wanaume mnapoogopa kutembea na wake zenu ugonjwa??AMA

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
mi niemjaribu mpaka kwenda hospital kujua hii hali jamani
utakuta mtu kamwoa mkewe kaenda kutoa mahari mwenyewe
akapewa tunda la roho mwenyewe,wakafurahia wenyewe
baya na wengine wakatotoa watoto wao wenyewe
jamani iweje leo hii mkeo ukiwa nae barabarani unamfanya kama yaya
hata wengine ma yaya tunawatoa aout na wake zetu jumapili
sasa hili swala mi nimeona tuliangalie vyema,tuwapende kuwaheshimu wake
zetu...huyo ndio wako kama ulichagua ukaoa ukahisi unaweza rudia too late
mpe heshima zake...inauma unapokutana na mtu alafu unamuuliza mama ajambo aaah yuko uko nyuma
linhgine kwenda maharausini shugulini...jamani tuwakumbuke awa ndio mama zetu jamani hata kama umekutana na nyoka wako...mpe asali akupende
wendeni nao shugulini jamani...na nyie wamama mwache biasahara ya kukaa home kama ma yaya...mumeo anatoka ati naenda sherehe ya kikazi nyoo chomoka nae aamue anaenda aaendi.,..huu utapeli wa kiini macho msiukubali
funga kibwebwe,...
 
Jamani kwenye biblia nimeona tu mke mwema hutoka kwa
bwana .....hili la hawa wanaume washenzi wanaowatesa wake
zao jamani hawa nao wanatokea wapi ndugu zanguni....wapo wanaume
vyerehani kila nguo waanashona wala awachagui bei hawa nao wanatokea wapi
tusaidiane jamani??
 
Mwambie!


Kuongea suala la tendo la ndoa (sex) katika ndoa au kwa mume wako au kwa mke wako ni moja ya topic ngumu sana chini ya jua au katika uso wa dunia.

Kama utakuwa na maongezi au mawasiliano kuhusiana na suala la sex katika ndoa yako maana yake mtakuwa wazuri katika hiyo department.


Wanandoa wengi ambao wamekuwa na tabia ya kuongea kuhusu maisha yao ya sex kwa uhuru na ukweli wamekuwa na maisha mazuri chumbani kwako kwani si rahisi kufahamu mwenzako anahitaji kitu gani hadi umwambie.

Kuwa wakimya kuhusiana na kuongea kuhusu sex na mke wako au mume wako husaidia kuwa wajinga zaidi na wakati mwingine kutoridhishana sawa na uhitaji wa mwili wako au feelings zako.


Hatari kubwa zaidi ni pale wanandoa wanaposhindwa kuongea wenyewe na matokeo yake kutoridhika na kutoridhika ndiko husaidia kukwetua njia ya mmoja au wote kuanza kuangalia nje (kuchepuka)

Firikia wewe ni mwanamke una vitu mume wako akifanya basi huwa unajisikia kusisimka na mwili kuanza kutoa kuwa juicy na kutamani sana sex na mume wako.

Kwa nini usiwe huru ukamwambia kwamba unapenda iwe hivi:


Mwambie!

WAKATI NIMESISIMKA

Natamani mume wangu uwe na wewe unatoa sauti au na wewe uwe unaongea,

Napenda uwe unaongea maneno matamu ya kimapenzi,

Napenda mume wangu nini unakipenda kwenye mwili wangu,

Napenda uniguse (touch) na kunichezea namna hii (onesha),

Napenda ufanye hivi kwenye chuchu na matiti yangu,

Napenda unitazame usoni,

Napenda unichezee kisimi namna hii (mwambie unapenda afanye kwa kutumia nini na namna gani)

Napenda ufanye hivi kwenye G- spot,

Napenda kuchezea uume wako hivi nk


WAKATI WA SEX

Napenda na wewe uwe unaguna na kutoa sauti za kimahaba au uongee maneno matamu na elezea namna unafurahia au unajisikia kuwa ndani yangu,

Napenda uendelee kunibusu namna hii,

Endelea kusisimua kisimi changu namna hii (eleza kwa kutumia nini)

Natamani tunapoanza tuanze kwa mlalo huu na baadae tumalize kwa mlalo (love making position) hii,

Natamani uanze kwa kasi au msuguano wa polepole na baadae haraka zaidi namna hii,

Nioneshe kama na wewe unafurahia,

Nk


UNAPOFIKA KILELENI

Napenda upunguze kasi na kuniacha au napenda uongeze kasi unapoona nakaribia kufika kileleni,

Napenda unikumbatie na kunibusu nk


BAADA YA KUMALIZA SEX

Napenda sana uendelee kubaki ndani yangu hadi tulale usingizi nk,

Napenda unikumbatie huku tunalala,

Napenda angalau mkono wako au mikono yako ibaki mwili mwangu huku tunalala,

Natamani tuendelee kupiga story,

Natamani uendelee kunibusu.


Kumbuka huu ni mwongozo tu kwani kila mwanamke ana mahitaji yake kutoka kwa mume wake jambo la msingi ni kwamba jisikia huru kuongea na mume wako nini unahitaji kabla, wakati na baada ya sex.


