Wanaume njooni huku tukumbushane mambo ya msingi

Brigadier Isaac

JF-Expert Member
Jan 2, 2021
426
1,229
Habari wana JF.

Leo kuna vitu ilinibidi niwaeleze wale wanaume wenzangu wenye akili za miaka ya tisini maana huwa wanapata shida sana kusaivu katika mapenzi kutokana na mabadiliko ya kitamaduni.
Kwanza nianze kuelezea miondoko ya dunia ya sasa ambayo amkuwa teyari kuyakabili:-

Dunia sasa twende bila kupepesa macho inampa mwanamke over power hata akiwa amekosea maana ukiangalia sasa kiukaribu malezi ya mtoto wa kike yanamlea binti kuamini kila kosa analofanya amesababisha mwanaume hichi ndio hupeleke watoto wa kike kufanya makosa makusudi akiamini jamii itamtetea na kweli jamii inamtetea vilivyo wanaume kwa wanawake jumrisha selikali wapo mbele yake wakimngia kifua yoyote atejaribu kumshutumu yani kiufupi miaka ya sasa mwanaume hauna chako japo ukweli unauma ndio bora ukubali tu ili hukuweke huru😂

VITU GANI TUZINGATIE ILI KIDOGO ULINDE MAN POWER YAKO DHIDI NA MIONDOKO HII YA JAMII

1.Kuwa na maamuzi na misimamo yako binafsi katika kila jambo linalotokea katika mahusiano bila kumshirikisha mtu yeyote hata wazazi mwanaume mwenzangu dunia ya sasa siyo ile dunia ukipeleka kesi kwa wazazi au mahakamani mwanamke amekosea basi atakutwa na hatia, No dunia ya sasa kama sio kuneutralize kesi basi utageuziwa kibao wewe mwanaume hapo utaambiwa haumridhishi mara haumtunzi sijui hauko romantiki mashitaka kibao yanageuziwa kwako kama vile wewe ndio mkosaji huku mkeo kazi yake kuongeza chumvi halafu wewe unabaki kusema haaaaa!!! jamani sio kweli😂😂 hakati hapo ungerahisisha mambo kwa mfukuzia kwao bila hata kutaka vikao sijui na wazazi, sijui ushauri wa naninani ila kwa vile bado unahekima za miaka ya tisini unaenda kujizolea dhihaka kama hizi😂😂

2.Acha kujibebesha matatizo yasiyo kuhusu kwa kudhani ndio uwanaume.unajua kuzaliwa mwanaume raha sana sema wanaume wenzangu kinachotuponza tunapenda sifa sana😂 ndio maama tunavihelehele kubeba majukumu na matatizo yasiyo yetu ili tusifiwe wewe kama haumini chukua pen na karatasi anza kuandika shida zote zinazokusumbua halafu chambua shida zinazo kukabil wewe binafsi achana hata na familia yako hapo lazima utakuta karibia matatizo kuanzia asilimia 90 kwenda juu sio yako umejivalisha tu😀

3.Fanya vitu unavyopenda wewe na tunga sheria zako za kuendesha familia au mahusiano yako wewe kama kichwa.unajua vijana wa siku hizi tunaakili za kitumwa sana za kutaka kujua mwanamke anataka nini sijui anapendeleanini ndio maana kila siku sisi ndio wa kufungua nyuzi za kuumizwa tu yote nikutaka kushare mamlaka na mwanamke.kama nilivoeleza point ya pili tuache kujibesha matatizo yasiyo tuhusu kumbukeni hamna certificate ukifa utapewa ukienda mbinguni

4.tengeneza urithi wako mwenyewe.kama nilivyoeleza hapo juu kwamba dunia ya sasa hadi hao watoto wako unao waona wote wapo pamoja na mkeo ndio maana naushauri wanaume tuweke akiba zetu wenyewe hakikisha unajipenda wewe halafu familia yako ifuate ila kama unadhani nashauri ubinafsi utakuja kukumbuka ukiwa kwenye gofu lako la upweke huku mkeo na watoto wako wamekutelekeza kiaina😁

5.Acha kujifanya dhaifu na mnyonge ukizani utapedwa na kuheshimiwa.unajua siku zote mwanaume sio wadhaifu kwa wanawake kama watu wengi wanavyofikiri ila tunapenda kuvaa udhaifu ili tuhuridhishe moyo wa mwanamke.kwa vile mwanamke ni kiumbe mnyonge kama ujuavyo mnyonge apate nafasi yafasi ya kumpunish mwenye nguvu lazima tu atamkamia sana tofauti na mwenye nguvu.sasa utakuta mwanaume mwenzangu eti anakubali kuuza nafasi yake ya mamlaka ili tu haeshimiwe na akubalike na mwanamke.sijui nani aliwaambia mnyonge anamweshimu mnyonge mwezake.

Nadhani mimi nitakuwa nimemaliza ya kwangu basi mimi naruhusu mwingine wakuongezea au wakuuliza swali katika kile kinachomsibu kwa sababu wanaume kusaidiana maana sisi tunaozikana.
 
Nani kakudanganya, Sasa hivi kuna kundi la Vijana wavulana wanakuwa bila maadili , Wabishi haswa, hawa mabinti wenu mnaosema wanalelewa wakijua kila kosa ni mwanaume wacha waje wakutane nao, itakuwa Jinsia Gonganana.
 
Nani kakudanganya, Sasa hivi kuna kundi la Vijana wavulana wanakuwa bila maadili , Wabishi haswa, hawa mabinti wenu mnaosema wanalelewa wakijua kila kosa ni mwanaume wacha waje wakutane nao, itakuwa Jinsia Gonganana.
Mkuu unasemea vijana gani ?kama ni hawa wamtaani sawa nakubali ila hawa walioko chuo wengi kinawakuta nilivyoelezea kwa sababu wengi wao wamekaa kichipsi halafu niwaoga kukabiliana na matatizo
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom