The Donchop
JF-Expert Member
- Jan 10, 2014
- 294
- 376
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Mimi ni mwanamke mtu mzima (wengi uwa wanachanganyikiwa na hii jina wakidhani ni mwanaume.) Nilikua na mpenzi wangu toka october 2014 na mpaka sasa.
Kwenye mapenzi kuna raha na karaha. Mwanzo tulipendana sana kiasi cha mwenzangu kutambulika kwenye ukoo wa mwenzangu pasipo sisi wenyewe kutambulishana rasmi. Pengine ni kwa sababu wakwe watarajiwa ni majirani na pia tunakutana sana kwenye shughuli za kijamii.
Mwaka 2016, tuligombana na mwenzangu. Lakini kila mmoja akiwa bado ana mapenzi na mwenzie. Lakini kila nilipojaribu kusimamia kisolvu tatizo mwenzangu ndiye aliyeleta shida. Leo siwezi kuingia kwa undani juu ya ugomvi sababu si muhimu kwa mada hii ila ni ugomvi wa kawaida sana ambao mnaweza kuelewana na maisha yakaendelea.
Mwenzangu akaamua kusikiliza watu wa nje waliompa ushauri kuwa ni bora aachane na mimi. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuachwa na ninaempenda. Nililia. Niliomba msamaha pasipo kujua kosa. Nilihangaika sana.
Mwenzangu hakujali wala kunionea huruma. Ndio kwanza akaendelea kunituhumu hadi kwa sifa za uongo. Akaenda mbali zaidi na kusema hawezi kurudi labda amdate mama yake. Kitu cha mwisho kabisa, aliamua kunichafulia kwa ndugu zake wote na akanisingizia mambo mengi mabaya.
Sasa amerudi anaomba msamaha sana. Anataka tuoane na tusahau yote ya nyuma. Nikamwambia kwa jinsi ulivyonichafua, utawalaumu ndugu zako kuweka vipingamizi vya kila aina? Imetosha mimi nilipogombana na wewe, kesho siwezi kugombana na ndugu zako ambao tayari wameonyesha chuki kwa mambo yako ya uongo nami sipo comfortable kama mwanzo.
Kuna la kujifunza mwana jf. Unapogombana na mpenzi wako hata kama kweli ni mbaya, jifunze kumhifadhia madhaifu yake moyoni mwako. Ni utoto na ujinga sana kupeleka madhaifu ya mwenzako na kuongeza juu ili kumchafua. Wanasema mchimba kaburi anaingia mwenyewe. Sasa nimetulia na mambo yangu, mwenzangu anahangaika hajui wapi pa kushika.
Usiku mwema.
Mimi ni mwanamke mtu mzima (wengi uwa wanachanganyikiwa na hii jina wakidhani ni mwanaume.) Nilikua na mpenzi wangu toka october 2014 na mpaka sasa.
Kwenye mapenzi kuna raha na karaha. Mwanzo tulipendana sana kiasi cha mwenzangu kutambulika kwenye ukoo wa mwenzangu pasipo sisi wenyewe kutambulishana rasmi. Pengine ni kwa sababu wakwe watarajiwa ni majirani na pia tunakutana sana kwenye shughuli za kijamii.
Mwaka 2016, tuligombana na mwenzangu. Lakini kila mmoja akiwa bado ana mapenzi na mwenzie. Lakini kila nilipojaribu kusimamia kisolvu tatizo mwenzangu ndiye aliyeleta shida. Leo siwezi kuingia kwa undani juu ya ugomvi sababu si muhimu kwa mada hii ila ni ugomvi wa kawaida sana ambao mnaweza kuelewana na maisha yakaendelea.
Mwenzangu akaamua kusikiliza watu wa nje waliompa ushauri kuwa ni bora aachane na mimi. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuachwa na ninaempenda. Nililia. Niliomba msamaha pasipo kujua kosa. Nilihangaika sana.
Mwenzangu hakujali wala kunionea huruma. Ndio kwanza akaendelea kunituhumu hadi kwa sifa za uongo. Akaenda mbali zaidi na kusema hawezi kurudi labda amdate mama yake. Kitu cha mwisho kabisa, aliamua kunichafulia kwa ndugu zake wote na akanisingizia mambo mengi mabaya.
Sasa amerudi anaomba msamaha sana. Anataka tuoane na tusahau yote ya nyuma. Nikamwambia kwa jinsi ulivyonichafua, utawalaumu ndugu zako kuweka vipingamizi vya kila aina? Imetosha mimi nilipogombana na wewe, kesho siwezi kugombana na ndugu zako ambao tayari wameonyesha chuki kwa mambo yako ya uongo nami sipo comfortable kama mwanzo.
Kuna la kujifunza mwana jf. Unapogombana na mpenzi wako hata kama kweli ni mbaya, jifunze kumhifadhia madhaifu yake moyoni mwako. Ni utoto na ujinga sana kupeleka madhaifu ya mwenzako na kuongeza juu ili kumchafua. Wanasema mchimba kaburi anaingia mwenyewe. Sasa nimetulia na mambo yangu, mwenzangu anahangaika hajui wapi pa kushika.
Usiku mwema.