Usisubiri eti utafaidi sana sex baada ya kumaliza kusomesha watoto au hadi mfanikiwe maisha au hadi umalize miradi Unafanya kwani itafika Mahali utakuwa na pesa na muda ila energy huna, kalaghe baho!

Maisha ni sasa!
 
Ni Kuwekana Wazi!


Kawaida linapokuja suala la mapenzi opposite attract na the same repel kwa maana kwamba mara nyingi huwa tunavutiwa na strength za mwingine kwa kuwa hufanana na weakness zetu.

Watu ambao hutuvutia sana ni wale ambao huonesha strength katika maeneo ambayo sisi tupo weak.

Ukikutana na mtu wa jinsia tofauti na wewe na mkawa pamoja kwa muda mrefu pamoja na ukavutwa kutokana na strength zake ambazo zinakubaliana kwenye weakness zako penzi huzaliwa na baadae inaweza kuwa ndoa

Ndoa ni kuwekana wazi.

Wakati Bwana harusi na Bibi harusi wanaposimama mbele ya Mhubiri kanisani na kutoa ahadi zao kwa Mungu na wageni wote walioalikwa huwa wanaahidiana kwamba

“Ninakuahidi kukupenda na kukunyenyekea kwa muda wote wa uhai wetu”

Hii ina maana kwamba maharusi huwa wanakazia kwamba kwa kuwa nakubali kiapo chako na unyenyekevu wako kwangu leo basi nitajifunua kwako mzimamzima kuanzia sasa si kimwili tu bali kisaikolojia pia kwani hadi hapa nimejidhihirisha/nimejifunua kwako katika upande ule wa mazuri tu (strength) kuhusu mimi.

Sasa kwa kuwa tunaoana nitajiweka wazi kwako mzimamzima na nina imani kubwa na wewe kwamba utaendelea kunipenda kama nilivyo.

Ndoa ni kuwekana wazi, ni kila mmoja kujidhihirisha kwa mwenzake kama alivyo pamoja na weaknesses zake.

Vitu vyote ambavyo vilikuwa vimejificha wakati wa uchumba hadi honeymoon basi kuanza kwa ndoa vyote huwa mezani juu kwa kila mmoja kuona.

Na hapo ndipo kwenye mtihani wa kwanza wa wanandoa wapya.

Honeymoon siyo residence ya kudumu ya ndoa, baada ya honeymoon (na wengine hata wakati wa honeymoon) wanandoa wapya hushikwa na mshangao wa partner anavyobadilika na kuwa kama mwingine kabisa.

Ukweli ni kwamba unapoona partner wako anaonekana kama mwingine tofauti na yule wa wakati wa uchumba, ukweli ni kwamba sasa matching inaanza, kufahamiana kikwelikweli kunaanza na wenye hekima na busara huwa makini katika kukabiliana na hizo tofauti na kuendelea kusherehekea hizo tofauti kwa upendo na kuvumiliana kwani huwezi kumbadilisha na kumbadilisha ni kupoteza muda wako.

Love may be blind but marriage is a real eye-opener
 
Huwa Bado Nimekasirika!


Swali:

Kaka Mbilinyi,

Asante sana kwa blog hii kwani tunajifunza mambo mengi sana katika ndoa zetu.

Swali langu ni kwamba kila tukiwa na msuguano (fight) mume wangu huniomba tufanye sex ili tusawazishe mambo hata hivyo binafsi hujikuta nimekasirika bado na sina mood na yeye analalamika kwamba bado nina donge moyoni na kwamba hatujayamaliza?

Ni mimi Mama Anon.


Mama Anon.

Kwanza asante sana kwa kuwa msomaji wa hii blog na pia kwa swali zuri ambalo inaonesha mume wako anakuweka kwenye njia panda.

Kila wanandoa wana aina yao ya kumaliza mambo baada ya valangati wengine hata wakimaliza bado hukaa kila mmoja na hasira hadi saa kadhaa au siku kadhaa au wiki, mwezi.

Kawaida wanandoa wakiwa na argument (kitu ambacho hakiwezi kuepukika kwani hata ndoa imara huwa na arguments na tofauti kubwa ndoa nzuri kukiwa na argument wanamaliza na kuendelea na kupendana) kunakuwa na mtazamo negative kila mmoja kwa mwenzake, hata hivyo jambo la msingi ni ninyi wote kujadiliana vile kila mmoja anajisikia na zaidi kila mmoja vile anapenda kuondoa zile negatives zilizo kwenye brain.

Tofauti kubwa kati ya mwanamke na mwanaume ni kuhusiana na namna ya emotions zinavyofanya kazi kwani mwanaume ni rahisi kumaliza mgogoro na kuweza kujihusisha na sex muda huohuo na mwanamke ni ngumu kidogo kwani bado unakuwa hujafunguka bado kihisia ndiyo maana huwa unajisikia bado umekasirika na huwezi kujiingiza kwenye suala la sex.

Baada ya mzozo kwisha ni vizuri kujikumbusha wewe mwenyewe ni vitu gani unavipenda kutoka kwa mume wako ili kubadilisha ubongo wako uondoe negatives kuhusu mume wako.

Kawaida unahitaji mambo mazuri matano ili kusawazisha negative moja kuhusu ubaya wa mume wako (argument).


Ni vizuri kujihusisha katika sex pale ukiona kila kitu kipo shwari na feelings zako zimerudi kwenye mstari kwani sex bila ukaribu ni kuumizana.


