Zee Korofi
JF-Expert Member
- Oct 5, 2021
- 1,612
- 1,410
Hakuna cha salamu, siku takribani saba nimekuwa nikisikitika mno kwa mambo kadha wa kadha.
Leo moyo umepiga 'paaa' baada ya kuangalia 'list' ya majina ya wanafunzi kumi bora kitaifa waliofanya vizuri zaidi katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka 2022.
wa kwanza na wa pili ambao wote ni 'PCB' ni wadada. Wawili wa mwisho katika hao kumi bora ni wakaka.
Yaani wadada wanakuja juu midume chali. Hivi inakuwaje hii? Ndiyo kusema mwanamke si dhaifu kama ilivyozoeleka?
Wanaume wameniangusha sana, na inauma mno. Leo sili chakula, yaani sijui ndiyo tuseme wanaume wanazidi kupungua au? Yaani bora ingekuwa mara moja moja, ila kila mwaka wanawake wanaongoza, na wanazidi kuja juu.
Hali hii haitoishia kwenye elimu tu msipoangalia, mpaka kwenye sekta zingine itafika. Tujadili hili tuone shida ni nini? Wapi tunakwama/madogo wamekwama? Nini kifanyike?
Kuanzia leo kwa muda usiojulikana, sili nyama na sitonyoa nywele wala kupaka mafuta, kucha sitokata. Hii ni adhabu niliyojipa kwa niaba ya magoi goi wote wa kiume.
Leo moyo umepiga 'paaa' baada ya kuangalia 'list' ya majina ya wanafunzi kumi bora kitaifa waliofanya vizuri zaidi katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka 2022.
wa kwanza na wa pili ambao wote ni 'PCB' ni wadada. Wawili wa mwisho katika hao kumi bora ni wakaka.
Yaani wadada wanakuja juu midume chali. Hivi inakuwaje hii? Ndiyo kusema mwanamke si dhaifu kama ilivyozoeleka?
Wanaume wameniangusha sana, na inauma mno. Leo sili chakula, yaani sijui ndiyo tuseme wanaume wanazidi kupungua au? Yaani bora ingekuwa mara moja moja, ila kila mwaka wanawake wanaongoza, na wanazidi kuja juu.
Hali hii haitoishia kwenye elimu tu msipoangalia, mpaka kwenye sekta zingine itafika. Tujadili hili tuone shida ni nini? Wapi tunakwama/madogo wamekwama? Nini kifanyike?
Kuanzia leo kwa muda usiojulikana, sili nyama na sitonyoa nywele wala kupaka mafuta, kucha sitokata. Hii ni adhabu niliyojipa kwa niaba ya magoi goi wote wa kiume.