Wanaume wametutawala muda mrefu bila suluhisho la matatizo mengi, tumuunge mkono Rais Samia atatuvusha

Tangu nchi yetu kupata uhuru tumekuwa chini ya utawala wa wanaume kama wakuu wa nchi, sasa mwanamke amechukuwa kwa mala ya kwanza.

Kwakuwa tumekuwa na matumaini ya kuishi maisha bora bila mafanikio chini ya wanaume basi tumuunge mkono mwanamke tunaweza kuvuka vikwazo vilivyo dumaza maisha yetu kwa muda mrefu.

Kuwa na Rais mwanake kwa nchi yetu ni kama mapinduzi (maana haikutarajiwa) hivyo tuwe na matumain kuwa atafanya mapinduzi ya kweli kiuchumi na kijamii.

Kumuunga mkono ni pamoja na kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake kwake na kwa taifa kwa ujumla. Na serikali ituwezeshe pale tunapohitaji uwezeshwaji.

Landson Tz
Kumbe kuna vita inayoendelea kati ya wanaume na wanawake, okay, ngoja tujiandae.
 
Imagine msiba ulioikuta CCM ungeikuta CHADEMA ikiwa imeshika dola rais angekua Salum Mwalimu🤗

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan💛💚
Kwani salum mwalim na chifu hangaya kuna tofauti gani hapo mama D zaidi ya jinsia.....maana wote ni wale flat heads wa kutokea kule kwenye urojo...hapa watanganyika tukubali tumepigwa.
 
Kwani salum mwalim na chifu hangaya kuna tofauti gani hapo mama D zaidi ya jinsia.....maana wote ni wale flat heads wa kutokea kule kwenye urojo...

Weee acha kulinganisha usingizi na kifo😂😂😂😂

Namheshimu sana Salum Mwalimu na namfahamu vizuri lakini kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania bado hajafikia.

Hata kama atakua na backup kubwa kiasi gani Salum bado.... aendelee kujifunza na kupata uzoefu labda baadae hukoooo
 
Weee acha kulinganisha usingizi na kifo

Namheshimu sana Salum Mwalimu na namfahamu vizuri lakini kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania bado hajafikia.

Hata kama atakua na backup kubwa kiasi gani Salum bado.... aendelee kujifunza na kupata uzoefu labda baadae hukoooo
Kwa mtazamo wangu ni kazi ngumu kuwa CEO wa kampuni kubwa lakini si Urais.

Na hoja ingekuwa ni hiyo basi watu kama kina Mwakyembe, Mwandosya, Mwigulu Nchemba and likes ndio wangepewa nafasi za kugombea kupitia ccm, ni watu wenye cv zimesimama, lakini wenye elimu za hapa na pale ndio wamekuwa wakipewa nafasi.
 
Kumbe kuna vita inayoendelea kati ya wanaume na wanawake, okay, ngoja tujiandae.
simaniishi kuwa kuna vita, nataka hii kuongozwa na jinsia ambayo haijawahi kuongoza nchi yetu. Nina imani na unyenyekevu na busara za mama zinaweza kutusaidia. Wanaume tunakuwa na ubabe mwingi muda tunaharibu mambo. Jambo la msingi ni kumueleza kumtaka mama atekeleze vipaumbele vya jamii.
Aachane na ubabe na ujuaji wa watangulizi wake aunganishe taifa na kulipa uhai uliopotea kwa muda mrefu.
Aongoze CCM, serikali na wananchi wote kwa ujumla kuliletea taifa heshima kwa kujenga na kukuza uchumi na jamii yenye usawa. Ajenge misingi ya demokrasia itayowezesha taifa kujiletea maendeleo.
Jamani mwanamke ndio Rais wetu sasa tuachane na mifumo dume au jike tuhangaike kumaliza matatizo kama umaskini, katiba mbovu n.k
 
simaniishi kuwa kuna vita, nataka hii kuongozwa na jinsia ambayo haijawahi kuongoza nchi yetu. Nina imani na unyenyekevu na busara za mama zinaweza kutusaidia. Wanaume tunakuwa na ubabe mwingi muda tunaharibu mambo. Jambo la msingi ni kumueleza kumtaka mama atekeleze vipaumbele vya jamii.
Aachane na ubabe na ujuaji wa watangulizi wake aunganishe taifa na kulipa uhai uliopotea kwa muda mrefu.
Aongoze CCM, serikali na wananchi wote kwa ujumla kuliletea taifa heshima kwa kujenga na kukuza uchumi na jamii yenye usawa. Ajenge misingi ya demokrasia itayowezesha taifa kujiletea maendeleo.
Jamani mwanamke ndio Rais wetu sasa tuachane na mifumo dume au jike tuhangaike kumaliza matatizo kama umaskini, katiba mbovu n.k
Mind set yako ni indocrinated I am sorry to say and you have a wrong and aggresive attitude and mindset against man.
 
Haya mambo ya jinsi haya yanakoleza vita ambavyo tayari vipo kwenye viunga na makundi ya wachumia tumbo na walevi wa madaraka!

Wanawake wanasiasa, wasomi na wanaharakati wa masuala ya kijinsia wasituchoshe! Naomba kwanza waje na maelezo ya kina kwanini wanawake wapambanaji kule mitaani wanawatelekeza badala yake wanadeal na wadangaji maarufu na wapambe wa wanaume wenye mamlaka?
Hivi wana mbinu zipi za kumkwamua mwananke kama huyu hapa kwenye picha?
Je, wanajua kuwa wao wanapoendekeza kuvuliwa vuliwa huko na kule idadi ya wanawake wapambanaji na walezi wa familia inazidi kuwa kubwa??
Screenshot_20210917-063505.png
 
Kwa mtazamo wangu ni kazi ngumu kuwa CEO wa kampuni kubwa lakini si Urais.

Na hoja ingekuwa ni hiyo basi watu kama kina Mwakyembe, Mwandosya, Mwigulu Nchemba and likes ndio wangepewa nafasi za kugombea kupitia ccm, ni watu wenye cv zimesimama, lakini wenye elimu za hapa na pale ndio wamekuwa wakipewa nafasi.
Kazi ya CEO wa kampuni ni ngumu sana inahitaji vision muweze kuendelea kutengeneza profit ama supernormal profit....... inahitaji ubunifu
uraisi ni mwepesi unaagiza tu ama unaongeza tozo
 
Mind set yako ni indocrinated I am sorry to say and you have a wrong and aggresive attitude and mindset against man.
Haya mambo ya jinsia/jinsi yamekuwa yakijadiliwa mara kwa mara, wakati wanaume haturiziki na yanavyopelekwa ila bunge sheria zinazofanya mwanamme na mke kuwa sawa zinatungwa. Kwani mpaka mwanamke anakuwa makamu wa rais nani alimuleta. Unadhani kuna tofauti kati ya rais na makamu wa rais? Sasa kama haukubali basi tu lakini ndio hiyo. Bora kutuliza akili akasubilia kesho yako yenye matumaini
 
Back
Top Bottom