Wanaume: Je mnakipa tafsiri gani kitendo cha mwanamke kukubali kujamiiana mapema...?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,806
15,379
black-couple-in-bed.jpg


Inawezekana ikawa ni kwenye mtoko wa kwanza, kutokana na mazingira kuruhusu na kuwa muafaka kwenu mkajikuta tu jambo hilo limefanyia bila nyie kujijua, au inawezekana baada ya mitoko miwili mkajikuta mmefikia hatua ya kujamiiana.

Hebu fungukeni, mnamchukulia vipi mwanamke anayekubali kujamiiana muda mfupi tu baada ya kujuana?

cheating-husband-450a121208-1258748685-378x394.jpg


1. Je ni malaya?

2. Je, anakupenda sana?

3. Je kuna kitu kimemvutia kwako na anataka kukunasa haraka?

4. Anajiamini na amekuamini na hana cha kupoteza hata ukimuacha,

5. Ana matarajio makubwa juu yako na anaamini uhusiano wenu utafika mbali kwa kuwa kuna mambo mengi mnaendana.
 
Mhmmm!!! Kwa upande wangu mimi huwa na judge hili swala kutokana na mwanamke mwenyewe jinsi alivyo kama vile tabia na mwenendo wake mzima wa maisha na si kwa sababu ya kujamiiana muda mfupi baada ya kujuana. Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kupelekea wapendao kujamiiana muda mfupi tu baada ya kujuana. Ila wanaume wengi mwanamke akikubali kujamiiana muda mfupi tu baada ya kujuana wengi wetu huwa tunamuona malaya na rahisi kudanganyika mawazo ambayo yanaweza yakawa sahihi au sio sahihi maana hata wenzetu wazungu husema "Dont judge a book by its cover"
 
Mimi anaye nisumbua simtaki ana nipotezea muda wa kufanya kazi zangu.
kama ana kupenda ita baki ana kupenda kumzungusha siyo ndiyo ina ongeza thamani ya m2
 
Mimi naona sawa tu kama wewe mwanaume umemtaka mapema na yeye akapubali mapema, basi poa tu !!

Atakavyo kuwa vyovyote vile basi mtakuwa sawa2 wote wawili !!!
 
Mie huwa namuona kama ni "cheap commodity" ambayo kila mtu anaweza kubeba........
Na akikubali fasta hata umkinai na kumuacha kwangu huwa ni fasta vile vile............
 
Mhmmm!!! Kwa upande wangu mimi huwa na judge hili swala kutokana na mwanamke mwenyewe jinsi alivyo kama vile tabia na mwenendo wake mzima wa maisha na si kwa sababu ya kujamiiana muda mfupi baada ya kujuana. Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kupelekea wapendao kujamiiana muda mfupi tu baada ya kujuana. Ila wanaume wengi mwanamke akikubali kujamiina muda mfupi tu baada ya kujuana wengi wetu huwa tunamuona malaya na rahisi kudanganyika mawazo ambayo yanaweza yakawa sahihi au sio sahihi maana hata wenzetu wazungu husema "Dont judge a book by its cover"

Hapo kwenye BOLD nakubaliana na wewe kuwa wanaume wengi huwa na mawazo hayo potofu.

Lakini malalamiko mengi ya wasichana niliowahi kuzungumza nao, wanadai kwamba wanaume wa siku hizi akiomba ki-date, siku hiyo hiyo anataka game na mdada akichomoa, ataendelea kulazimisha jambo hilo lifanyike kwa nguvu zote yaani hatoi hata nafasi ya kujuana zaidi ya kutaka game tu basi, na akiendelea kuwa mgumu, jamaa anakata kamba na harudi tena......

Najua wapo wanaojisitiri na kukataa moja kwa moja kama lengo la mwanaume huyo linaonekana kulazimisha kujamiiana, lakini kuna ambao wanaona labda kuendelea kukataa ni kupoteza bahati, na hawa ndio wahanga maana wanakuwa kama vile wanacheza bahati nasibu...........

Hebu tuliweke wazi jambo hili, ili dada zetu ambao wako mawindoni wapate kupumuwa............
 
Hapo kwenye BOLD nakubaliana na wewe kuwa wanaume wengi huwa na mawazo hayo potofu.

Lakini malalamiko mengi ya wasichana niliowahi kuzungumza nao, wanadai kwamba wanaume wa siku hizi akiomba ki-date, siku hiyo hiyo anataka game na mdada akichomoa, ataendelea kulazimisha jambo hilo lifanyike kwa nguvu zote yaani hatoi hata nafasi ya kujuana zaidi ya kutaka game tu basi, na akiendelea kuwa mgumu, jamaa anakata kamba na harudi tena......

Najua wapo wanaojisitiri na kukataa moja kwa moja kama lengo la mwanaume huyo linaonekana kulazimisha kujamiiana, lakini kuna ambao wanaona labda kuendelea kukataa ni kupoteza bahati, na hawa ndio wahanga maana wanakuwa kama vile wanacheza bahati nasibu...........

Hebu tuliweke wazi jambo hili, ili dada zetu ambao wako mawindoni wapate kupumuwa............

Mkuu Mtambuzi nakubaliana na maelezo yako kwa 100%. Unajua dada zetu na sio dada zetu tu bali na vijana wote pia kwa ujumla wanapaswa kuwa makini wanapoanzisha uhusiano wa kimapenzi. Watambue kuwa kila mtu huwa ana sababu au madhumuni ya kuanzisha uhusiano huo. Hivyo hata siku moja wasije wakadhani na kuamini kuwa wazo au dhumuni ulilonalo la kuanzisha uhusiano huo ndilo hilo hilo ambalo analo mwenzako. Ukifanya hivyo utakuwa umekosea sana na hapa ndio vijana wengi tunapoangukia pua.

