Troublemaker
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 19,881
- 38,509
Can u mind ur own business?Nilikuwa nasikia zamani wakati ndo tunakua,tunanukia umri wa kuanza kumjua mwanaume,wasichana wanatusimulia wanavyokuwa wanasafiri kwenye mabasi wanakaa sit moja na wakaka wanapiga stori za hapa na pale hadi mwisho wa safari,muda mwingine safari inaishia na matumaini mapya ya mahusiano,yaani unaingia nyumbani unafarijika na zile stories za mkaka yule na cha ajabu ndo mara ya kwanza kukutana ndani ya hilo basi
Siku hizi unaingia ndani ya basi, unabahatika unakaa na mkaka sit moja,safari inaanza,kituo cha kwanza,hamna kitu,cha pili,hamna kitu,cha tatu unajifanya kumuulizia sehemu fulani basi linafikapo SAA ngapi,anajibu tu bado SAA moja
Halafu anarudisha earphone masikioni,anacheza games
Mnakuwa mabubu mpaka mwisho wa safari
Huwa hamtutendei haki kwa kweli
Mkiwa kwenye usafiri hasa mrefu msijifanye bize sana,huwa tunapenda tupige story mbili tatu
Ubize wetu kwenye mabasi huwa ni kupretend tu ,anza mazungumzo uone kama hutajibiwa