Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kuna Mambo sisi wanaume lazima tuyaache na tujue jinsi ya kuwa wasafi.
1. Mtu soksi zinanuka kwa sababu ya kuvaliwa kwa muda mrefu haoni kama ni tatizo
2. Hotelini mtu anasukutua na kutemea mate au kohozi kwenye sink linalotumiwa na watu wote. raha mustarehe
3. Una Soksi ina bonge la tobo kwenye kisigino na kwenye dole gumba lakini bila ya aibu unaivua mbele za watu.
4. Unaingiza dole lako kwenye pua na kutoa Kamasi au ugando wa kamasi bila ya wasiwasi mbele za watu
5. Unafanya kazi Gereji hufui nguo zako hadi tofauti kati yako na Grease za gereji inakuwa sawasawa na Ziro
6. Unajijua una kikwapa lakini kunyoa nywele zako za kwapani inakuwa ni mgogoro mkubwa.
7. Unakula kitimoto, unakunywa bia na vitu vingine kadha wa kadha,lakini mswaki kwako mwiko!
8. Huwezi kuoga mpaka ujue unakwenda kwenye kideti kipya.
9. Domo lako unajua kwamba linanuka lakini wewe ndiyo kinara wa kutaka kunong'oneza watu.
Update:
10. Mtu mkewe akisafiri wiki nzima basi na yeye hatandiki kitanda chake wiki nzima. Huo ni u-smart au ni uchafu?
11. Kila ukikutana na kichochoro au kigiza kidogo, mzee lazima umwage "kojo" tena lenye harufu kali. Jiheshimu!
Hizi ni tabia ambazo baadhi yetu wanaume tunazo ila wengine wanazitetea eti ndiyo "ugumu" jamani tuwe wasafi kwani usafi nao ni sehemu inayochochea mapenzi.
1. Mtu soksi zinanuka kwa sababu ya kuvaliwa kwa muda mrefu haoni kama ni tatizo
2. Hotelini mtu anasukutua na kutemea mate au kohozi kwenye sink linalotumiwa na watu wote. raha mustarehe
3. Una Soksi ina bonge la tobo kwenye kisigino na kwenye dole gumba lakini bila ya aibu unaivua mbele za watu.
4. Unaingiza dole lako kwenye pua na kutoa Kamasi au ugando wa kamasi bila ya wasiwasi mbele za watu
5. Unafanya kazi Gereji hufui nguo zako hadi tofauti kati yako na Grease za gereji inakuwa sawasawa na Ziro
6. Unajijua una kikwapa lakini kunyoa nywele zako za kwapani inakuwa ni mgogoro mkubwa.
7. Unakula kitimoto, unakunywa bia na vitu vingine kadha wa kadha,lakini mswaki kwako mwiko!
8. Huwezi kuoga mpaka ujue unakwenda kwenye kideti kipya.
9. Domo lako unajua kwamba linanuka lakini wewe ndiyo kinara wa kutaka kunong'oneza watu.
Update:
10. Mtu mkewe akisafiri wiki nzima basi na yeye hatandiki kitanda chake wiki nzima. Huo ni u-smart au ni uchafu?
11. Kila ukikutana na kichochoro au kigiza kidogo, mzee lazima umwage "kojo" tena lenye harufu kali. Jiheshimu!
Hizi ni tabia ambazo baadhi yetu wanaume tunazo ila wengine wanazitetea eti ndiyo "ugumu" jamani tuwe wasafi kwani usafi nao ni sehemu inayochochea mapenzi.