Ni muhimu kujadiliana na mume wako namna ambavyo huwa unajisikia baada ya mzozo ili afahamu na zaidi wote kwa pamoja mfurahie ndoa yenu badala ya wewe kujihusisha huku una hasira
 
Mlalo upi?

Baada ya harusi tu nataka nizae mtoto!

Linapokuja suala la mwanamke kupata mimba (ujauzito/ conception) kuna mijadala mingi ipo kuhusiana na mlalo (sex making position/love making position) upi unafaa kwa ajili ya kutengeneza mtoto.

Hata hivyo hakuna mlalo ambao unajulikana au kushauriwa kwamba ndio unafaa duniani hata hivyo kuna maswali mengi ambayo huhusiana na suala zima la tendo la ndoa na kupata mimba.

Je, Baadhi ya milalo ni bora zaidi ya mingine linapokuja suala la kupata mimba?

ingawa kumekuwa na utafiti mdogo kuhusiana na hili suala bado utafiti umekuwa unaonesha kile hutokea wakati wa tendo la ndoa.

Katika zote missionary position (Mwanaume juu mwanamke chini huku wakiangaliana) inaonekana ndiyo inatoa uwezekano mkubwa zaidi kwa kuwa husaidia kuwa na deep penetration huzihakikishe sperms zaidi ya mlango wa uzazi (womb).

Pia mwanamke kuingiliwa kwa nyuma (rear entry) huwezesha positioning ya sperms vizuri kama missionary position.

Je, kama mwanamke natakiwa kulala na si vinginevyo ili kupata mimba?

Wanasayansi wanasema ili kuondoa uwezekano wa sperms kushindwa kuogelea kutokana na gravity hasa mwanamke anapokuwa amekaa au simama juu ya mwanaume. Kama sperms zina afya hakuna tatizo ingawa kama sperms hazing a afya mwanamke anashauriwa kulala wakati wa tendo la ndoa au hata baada ya tendo la ndoa ili sperms kufikia target.

Je kuna muhimu wowote kufika kileleni (orgasm) ili kupata mimba?

Ni dhahiri kwamba mwanaume ni vizuri afike kileleni (mshindo) katika process ya “baby making” ili kuhakikisha anazipa sperms speed inayotakiwa kufika kwenye target. Utafiti wa karibuni unaonesha pia mwanamke ni vizuri afike kileleni ikiwezekana wakati mmoja na mume wake kwani contractions zinapotokea husaidia sperms kufikia mji wa uzazi.

Je, kama ninataka mtoto wa kike au kiume mlalo gani unafaa?

Suala la milalo halina uhusiano na jinsia ya mtoto bali timing na frequency ndiyo muhimu kwa kusababisha jinsi ya mtoto.
 
Nimechoshwa!


Je, unajisikia frustrated linapokuja suala la sex katika ndoa yako?

Ukweli lazima uongelewe na kuna ulazima wewe unayesoma sasa hivi kujibu na kuwa mkweli.

Kama jibu lako ni NDIYO basi swali la pili ni kwa nini upo frustrated?

Hebu tuangalia sababu kubwa tatu za msingi

Kwanza inawezekana umekuwa na matarajio yasiyo halisi,

Pili inawezekana kuna uchoyo na ubinafsi au umimi,

Na tatu inawezekana humuelewi mwenzi wako.

Hapo ndipo kwenye source ya matatizo ya mume na mke chumbani kama kungekuwa hakuna unrealistic expectation usingekuwa unakuwa disappointed na hali ya mapenzi na mume wako au mke wako

MATARAJIO YASIYO HALISI

Baadhi ya njia za kukuwezesha kuondoa matarajio yasiyo halisi na kuondoa frustration ni pamoja na kuondokana na matumizi ya mikanda ya ngono ambayo wanandoa wengi hutumia eti kujifunza.

Hii ni pamoja na kuangalia pornography.

Video za ngono hazielezei maisha halisi ya mapenzi katika ndoa na kuangalia kunakufanya ujiweke katika kundi la failures kwani hakuna mwanamke ambaye yupo na afya njema kihisia anaweza kufanya kama wanavyofanya Wanawake wa kwenye mikanda (porno) kwani wao wanafanya business na wanaigiza.

Porn stars wao wanatengeneza pesa kwa kuigiza na kuwakamatisha wanaume wenye tama na ni laana ya mapenzi (intimacy).

Biblia inafundisha kutoa ndiyo msingi kwa ajili ya kufurahia mahusiano ya ndoa. Ili kufurahia tendo la ndoa kwanza huanza kwa upendo wa kweli na upendo wa kweli ni kwanza kumpa au kufanikisha mahitaji ya mwenzi wako kwanza na wewe baadae.

UCHOYO NA UBINAFSI

Kama wewe ni mchoyo, mbinafsi (selfish), maisha yako yatakiwa balaa, huwezi kukwepa kuwa na frustrations linapokuja suala la sex na mwenzi wako.

Kwani mzunguko wa maisha yako ni kujipa raha wewe tu na kila kitu kuvutia kwako na si mwenzi wako.

Mtazamo wa aina hii ni adui na huweza kuharibu ukaribu wa mapenzi baina ya wanandoa.

