TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 4,917
- 15,067
Mkuu,Basi hapo unajiona mjanjaaa. Hakuna dhambi mbaya na yenye gharama, mikosi na nuksi maishani kama ya kula mke wa mtu. Sasa wewe furahia tu lakini utakuja kuona matokeo yake kwako mwenyewe, familia yako na watoto wako huko mbele ya safari.
Mfalme Daudi alijifanya mwamba lakini dhambi ile ilimtesa sana pamoja na familia yake - vifo, matoto kubakana, mengine yanauana na hata litoto limoja likaishia kuwa na wake 700 na michepuko 300. Alisamehewa dhambi yake ya kulala na kuzaa na mke wa mtu lakini madhara yake yaliendelea mpaka vizazi na vizazi.
Ndoa ni taasisi takatifu sana mbele ya Mungu. Usiiingilie!
Kama umeoa, mi nafikiri ni muhimu sana kutimiza majukumu yako kama mume kwa mke wako. Hivi vitisho vya ku quote mistari nk havitasaidia chochote. Hayo matatizo yote uliyoyataja yakitaka kukupata yatakupata tuu hayaangalii kwamba ulitembea na mke wa mtu ama la!