Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,272
Tunacheza upatu, vikoba, vibubu ni kwa kujikwamua kiuchumi. Kuna mengine tunashindwa kuwaambia maana mkikasirika hamchagui maneno.
Unatumiwa ujumbe nyumbani nyumba inavuja, paa limechoka. Hawana msaada mwingine wanakutegemea wewe. Ukimshirikisha mumeo katika hili, wee usipompigia pasi shati lake utasikia, “shukran huna juzi tu niwebadilisha paa kwenye nyumba ya baba yako”.
Tumeamua, katika ile 5,000 ya mboga unayoacha tunakata 3,000 inaingia kwenye kibubu na inaunganishwa na upatu J’mosi. Hii 2,000 inatosha fungu la dagaa kavu na bamia. Ukirudi unakuta roast ya dagaa na juice ya maembe.
Mnafanya mengi lakini hatuwaambii kwakuwa wengine makoo yenu yako wazi mno.
Unatumiwa ujumbe nyumbani nyumba inavuja, paa limechoka. Hawana msaada mwingine wanakutegemea wewe. Ukimshirikisha mumeo katika hili, wee usipompigia pasi shati lake utasikia, “shukran huna juzi tu niwebadilisha paa kwenye nyumba ya baba yako”.
Tumeamua, katika ile 5,000 ya mboga unayoacha tunakata 3,000 inaingia kwenye kibubu na inaunganishwa na upatu J’mosi. Hii 2,000 inatosha fungu la dagaa kavu na bamia. Ukirudi unakuta roast ya dagaa na juice ya maembe.
Mnafanya mengi lakini hatuwaambii kwakuwa wengine makoo yenu yako wazi mno.