Kuwa karibu kimapenzi (intimacy) kwa wanandoa huweza kusababisha kuwa na sex inayoridhisha na pia maisha bora kwa kila mwanandoa.

Jambo la msingi unahitaji kubadilika kabla huharibu ndoa yako kwanza jikubali kwamba wewe ni selfish na anza kumpa priority mke wako au mume wako kwanza.


Pili lazima uwajibike kwa yule unampenda yaani mke wako au mume wako na kubali kubadilika inawezekana.

Na mwisho confess kwamba umekosa na sasa unaanza plan mpya maisha mapya.

KUTOMWELEWA MWENZI WAKO

Sababu kubwa ya wengi kuwa frustrated na ndoa kimapenzi ni suala la kutomfahamu vizuri mke au mume.

Ukiwa na mtazamo kwamba mke wako au mume wako ana mahitaji sawa ya kimapenzi kama wewe basi hilo tayari ji tatizo kubwa.

Mungu alituumba tofauti kati ya mwanamke na mwanaume na lazima mahusiano yetu yakubaliane na hiyo design ambayo Mungu aliiweka.

Kumbuka mahitaji ya mwanamke na mwanaume ni tofauti na ni muhimu kila mmoja kutimiziwa mahitaji yake.

Mwanamke huhitaji LOVE na mwanaume huhitaji RESPECT
 
Nitajuaje tunafanana kitandani?


Mimi ni kijana wa kiume naishi Arusha kwanza nashukuru sana kwa masomo ambayo tunajifunza kupitia blog yako swali langu la msingi ni kuuliza hivi “Kama huruhusiwi sex kabla ya ndoa, je nitajuaje ninayeoana naye tunafanana katika kiwango cha kuhitaji sex?”

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Kaka nashukuru sana kwa swali lako zuri ambalo linaonekana ni kama mtego, na kibinadamu linaonekana kama lina hekima fulani hivi hata hivyo mbele za Mungu ni swali rahisi mno.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Jambo la msingi kwenye swali lako ni kukuuliza wewe mwenyewe ni kipi kigumu hapo? Unataka kujua kiwango kwa kufanya sex au kwa sharing ya mawazo na ukaribu kufahamu anajisikia vipi au unajisikia vipi kuhusiana na suala zima na ninyi kuwa pamoja.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Kuna mambo makuu mawili kwenye swali lako yaani tamaa ya mwili na upendo wa kweli ambao hubebwa na uvumilivu, subira na imani katika Mungu na kumpenda mtu kwa ndani na si mwili tu.

Je ukitembea naye (sex) ndipo utajua mnafanana uhitaji wa sex? Au kukaa naye na kuongea naye na kushare ndoto mawazo na feelings kutakusaidia kufahamu ni mtu wa aina gani.



Unaweza kufahamu kufanana kwa kiwango cha sex kwa sharing ya kimawazo na hisia katika kuwasiliana kwenu na si kwa kupeana mwili.



Kupeana sex kabla ya ndoa hakuwezi kutatua tatizo lolote au kuwa jawabu la kuwasaidia kujuana kama mpo mnafanana kwenye suala sex baada ya ndoa.



Kupeana sex kabla ya ndoa huweza na husaidia kufunika matatizo kati yenu na hayo matatizo huweza kuwa juu ya meza baada ya ule upendo wa kwanza (illusions, fall in love) kwisha.

Na kinachotokea ni kwamba baada ya kupeana mwili na fall in love kwisha unachobakiwa ni mtu ambaye humjui kabisa.



Jambo la ajabu lingine ni kwamba vijana wengi wa leo hawana lolote, akiona mpenzi wake anasuasua basi wanahongana kwa sex ili warudiane (eti kuleta connection upya) ukweli ni kwamba hiyo connection ni ya mwili tu na ni kwa muda mfupi.



Hata hivyo kuweka msingi wa mahusiano ya ndoa kwa kipengele cha kufanana kwa uhitaji wa sex ni hatari kubwa kwani ndoa ni zaidi ya kupendana na mapenzi.



Kama ukisubiri sex hadi ukiolewa au kuoa suala la kufanana kwa kiwango cha kuhitaji sex itakuwa si tatizo kwani utakuwa hukuwa na uzoefu wowote ambao unaweza kuulinganisha, kwani uzoefu wote huwa baada ya ndoa na baada ya ndoa tayari ni mke na mume, wote mpo wapya.



Kwa ufupi ukiona umefanya sex kabla ya ndoa yafuatayo huweza kutokea

Kwanza uchumba unaweza kuvunjika muda wowote,

Pili uliyenaye anaweza kukwambia anataka kumuoa au kuolewa na bikira

Tatu unaweza usiwe mtu wa furaha katika ndoa yako,

Nne unaweza kuachwa baada ya ndoa.

Tano unaweza kuanza kutoka nje ya ndoa (adultery)

Sita unaweza kudanganywa kwa kuolewa au kuoa kwa sababu potofu.

Saba unaweza usifurahie mapenzi katika ndoa yako.

Nane unaweza kujisikia hatia (guilt) katika ndoa yako.



Mwisho ni wazo zuri sana kusubiri sex hadi ukioa au kuolewa na yule unataka kuoana naye na kuishi naye maisha yako yote. Kwa njia hii wote mtafurahia uzoefu mpya kabisa pamoja na ni kweli hicho kitendo kitakuwa so special hasa ukizingatia kwamba kila mmoja alivumilia na kusubiri kwa muda mrefu hadi mmeoana.



Ni kweli sex lilikuwa wazo la Mungu na Mungu aliumba sex na sex ni kitu kizuri, tatizo linakuja pale binadamu anapo distort na kukataa standards halisi ambazo Mungu ameweka na matokeo yake ni uharibifu na matatizo.

Hivyo tunaweza kuchagua kufanya mambo katika njia ya Mungu na tukabarikiwa au tukachagua kufanya kwa njia zetu zilizopotoka na tukaangamia

Mithali 16:25
 
Ananitaka!


Kaka Mbilinyi,

Mimi ni binti wa miaka 28 nimepata mchumba ambaye sasa ni miezi 4 tangu tumefahamiana na tatizo kubwa ambalo naomba msaada ni kwamba huyu mchumba wangu sasa ameanza kunitaka mapenzi (sex) kabla ya kuoana na mimi ninampenda Mungu na pia nampenda mchumba wangu anioe sasa nifanyeje?

Dada Herieth,

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Dada Herieth,

Asante sana kwa swali zuri ambalo naamini akina dada wengi hujikuta wapo njia panda katika kutoa uamuzi kuhusiana na wanaume wa aina hiyo ya kwako.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Suala la sex kabla ya ndoa na Yule unategemea atakuoa au kuolewa naye mara nyingi ni kutembea na mume ambaye atakuwa mume wa mwenzako kwani akishatembea na wewe uwezekano wa kukuacha unakuwa mkubwa zaidi.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Mwanaume makini na mwenye upendo wa kweli hata kama utasafiri kwenda sayari ya Mars au North pole bado atakuwa tayari kusubiri na kuvumilia kufanya mapenzi na wewe hadi ndoa kwanza.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Kufanya sex ni kujuana, na ukishamjua mtu basi amekwisha, zawadi kubwa ambayo mwanaume huweza kumpa mwanamke anayempenda ni kuvumilia hadi siku wakioana au kufunga naye ndoa kwanza ndipo sex.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Pia wanaume wanajua mwanamke wa kuchezea na mwanamke wa kuoa, mwanamke wa kuoa huwa hakubali kuchezewa mwili hadi siku aolewe (precious woman) na mwanamke wa kuchezea ni Yule mwanaume akimtishia kidogo kwamba sikuoi kama hunipi nionje (mwanamke rahisi au cheap) atakubali yaishe, anajifariji eti wanaume siku hizi hawapatikani!

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Ni mwanaume gani duniani na akili zake au busara zake atakubali kuoa mwanamke rahisi, cheap?

HAKUNA


Ni saikolojia ya mwanaume akishamjua mwanamke hasa kabla ya ndoa kuachana naye na kutafuta Yule ambaye atafaa kumjua (SEX) baada ya ndoa.

Thamani ya mwanamke hupungua sana baada ya kufanya mapenzi (sex) na mwanaume kabla ya ndoa na ni sababu tosha kwa mwanaume kutafuta mwanamke ambaye ataoana naye kwanza then sex.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Hata kama mwanaume atamshauri mwanamke waishi pamoja kwanza ndipo wafunge ndoa kwa maana ya kujuana kwanza ndipo wafunge ndoa, bado si ticket ya kwamba atakuoa bali ni kukuchezeana tu kwani hana ahadi wala kifungo kinachomfunga au kinachokulinda wewe, hapo mnafanya uasherati tu!.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

KUMBUKA!

Kabla ya kuolewa huna commitment or covenant yoyote na mwanaume anayekwambia anakupenda na baada ya ndoa kunakuwa na commitment na covenant au agano/ahadi nzito ambayo mwanaume huitoa mbele za Mungu, watumishi wa Mungu, ndugu zake na ndugu zako, marafiki na jamaana kukubali kuishi na wewe katika maisha yake yote hadi kifo.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Kabla ya ndoa chochote kinaweza kubadilishwa na baada ya ndoa hakuna kinachoweza kubadilishwa.

Baada ya ndoa huwezi kubadilisha mawazo au maamuzi au hisia kuhusu kuoana.


Unafanya sex ukijua kwamba hajakuoa, ndio ukweli, kujisikia atakuoa hakuwezi kukufanya uwe umeolewa; na kufanya sex hakukufanyi uwe umeolewa, kinachofanya uwe umeolewa ni ahadi zenu wawili mbele za watu, kanisa na Mungu kwamba mnataka kuishi pamoja kama mke na mume hadi kifo kitakapowatengenisha.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Wakati wa ndoa wawili mnatoa ahadi kwa Mungu na baina yenu na mbele ya kanisa ambao ni mashahidi.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Kabla ya ndoa hakuna ahadi mbele za Mungu wala mbele za mashahidi hata kama amekuvalisha pete ya uchumba (engagement) inayong’aa kama dhahabu zilizotumika kujenga hekalu la mfalme Suleman au hata kama anakwambia anakupenda from earth to the moon, unadhani kumpa mwili wako kabla ya ndoa ndo kuolewa au hawezi kukuacha, utajuta bure!

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Akishafanya sex na wewe anakuwa tayari ameshajua wewe ni wa ladha gani na jinsi unavyozidi kumpa ndivyo anazidi kukinai na kuhitaji mwingine ambaye ni mke wa kuoa.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Anajua kabisa kwa kuwa mmevunja amri kubwa ya Mungu ya kufanya mapenzi kabla ya ndoa hutamwamini kabisa baada ya kuoana kwani anajua utakuwa unawaza na kujiuliza swali kwamba; kama aliweza kuvunja sheria za Mungu kabla ya ndoa, je si anaweza kutembea na mwanamke mwingine hata katika ndoa?.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Biblia inakataa sex kabla ya ndoa hata kama ulimwengu unaona sahihi ila ndani ya nafsi yako wewe mwenyewe ni shahidi kwamba ni makosa.


Kufanya mapenzi na mwanaume ambaye amekuahidi kukuoa hakufanyi uwe hujavunja sheria hata kama mnasali sala tano kwa siku, ukweli unabaki palepale kwamba hata mkiingia kwenye ndoa hamtaaminiana tena.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Kumbuka msingi wa nyuma au ndoa hujengwa kwenye uchumba na kama kwenye uchumba mmeanza kwa kuvunja sheria basi hata kwenye ndoa itakuwa kila mmoja kuvunja sheria kwa kwenda mbele.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Afadhari uachwe hujafanya naye sex kuliko kuachwa huku umefanya naye sex ni aibu, ni maumivu, ni uchungu na kuchezewa mwili na utu wako kusiko tamkika.

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Wakati mwingine unaachwa na magonjwa au mimba na kupoteza utu wako na heshima yako na pia ni kama label ambayo utatembea nayo katika maisha yako kwamba wewe ni failure!

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->

Hata hivyo habari njema ni kwamba bila dhambi hakuna msamaha na tunaye mwokozi ambaye tukimuomba msamaha yeye hutusaheme na kutuondolea dhambi zetu zote.

(1Yoh: 2:1-2)

<!--[if !supportEmptyParas]--> <!--[endif]-->
 
Unatimiziwa?

Dada Jelisa yeye anasema mahitaji yote anatimiziwa na mume wake.

MAHITAJI MUHIMU KATIKA MAHUSIANO YOYOTE YA KIMAPENZI

Ni kitu cha msingi sana kuhakikisha katika mahusiano mahitaji yako yanajulikana na kueleweka kwa mwenzako.

Mahitaji yako yakijulikana na kutekelezwa kawaida unajisikia vizuri na kujiona upo salama katika hayo mahusiano iwe ndoa au uchumba.

Partner wako hawezi kusoma mind (wanaume mara nyingi tunasoma magazeti na si nini mwanamke anawaza kichwani) na kujua mahitaji yako, ndiyo maana kuna wakati unahitaji wewe mwenyewe kumueleza ili aweze kukupa kile unahitaji, ingawa ni kweli wapo ambao wameshakata tamaa kabisa kwamba hata nikimwambia najua hatafanya, bado hilo si jibu kwani jambo la msingi ni wewe kuongea na mpenzi wako na kumueleza nini unahitaji kutoka kwake tena kwa busara na hekima au kwa upendo.

Mahitaji muhimu katika mahusiano ya ndoa yamegawanyika katika sehemu kuu tano nazo ni

Mahitaji ya kihisia (emotional)

Mahitaji ya Kimwili (physical)

Muhitaji ya kijamii (social)

Mahitaji ya kiroho (spiritual)

Mahitaji ya kiusalama (security)

Mfano wa muhitaji ya kihisia ni kama ifuatavyo

Hitaji la kusikia na kuambiwa unapendwa, una thamani kwa mpenzi wako, kujisikia wewe ni muhimu katika maisha yake, kujisikia wewe ni mali yake, hitaji la kujisikia unaheshimiwa wewe binafsi na yeye, hitaji la kujisikia mpenzi wako anakuhitaji zaidi ya kazi zingine unazofanya kama kulea watoto nk, hitaji la kujisikia wewe ni mtu wa kwanza kwake kwa kila kitu, kujisikia wewe ni mtu maalumu kwake, hitaji la kujisikia unaaminiwa, unakubalika na pia anakupenda na kukuhitaji, hitaji la kujisikia ana appreciate kwa jinsi ulivyo na unavyofanya nk

Mfano wa muhitaji ya kimwili ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kuguswa (touched and caressed), kupata busu, kukumbatiwa, na kushikwa hata kubebwa akiweza, hitaji la kujiona unaruhusiwa kuwa naye katika faragha yake, kujisikia huru kuwa naye kimwili pale unapo muhitaji, kujisikia wewe ni sehemu yake pale mnapowasiliana na watu wengine, kutiwa moyo, kuwa na tendo la ndoa linalokuridhisha kama upo kwenye ndoa.

Mfano mahitaji ya kiroho ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kuheshimiwa na kusaidiwa mambo yako ya kiroho, kuheshimiwa kwa tofauti za kiroho zilizopo.

Kuwa na wakati wa pamoja kuomba pamoja huku mmekumbatiana au kushikana mikono na kuwa kitu kimoja kwa Mungu wenu.

Mahitaji ya kihisia (tukuto) ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kupenda na kupendwa.

Hitaji la kuwa mali ya mume wako au mke wako na kuwa na maana ya maisha pamoja naye.

Hitaji na kujiamini (self positive image)

Hitaji la kuwa na usiri yaani kuwa mwenyewe bila kuingiliwa (privacy)

Mahitaji ya kijamii ni kama ifuatavyo:

Hitaji la urafiki na mke au mume pamoja na wengine wanaowazunguka.

Hitaji la uhuru wa kujihusisha na masuala ya jamii bila kukatazwa na mke au mume.

Mahitaji ya kiusalama ni kama ifuatavyo:

Hitaji la kujisikia salama na hatari yoyote.

Hitaji la kujisikia salama kwamba mahitaji yote katika ndoa yanatimizwa
 
Pesa au Penzi?
Pesa au Penzi?


Huwezi kuongelewa mapenzi bila kutaja suala la pesa. Wapo watu ambao wanaamini kuwa na pesa nyingi, nyingi kabisa za kutosha husaidia pesa kuwa imara na linaloridhisha.


Hata hivyo tumeona penzi la uhakika hata wakati pesa zikiwa hazipo au tumeona penzi la kweli hata katikati ya umaskini uliokithiri.


Hii haina maana kwamba pesa siyo muhimu, pesa ni muhimu sana. Na pesa ina umuhimu kwa kila mahusiano hata, hivyo inabidi ujiulize mwenyewe je, upo kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.

Utakuwa mtu wa maana sana kama utakuwa unatazama na kuwekeza kwenye penzi la kweli na si pesa.


Pia ni vizuri kuwa makini na mtazamo wa mpenzi wako je yupo kwako kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.

Mtazamo wake kuhusu pesa ni muhimu sana


Huwezi kuongelewa mapenzi bila kutaja suala la pesa. Wapo watu ambao wanaamini kuwa na pesa nyingi, nyingi kabisa za kutosha husaidia pesa kuwa imara na linaloridhisha.


Hata hivyo tumeona penzi la uhakika hata wakati pesa zikiwa hazipo au tumeona penzi la kweli hata katikati ya umaskini uliokithiri.


Hii haina maana kwamba pesa siyo muhimu, pesa ni muhimu sana. Na pesa ina umuhimu kwa kila mahusiano hata, hivyo inabidi ujiulize mwenyewe je, upo kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.

Utakuwa mtu wa maana sana kama utakuwa unatazama na kuwekeza kwenye penzi la kweli na si pesa.


Pia ni vizuri kuwa makini na mtazamo wa mpenzi wako je yupo kwako kwa ajili ya pesa au kwa ajili ya penzi la kweli.

Mtazamo wake kuhusu pesa ni muhimu sana
 
Mtimizie!

Kazi si kuoana kazi ni kutimiziana mahitaji bila kuchoka!

Ndoa ni kazi.

Inayochukua muda, jitihada na commitment na wakati mwingine huhitaji professional counselling.

Kama umefika Mahali ambapo wewe na mume wako au mke wako hamuwezi hata kuwasiliana (kuongea) bila kuvurugana (fight) na umeanza kufikiria kuachana kama njia bora zaidi basi unahitaji msaada kwani kuachana bado si jibu la matatizo yote.


Katika ndoa mwanaume na mwanamke ni tofauti na kila mmoja ana mahitaji muhimu ambayo ni lazima mwenzake ayatimize na kutotimizwa hayo mahitaji husaidia kukwetua njia ya kila mmoja kutoridhika na mwenzake.


Kwa ufupi mahitaji muhimu ya mwanaume (yale anapenda mke wake amtimizie) ni kama ifuatavyo

HITAJI LA KURIDHISHWA KIMAPENZI (SEX).

HITAJI LA KUBURUDISHWA, RAHA, KUSTAREHE, KUPUMZIKA, NAFASI YA KUPUMUA, BURUDANI.

HITAJI LA KUWA NA MKE ANAYEVUTIA.

HITAJI LA KUWA NA AMANI NA UTULIVU.

HITAJI LA KUAMINIWA, KUHUSUDIWA NA KUHESHIMIWA.


Mahitaji ya mwanamke katika maisha ya ndoa (vile mwanamke anapenda mume amfanyie au kumtimizia) ni kama ifuatavyo:

HITAJI LA UPENDO, KUPENDWA, MAHABA NA HURUMA.

HITAJI LA MAONGEZI, MAZUNGUMZO, MISEMO, POROJO, KUSIMULIANA NA SOGA.

HITAJI LA UKWELI, UADILIFU, KUAMINIANA, UNYOFU, WIMA NA UWAZI.

HITAJI LA UHAKIKA WA KIFEDHA, AMANA KIFEDHA, UHAKIKISHO KIFEDHA, ULINZI KIFEDHA, USALAMA KIFEDHA, UTHABITI NA AMANI KIFEDHA.

HITAJI LA KUJITOA KWA AJILI YA FAMILIA.


Kwa ufafanuzi ni kwamba mwanamke hupenda mume akimaliza kazi jioni kwanza ajithidi kuwahi nyumbani ili ale chakula (supper/dinner) na mke na watoto, akae na mke na kuongea masuala ya familia kama watoto, matumizi ya fedha nk na hupendelea baba kutumia muda na watoto na mke na si kuangalia TV.


