile ndoa za ramadhani zile... Sasa kilichonifanya nianzishe Uzi Ni jinsi anavo mtreat mkewe yaan sio sawa kabisa , kwanza binti wa watu ana miaka kumi na Tisa tuu kametolewa kijijini kuletwa mjini Kuja kuteseka kabinti kawatu kanapigwa na ndo kwanza ndoa Haina hata miezi mitatu.... Mwanaume Ni Malaya huyuuu kila nikirudi kutoka kwenye mizunguko yangu namfuma maeneo ya hatari ila najikausha tuu Leo nimeshindea kuvumilia kwakweli maana leo tena kampiga vibao mtoto wa watu kwa kosa la kijinga kabisa.....

Swali langu kwa wanaume wa huku jf wenye tabia Kama hi kwanini ukaoe mtoto wa watu mdogo anaesalimia kwa kupiga goti uje umtese???? SI Bora utafute gume gume za huku mjini tuuu.....

Wito kwa wazazi na wale wenye ndugu zao vijijin msiozeshe mabinti zenu wadogo kwa mwanaume ambae hajajuana nae yaan amekuja tuu kijijin kwa ajil ya kutaftiwa mke tuuu wanakuja kuteseka huku jamani...

Uyu msichana anapenda kajifunika funika kumbe anaficha alama za alipopigwa
Wewe mwanaume wewe naomba Mungu uwe tuu jf uje usome hapa ili angalau uache ujirekebishe

Hii ni tabia ya kipuuzi sana, hlf huyo jamaa atakuwa ana kasoro anazozificha kupitia mwanamke.

Kwanza kaoa binti mdogo
Pili kaamua kumtoa kijijini
Tatu anampiga

Hizo zote ni dalili za inferiority complex, upuuzi sana
 
Ndo hivyo hawa wanaume hawaaa Mungu anawaona.... Ingekuwa Ni Hawa wanawake wa Mjini hata nisingeshtuka lkn haka katoto hata hakajui haki zake jamani .....

Mfundishe haki zake, Mfundishe namna ya kujitetea.
 
Ipo namna njema zaidi ya hiyo, huyo jamaa ni dhaifu sana
Dogo hawezi mcontrol jamaa.. Jamaa anaona huyo ni mtoto tu hawezi elewa kwa kuambiwa ni kipigoo tuu...!! So hapo either dogo avumilie kipigo au watu wazima waende kuongea na jamaa apunguze kumpiga dogo ila dogo huyo hawezi fanya lolotr kujisaidia labda atorokee
 
Miaka 19 ni mdogo sana.
Pengine hata mwanaume anaongea na vicheche wake mbele yake na hakafanyi kitu.
Huyo mwanaume angenioa mimi ningeshamkata naniii zake nichemshe supu. Nimechukia sana

:D :D :D kumbe kakorofi wewe
 
Wivu umekujaa mpaka umeota makunyanzi usoni
Hahahaaaa poleee Sina kunyanzi hata Moja...... Na Wala Sina wivu Ni kwamba namsaidia tuu huyu binti sijui kesho Nani atanisaidia Mimi ama wanangu ama ndugu zangu upoo
Nafanya tuu Kama sadaka.... Nawewe Kama unatabia izi kaa ukijua tuu kuwa dunia ni mzunguko leo unamfanya mwana wa watu kesho watafanyiwa wanao Tena Mara elfuuuu
 
Dada naomba, naomba sana ulifanye hili kwa ajili yangu, iko siku utanielewa. Zungumza vizuri na huyo binti kama mzazi wake, bado ni binti mdogo mno! Ongea nae uangalie namna ya kumsaidia mpaka Ustawi wa Jamii, usiangalie mambo ya kuvunja ndoa ya watu, ni bora ivunjike tu huyo binti abaki salama. Unaweza ukawa unasita kumsaidia hivyo, likampata kubwa zaidi hata kupoteza maisha yake kitu kitakachokutesa maisha yako yote. Msaidie huyu binti dada tafadhali sana
Nipo kwenye process...... Wala ndoa yake haitavunjika labda tuu Kama mwanaume hata acha upuuzi wake
 
Wanawake wengi tu wanapigwa sana na waume zao, only that its not easy to open up.
Kama Ni Hawa wajanja wa mjini unakuta wana pigwa kwasababu za msingi kabisaaa..... Lkn hiki kitoto noooo kinanyanyasika bure
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom