Wanaume tukome kuwekeza kwa mahawara!

Bishanga

JF-Expert Member
Jun 29, 2008
15,323
10,050
Hii sms jana mke wa ndugu yangu kaibamba kwenye simu ya mumewe ambaye alisevu jina la mtuma meseji kuwa anaitwa ' Mose fundi bomba':
'Mpenzi leo nimepita madukani Kariakoo.Bei ya vifaa ni hizi: Stima (500,000._), Draya(400,000.-), Stima ya fasho(200,000.-), viti (60,000.-) na sinki(600,000._). Fanya hima kesho (yaani leo) unipatie hizo pesa maana nasikia bei karibu zitapanda.Ukinipa milioni mbili na nusu zitanitosha na kununulia dawa za kuanzia.mmmmmwwwaaaa i love you,ikamalizia hiyo sms.

Wakuu timbwili linaendelea,na tatizo kubwa bi mkubwa mradi wake wa kuku umesimama mzee anasema hana hela na wanaishi nyumba ya kupanga. Kinababa haya mambo ya kuzima moto kwa jirani huku kwetu kunaungua matokeo yake ndo haya.
Nawasilisha.
 
hawa ndo wanatelekeza familia na kuwekeza nyumba ndogo. Wanaume wengi wanajifanya vipofu /viziwi hawajui kuwa mwanamke anakubali mume wa mtu ili amchune. Hakuna mapenzi pale fedha tu
 
hahaha! sasa ntaamini nilisikia mwanamama anaambiwa ' u should never be understanding'. sio unaambiwa sina hela ndo kwanza unampa za upatu mwenzio akapeleke small house. aah, mjini raha sana jamani,kha!
 
Duh huyo mwanaume ni balaa
Nyumba ya kupanga na bado anaambiwa apeleke milioni mbili na nusu
Ni matofali mangapi au ni mifuko mingapi ya cement au si anapata sehemu ya miguu ishirini kw aishirini nje kabisa ya mji wakati akisubiri amalizie bei ya manunuzi
Kweli akili ya kuambiwa changanya na ya kwako
 
Una maana gani!
Mbona unamtuhumu mtu asiye na kosa?
Kosa lake ni kutomsechi bwanake mifukoni, au?
shem anasema sms iliingia usiku mzee akiwa amelala ndo akaisoma na kuifowadi kwenye simu yake.
 
Una maana gani!
Mbona unamtuhumu mtu asiye na kosa?
Kosa lake ni kutomsechi bwanake mifukoni, au?

My bad ......mgonjwa ni ndugu yake.

Itakuwa sikuamini kuwa aliyefanya hivi ni ndugu yake Bishanga. (@-@)
 
mi
Duh huyo mwanaume ni balaa
Nyumba ya kupanga na bado anaambiwa apeleke milioni mbili na nusu
Ni matofali mangapi au ni mifuko mingapi ya cement au si anapata sehemu ya miguu ishirini kw aishirini nje kabisa ya mji wakati akisubiri amalizie bei ya manunuzi
Kweli akili ya kuambiwa changanya na ya kwako

Rocky my friend ukistaajabu ya Musa utayaona ya firauni, haya mambo yanatokea duniani chini ya mbingu hii hii tunayoishi. Hata mimi nimekuwa shocked na ujasiriamali huu wa kuwekeza kwa hawara. Kusoma nisome mimi, kazi nifanye mimi halafu hela zangu aje kuzila lijananke ambalo hata si mama, dada , binti wala mke wangu? This is ridiculous na ma kweli wanaume tunatofautiana!!!!!!!!.
 
Hii sms jana mke wa ndugu yangu kaibamba kwenye simu ya mumewe ambaye alisevu jina la mtuma meseji kuwa anaitwa ' Mose fundi bomba':
'Mpenzi leo nimepita madukani Kariakoo.Bei ya vifaa ni hizi: Stima (500,000._), Draya(400,000.-), Stima ya fasho(200,000.-), viti (60,000.-) na sinki(600,000._). Fanya hima kesho (yaani leo) unipatie hizo pesa maana nasikia bei karibu zitapanda.Ukinipa milioni mbili na nusu zitanitosha na kununulia dawa za kuanzia.mmmmmwwwaaaa i love you,ikamalizia hiyo sms.

Wakuu timbwili linaendelea,na tatizo kubwa bi mkubwa mradi wake wa kuku umesimama mzee anasema hana hela na wanaishi nyumba ya kupanga. Kinababa haya mambo ya kuzima moto kwa jirani huku kwetu kunaungua matokeo yake ndo haya.
Nawasilisha.
Lakini kumbuka kuna theory inayosema usiweke mayai yako yote kwenye kapu moja. Nakumbuka niliambiwa na mwalimu wangu wa portfolio Analysis
 
hah maisha ndivo yalivo

Life cannot just take any course !!!!!! hili nakataa na ndiyo maana vichwa vyetu havina upepo ndani kama mpira bali ubongo tuliopewa na Mungu kufikiri na kufanya maamuzi sahihi1.!!!!
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom