Tuwe waungwana, mtu akikuomba msaada wa chakula usimpe makombo

IROKOS

JF-Expert Member
Aug 13, 2011
10,184
7,819
Nimeingia bar moja maarufu hapa Dodoma nikitokea Kigoma ili nipate mlo na bia mbili tatu.

Sasa meza jirani nami mwanaume mmoja kaagiza ugali na makange naona ya mbuzi au ng'ombe, mdada mmoja mrembo sana anajituma kweli kumhudumia, huku akichombeza hapa na pale kwamba na yeye toka asubuhi hajala. Jamaa anamwambia usijali utakula mpaka uvimbiwe.

Mwisho wa mchezo jamaa ule ugali ameutia mavidole yake woootee na nyama kala zooteee halafu kamuita mdada wa watu akamsukumia ile left overs huku jamaa anaondoka. Sasa kilichonitia huruma ni yule dada kuamua kuanza kule ile left over huku akilalamika!! Kwa kuwa nilikuwa meza jirani nikamuuliza mbona wala huku walalamika?

Akajibu nifanyeje sasa? Wataka nilale na njaa kama jana? Aisee ilibaki chenji yangu buku 4 nikamwambia akachukue.

Muda nataka kuondoka akanipa kikaratasi kumbe kina namba yake, nilipofika gest nikampigia akaniambia ukitaka nije ulikofikia nipigie maana umeniokoa leo, nikamwambia nimeguswa tu na shida zako.

Back to wanaume kwa nini tufanye hivi kwa hawa ndugu zetu? Kwani ungemeambia nina pesa ya mlo wangu tuu si angeelewa?

Kwanini umdhalilishe binadamu mwenzako kwa kuwa tuu umemkuta bar?
 
Duh tuseme kweli tu hizi story za wanasiasa kwenye majukwaa eti nchi ipo kwenye uchumi wa kati ni porojo tu watu wana hali mbaya mno. ifike mahali tuache ushabiki usio tusaidia tufanye uchaguzi wa viongozi walio sahihi, kama ni maendeleo yafanywe yanayo saidia walio wengi sio wachache wafaidi huku walio wengi mlo mmoja kwa siku shida.
 
Hamna kitu kama hiyo hapa Dodoma,
warembo na jirani na Bar hiyo wana hela za kutupwa, hawajawa ombaomba mpaka usiku
ungesindikiza na kapiha au ungesema Bar hiyo ipo sehemu gani labda Tango Uhindini ndio kuna makange lkn warembo wanajitosheleza
 
Nimeingia bar moja maarufu hapa Dodoma nikitokea Kigoma ili nipate mlo na bia mbili tatu....

Kwanini umdhalilishe binadamu mwenzako kwa kuwa tuu umemkuta bar?
Tumeubwa tofauti sana ndugu. Mie hicho chakula huenda kisingepanda kabisa. Kula huku kuna mhitaji mwenzangu pembeni anaangalia!
Hebu nikupe story moja.

Kuna kijiji fulani huwa naenda mkoani Iringa kibiashara, na ni kawaida yangu kula mghahawa mmoja. Siku moja nikamuona mama fulani anavizia left overs pale. Nikakata samaki wangu nusu nikapunguza na msosi kidogo nikamuwekea kwenye sahani aliyokuwa ameishika(iko na left overs kidogo).

Cha ajabu kijana muuzaji wa pale akaja kumnyang'anya yule mama sahani, eti anaenda kuosha! Tulimzomea baadae akamrudishia.
 
Back
Top Bottom