Kutambua sababu au dhumuni la mpenzi wako kuanzisha uhusiano na wewe ni hatua muhimu sana ambayo vijana wengi huwa tunaipuuza na matokeo yake tunaishia kulaumu kwamba wanaume ni wabaya au wanawake ni wabaya wakati kosa umelifanya mwenyewe.
 
Moja mpaka tano sijaona sababu ambayo nakubaliana nayo,ninacho weza kusema kwa wanaume wengi tulivyo mwanamke akikubali tendo la ndoa haraka anasababisha maswali mengi...Labda iwe ni mtu ambaye mnafahamiana kwa muda mrefu na kila mmoja anamfahamu mwenziwe vizuri haijatokea tu kutakana kimapenzi,lakini sio mmekutana kwenye daladala siku ya pili 'kitu pwani' atakuwa na walakini huyo.
 
As u said none among th 5 is the reason,labda turevert swali liwe kwann majority ya wanaume wana-ask 4sex mapema??why? Je ni malaya?? Kwao thaman ama uzuri wa mwanamke ni kitumbua 2? Lengo la date kwao ni nn?? Wakihitaji hyo ngono mapema wanategemea jibu gani kutoka upande wa pili??
Moja mpaka tano sijaona sababu ambayo nakubaliana nayo,ninacho weza kusema kwa wanaume wengi tulivyo mwanamke akikubali tendo la ndoa haraka anasababisha maswali mengi...Labda iwe ni mtu ambaye mnafahamiana kwa muda mrefu na kila mmoja anamfahamu mwenziwe vizuri haijatokea tu kutakana kimapenzi,lakini sio mmekutana kwenye daladala siku ya pili 'kitu pwani' atakuwa na walakini huyo.
 
kwa mtizamo wangu ni kuwa kuna wanawake wengi ambao ambao wanatoa nanihii cku ya kwanza wako honest zaidi kuliko wanaopiga danadana ili waonekane credible, kwa sababu jamii na tamaduni nyingi zinaelekeza kuwa eti kujiachia kirahisi ni umalaya.
 
As u said none among th 5 is
the reason,labda turevert swali liwe kwann majority ya wanaume wana-ask
4sex mapema??why? Je ni malaya?? Kwao thaman ama uzuri wa mwanamke ni
kitumbua 2? Lengo la date kwao ni nn?? Wakihitaji hyo ngono mapema
wanategemea jibu gani kutoka upande wa pili??
...

lo! .. mwaswali maswali mazuri haya ... yajibiwe tafadhali
 
Wanaume tunatofautiana kwenye hili kamwe hatuwezi kuwa na msimamo mmoja. Wengine walinanihii mapema kabisa na hawakuona tatizo na mapenzi yakapamba moto hadi wakafunga ndoa. Sasa kama njemba inataka KUNANINO mapema na binti naye akawa kampenda jamaa kupita kiasi akiamua kumpa tatizo liko wapi? Si njemba ndiye aliyeomba apewe mapema mapema? Kama akipewa mapema kwanini lawama ziwe kwa Bi dada pekee yake na si kwa njemba aliyetaka kunanino mapema mapema?

 
Last edited by a moderator:
black-couple-in-bed.jpg


Inawezekana ikawa ni kwenye mtoko wa kwanza, kutokana na mazingira kuruhusu na kuwa muafaka kwenu mkajikuta tu jambo hilo limefanyia bila nyie kujijua, au inawezekana baada ya mitoko miwili mkajikuta mmefikia hatua ya kujamiiana.

Hebu fungukeni, mnamchukulia vipi mwanamke anayekubali kujamiiana muda mfupi tu baada ya kujuana?

cheating-husband-450a121208-1258748685-378x394.jpg


1. Je ni malaya?

2. Je, anakupenda sana?

3. Je kuna kitu kimemvutia kwako na anataka kukunasa haraka?

4. Anajiamini na amekuamini na hana cha kupoteza hata ukimuacha,

5. Ana matarajio makubwa juu yako na anaamini uhusiano wenu utafika mbali kwa kuwa kuna mambo mengi mnaendana.
Mi huwa najisikiwa kuwa najuwa kutongoza, na ndiyo maana nimekubakiwa fasta. Vile mkumbuke kuwa mwanamke anapongonoka na wewe iwe fasta au baada ya muda mrefu, anakuwa ameshafanya hivyo akilini mwa muda mreefuu uliopiata, ila tu mida wa kifanya kwa matendo ndo unakuwa umefika
 
Nadhani wanawake wa siku hizi tuko tofauti sana na wa zamani. Hatufanyi sex blindly tena. Na sie tunakuwa na mahesabu kichwani, wakati mwingine mahesabu ya mapenzi na wakati mwingine ya kumtumia mwanaume (kingono, kihisia, kiuchumi au hata kitaaluma). But as said, wakati mwingine mwanamke alikulengesha na wewe ukadhani ndo ulianza kumuon na kumshawishi, kumbe alishamalizana na wewe siku mingi kabla haujamuona.
 
...Unahitaji kushika mkono tu wala huna haja ya kubwabwaja kuanza kupanga mistari ya mtongozo lol!



Nadhani wanawake wa siku hizi tuko tofauti sana na wa zamani. Hatufanyi sex blindly tena. Na sie tunakuwa na mahesabu kichwani, wakati mwingine mahesabu ya mapenzi na wakati mwingine ya kumtumia mwanaume (kingono, kihisia, kiuchumi au hata kitaaluma). But as said, wakati mwingine mwanamke alikulengesha na wewe ukadhani ndo ulianza kumuon na kumshawishi, kumbe alishamalizana na wewe siku mingi kabla haujamuona.
 
Last edited by a moderator:
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom