Wanaume ni uchoyo au ni roho mbaya? au ni kutokujiamini

Miss Natafuta

JF-Expert Member
Sep 16, 2015
25,470
45,614
Inatokea binti ana rafiki wa kiume rafiki mzuri tu hata muda mwingine anakutongoza ila labda upo unamchunguza kama anafaa au vipi. Ikatokea siku ukakwama kifedha kama rafiki ukamuomba akukopeshe na rohoni mwako unajua kabisa utalipa

Kutoka hapo hata kukutongoza naaacha hata urafiki hataki tena kama huna sema huna sio unakimbia . Kwani ni lazima?

Naomba kuuliza wanaume ina maana kila mwanamke ni mchunaji? Ni kosa wewe kumsaidia rafiki wa kike? Kwani hatukwami sisi? hatuitaji msaada? Mbona mnakwama?? Nyie mbona mnakopa?

Kuna wanawake wengine mpaka akuombe hela kwanza ujue amekuheshimu sana na ukitoa ujue heshima yako inaongezeka mara dufu.

Tabia ya mwanamke hutoijua kwa kukuomba elf 20,au 30 ya kusukia . Anaweza asikuombe kumbe ndani ni mbwa mwitu. Mahusiano mangapi ya watoto wa kishua yapo vibaya? si wana hela wale hawana shida yoyote, Je hawasumbui? Mbona nao wanashindikana?

Kaka zangu rafiki yako akikuomba hela mara ya kwanza kama unayo wewe mpe tu kiroho safi . Usimjudge mtu kwa mambo ya dunia yasiyo na thamani utakuja kupishana na malaika mlangoni kwako kisa hela umkaribishe shetani kisa kuweka akiba isiyo na mlaji
 
Mkuu tatizo sio uchoyo wala kutokujiamini...ILA TUNAWAENZI WAHENGA WETU WALIOSEMA UKING'ATWA NA NYOKA,UTASHITUKA HATA UKIGUSWA NA UJANI
si bora utoe tu hyo hela ili ujue kama huyu nae ni nyoka au vipi mapema? kuliko ukae na mtu kumbe sio .kama elf 50 ya siku moja inaweza kukupa ukweli si bora utoe tu.
 
Tatizo wanawake huwa mnafikiri pesa ni suluhisho la shida zenu, omba maarifa ya kusaka pesa.

Kingine mkikopa kulipa mna tabu sana, mnapenda kutumia udhaifu wetu kama kinga dhidi ya deni. Kwa mwanaume mwenye akili huwa hakopeshi mwanamke ila anatoa kama kusaidia tu and not otherwise.
hata wenye biashara kubwa nao wanakopa muda mwingine.hujui kitu emergency wewe? kukopa hela ni kwamba huna chanzo cha hela?
 
Tatizo wanawake huwa mnafikiri pesa ni suluhisho la shida zenu, omba maarifa ya kusaka pesa.

Kingine mkikopa kulipa mna tabu sana, mnapenda kutumia udhaifu wetu kama kinga dhidi ya deni. Kwa mwanaume mwenye akili huwa hakopeshi mwanamke ila anatoa kama kusaidia tu and not otherwise.
Mkiombwa maarifa hamtoi
 
inatokea binti ana rafiki wa kiume rafiki mzuri tu hata muda mwingine anakutongoza ila labda upo unamchunguza kama anafaa au vipi. ikatokea siku ukakwama kifedha kama rafiki ukamuomba akukopeshe na rohoni mwako unajua kabisa utalipa
kutoka hapo hata kukutongoza naaacha hata urafiki hataki tena
naomba kuuliza wanaume ina maana kila mwanamke ni mchunaji? ni kosa wewe kumsaidia rafiki wa kike? hatukwami sisi? hatuitaji msaada? nyie mbona mnakwama?? nyie mbona mnakopa?
kuna wanawake wengine mpaka akuombe hela kwanza ujue amekuheshimu sana na ukitoa ujue heshima yako inaongezeka mara dufu.
tabia ya mwanamke hutoijua kwa kukuomba elf 20,au 30 ya kusukia .anaweza asikuombe kumbe ndani ni mbwa mwitu.mahusiano mangapi ya watoto wa kishua yapo vibaya si wana hela wale hawana shida yoyote hawasumbui? mbona nao wanashindikana?

kaka zangu rafiki yako akikuomba hela mara ya kwanza kama unayo wewe mpe tu kiroho safi . usimjudge mtu kwa mambo ya dunia yasiyo na thamani utakuja kupishana na malaika mlangoni kwako kisa hela umkaribishe shetani kisa kuweka akiba isiyo na mlaji
Ukisikia jiwe limerushwa kwenye giza na mtu akalia...
 

Similar Discussions

23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom