Annina
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 437
- 57
Katika vitu vinavyonisikitisha ni pamoja na hii tabia ya wanaume wanapokosana na kufikia kutengana na wake zao mara nyingi wamekuwa wakijikuta wametengana na watoto wao pia! Sina hakika ni kutokana na hasira au huwa ni jitihada za kumkomoa huyu mwanamke ambae awali alijulikana kwa majina mazuri kama honey, sweetie nk.
Nimeshuhudia matukio mengi ya akina mama kulea watoto waliotokana na ndoa zao zilizovunjika bila msaada wa waume zao, mara nyingi akina mama hawa huwa na kipato kidogo ukilinganisha na waliokuwa waume zao ambao wameenda kuanzisha familia mpya! Kweli sielewi logic ya kuacha mke na kukataa kuwatunza na kuwapenda watoto wako...sielewi ni nini?
Nimeshuhudia matukio mengi ya akina mama kulea watoto waliotokana na ndoa zao zilizovunjika bila msaada wa waume zao, mara nyingi akina mama hawa huwa na kipato kidogo ukilinganisha na waliokuwa waume zao ambao wameenda kuanzisha familia mpya! Kweli sielewi logic ya kuacha mke na kukataa kuwatunza na kuwapenda watoto wako...sielewi ni nini?