Mume naye hupenda anaporudi kazini mke ampe angalau dakika 15 apumue ndipo aanze kuuliza maswali na kuelezea siku ulivyokuwa na ikifika muda wa kulala mke aanzishe kwamba anahitaji tendo la ndoa.
 
Ina aminika kuna mzungu mmoja kashuka Bongo toka Australia na ameingia na mafua makali sana eneo la mgodini. Habari za kuaminika zinasema jamaa ana mafua ya ndege. Imekuwa ni hali tete hasa baada ya wasemaji kuonekana kugwaya kusema chochote licha ukweli kwamba watu kadhaa wamelazwa Hospitalini.
Leo kuna tangazo linasema kuna ugonjwa wa mafua umeingi bila kufafanua chochote. Tangazo lilienda mbali zaidi na kusema ilikuepuka maambukizo watu wanatakiwa kunawa mikono, kuacha kula vitu hovyo.....
Hivi jamani watanzania tumekuwa watu wa aina gani??
 
Nimechoshwa!


Je, unajisikia frustrated linapokuja suala la sex katika ndoa yako?

Ukweli lazima uongelewe na kuna ulazima wewe unayesoma sasa hivi kujibu na kuwa mkweli.

Kama jibu lako ni NDIYO basi swali la pili ni kwa nini upo frustrated?

Hebu tuangalia sababu kubwa tatu za msingi

Kwanza inawezekana umekuwa na matarajio yasiyo halisi,

Pili inawezekana kuna uchoyo na ubinafsi au umimi,

Na tatu inawezekana humuelewi mwenzi wako.

Hapo ndipo kwenye source ya matatizo ya mume na mke chumbani kama kungekuwa hakuna unrealistic expectation usingekuwa unakuwa disappointed na hali ya mapenzi na mume wako au mke wako

MATARAJIO YASIYO HALISI

Baadhi ya njia za kukuwezesha kuondoa matarajio yasiyo halisi na kuondoa frustration ni pamoja na kuondokana na matumizi ya mikanda ya ngono ambayo wanandoa wengi hutumia eti kujifunza.

Hii ni pamoja na kuangalia pornography.

Video za ngono hazielezei maisha halisi ya mapenzi katika ndoa na kuangalia kunakufanya ujiweke katika kundi la failures kwani hakuna mwanamke ambaye yupo na afya njema kihisia anaweza kufanya kama wanavyofanya Wanawake wa kwenye mikanda (porno) kwani wao wanafanya business na wanaigiza.

Porn stars wao wanatengeneza pesa kwa kuigiza na kuwakamatisha wanaume wenye tama na ni laana ya mapenzi (intimacy).

Biblia inafundisha kutoa ndiyo msingi kwa ajili ya kufurahia mahusiano ya ndoa. Ili kufurahia tendo la ndoa kwanza huanza kwa upendo wa kweli na upendo wa kweli ni kwanza kumpa au kufanikisha mahitaji ya mwenzi wako kwanza na wewe baadae.

UCHOYO NA UBINAFSI

Kama wewe ni mchoyo, mbinafsi (selfish), maisha yako yatakiwa balaa, huwezi kukwepa kuwa na frustrations linapokuja suala la sex na mwenzi wako.

Kwani mzunguko wa maisha yako ni kujipa raha wewe tu na kila kitu kuvutia kwako na si mwenzi wako.

Mtazamo wa aina hii ni adui na huweza kuharibu ukaribu wa mapenzi baina ya wanandoa.

Kuwa karibu kimapenzi (intimacy) kwa wanandoa huweza kusababisha kuwa na sex inayoridhisha na pia maisha bora kwa kila mwanandoa.

Jambo la msingi unahitaji kubadilika kabla huharibu ndoa yako kwanza jikubali kwamba wewe ni selfish na anza kumpa priority mke wako au mume wako kwanza.


Pili lazima uwajibike kwa yule unampenda yaani mke wako au mume wako na kubali kubadilika inawezekana.

Na mwisho confess kwamba umekosa na sasa unaanza plan mpya maisha mapya.

KUTOMWELEWA MWENZI WAKO

Sababu kubwa ya wengi kuwa frustrated na ndoa kimapenzi ni suala la kutomfahamu vizuri mke au mume.

Ukiwa na mtazamo kwamba mke wako au mume wako ana mahitaji sawa ya kimapenzi kama wewe basi hilo tayari ji tatizo kubwa.

Mungu alituumba tofauti kati ya mwanamke na mwanaume na lazima mahusiano yetu yakubaliane na hiyo design ambayo Mungu aliiweka.

Kumbuka mahitaji ya mwanamke na mwanaume ni tofauti na ni muhimu kila mmoja kutimiziwa mahitaji yake.

Mwanamke huhitaji LOVE na mwanaume huhitaji RESPECT

kuna umuhimu wa invisible kuanzisha jukwaa la wanandoa.jukwaa ambalo ku-acce$s ni lazima uattach kopi ya certificate of marriage kwa invisible.kinyume na hilo,tunawatisha wakina fidel na gp ambao hawajaoa.wanaweza kudhani ndoa ni ngumu sana.USHAURI BINAFSI JAMANI
 
Naona leo mkuu wangu umekuja "kivingine".umesababisha nianze bia na wisk mapemaaa kwenye thread ya vituko vya ATC.hapa nimeshalewa kwa sababu yako...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom