GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,518
- 108,793
AUA MKE KWA KISU KISA WIVU WA MAPENZI
SHINYANGA: Oktoba 11, 2020
Mkazi wa Didia Shinyanga Vijijini, Eliya Paulo Shija (30) anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma ya kumuua Mke wake Mariam Juliasi (26) kwa kumchoma na kisu sehemu za shingoni usiku akiwa amelala akimtuhumu kuwa si mwaminifu katika ndoa yao.
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba, ambayo imesema kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya Saa saba usiku ambapo Eliya alitekeleza mauaji hayo akimtuhumu mkewe anamahusiano na mwanaume mwingine.
“Baada ya kutekeleza mauaji hayo Eliya alijijeruhi kwa kujichoma kwa kisu tumboni na kusababisha utumbo kutoka nje kwa lengo la kujiua kwa sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga na hali yake ni mbaya.” Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba.
uhurudigital
Mwanaume ukiwa na 'Hawara' tena Warembo kamwe huwezi kuwa na 'Umbwiga / Ushamba' na 'Upopoma / Upumbavu' huu kwa Mpenzi / Mkeo.
SHINYANGA: Oktoba 11, 2020
Mkazi wa Didia Shinyanga Vijijini, Eliya Paulo Shija (30) anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma ya kumuua Mke wake Mariam Juliasi (26) kwa kumchoma na kisu sehemu za shingoni usiku akiwa amelala akimtuhumu kuwa si mwaminifu katika ndoa yao.
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba, ambayo imesema kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya Saa saba usiku ambapo Eliya alitekeleza mauaji hayo akimtuhumu mkewe anamahusiano na mwanaume mwingine.
“Baada ya kutekeleza mauaji hayo Eliya alijijeruhi kwa kujichoma kwa kisu tumboni na kusababisha utumbo kutoka nje kwa lengo la kujiua kwa sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga na hali yake ni mbaya.” Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba.
uhurudigital
Mwanaume ukiwa na 'Hawara' tena Warembo kamwe huwezi kuwa na 'Umbwiga / Ushamba' na 'Upopoma / Upumbavu' huu kwa Mpenzi / Mkeo.