WANAUME haya ni mambo muhimu ukiwa unatafuta mke,sifa na mambo muhimu 25 kama MDADA hana achana nae

Mshinga

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
3,532
1,124
1.A-age(younger than you but not too young atmost 6years)
2.B-beauty(lazima awe mzuri)
3.C-character(lazima awe na tabia nzuri)
4.D-distance(umbali unakomtolea mpenzi wako ni jambo muhimu sana pia,kama mume akitoka bukoba na mke lindi na wakaishi bukoba, ikitokea dharula kwa mke kurudi nyumbani ama ama wote kwenda huko ni tatizo katika mambo ya kiuchumi na unalazimika kuingia gharama kubwa)
5.E-educaton(kigezo cha elimu ni muhimu sana,angalau usimzidi sana ili hata ukifa yeye ataihumia familia,akikuzidi ni utata pia)
6.F-family backround(lazima na ni muhimu sana kujua historia ya familia yake,wazazi wake,kaka zake na dada zake ili upate picha kuwa ni watu wa aina gani)
7.G-generosity(lazima awe na moyo wa kutoa na asiwe mbinafisi)
8.H-healthy(lazima mwanamke mwenye afya njema kabla hujamuoa)
9.I-intelligent(mke wako anatakiwa kuwa na akili nyingi na asipokuwa nazo ni tatizo zaidi kuliko unafuu kwenye familia)
10.J-joy(lazima awe ni mtu mwenye kuonyesha furaha)
11.K-knowledge(lazima awe ni mke mwenye uelewa wa kutosha,ukioa asiye na uelewa ni tatizo pia)
12.L-love(lazima aonyeshe kukupenda kwa dhati, kama hajakupenda na ukamlazimisha ama akalazimishwa ujue ataleta shida baadae)
13.M-morals(lazima mwanamke awe binti aliyelelewa kwa maadili mazuri na awe na hayo maadili mazuri)
14.N-neatness(lazima mwanamke awe ni msafi,si munajua tena mwanamke ni ua, mambo ya kukaa rough rough yatakufanya umuone mbaya muda si mwingi kwa urough wake na nyumbani patakuwa hovyohovyo)
15.O-opinions(awe ni mwanamke mwenye uwezo wa kuwa na maoni kwa msitakabali wa maendeleo ya familia)
16.P-parental(lazima awe ni mwanamke aliyetayari kubeba majukumu ya uzazi, usije kuoa mwanamke hasa wale wasiotaka kuzaa,yaani hao kudumu nao ni utata na mtaachana tu maana hakuna kitachomuuma akikuacha)
17.Q-questioning(lazima mwanamke wa kuoa awe na uwezo wa kuhoji, isije ukawa unafanya mambo ya kipumbavu alafu anaangalia wakati munaangamia,lazima akurekebishe)
18.R-respect(awe mwanamke mwenye mwenye heshima kwa watu wote)
19.S-satisfying(lazima awe anauwezo wa kukuridhisha hasa kwenye mambo ya kitandani)
20.T-tolerance(lazima mwanamke awe ni mvumilivu katika vipindi vya mpito maana maisha na milima na mabonde ili asije shawishika ama kukuacha wakati wa shida)
21.U-union(lazima awe ni mtu wa kujumuika na kuunganika na jamii ili kujenga mahusiano mazuri na jamii inayokuzunguka)
22.V-volunteer(lazima awe ni mwanamke mwenye kujitolea,asiwe mtu wa kusukumwa kila mara kufanya jambo)
23.W-wise(akili lazima ziwe ziko timamu)
24.X-xmass(lazima awe amezaliwa upya na kumpokea yesu,kama ni mwisilamu yaani awe mcha mungu, )
25.Y-yourself(lazima awe ni mwanamke anayejikubali kwa jinsi alivyo, si mara anata weupe wakati yeye ni mweusi, mara anataka ------ makubwa wakati hana,nk ili aendelee kuwa natural muda wote na kulinda uzuri na afya yake)
26.Z-zeal
HAYA KUNA SIKU NILIMEGEWA NA BABU WA MIAKA 78 NA MKE WAKE ANA MIAKA 73, NILIKUTANA NAO WOTE NA WALIONEKANA WENYE FURAHA ZAIDI NA TULIONGEA NAO MAMBO MENGI SANA JAPO SISI VIJANA TULIKUWA WASIKILIZAJI ZAIDI.
ni kama wiki tatu zilizopita.
kazi kwenu.
sifa na vigezo hivi hata wanawake wanatakiwa kuvitumia kutafuta mume
 
sidhan kama kuna mwanaume dunian alishawahi kuoa mwanamke mwenye sifa zote ulizozitaja, labda awe malaika, hakuna binadamu aliyekamilika kila idara (kwa ufahamu wangu huu mdogo). mambo mengine ni kuelekezana tu
 
vigezo vingi sana hivyo na ikitokea umempata hata mwenye zaid ya kimoja shukuru MUNGU.
 
Yani kupata alietimiza vigezo vyote hivo siyo rahisi,hakuna mkamilifu hata m1 katika huu ulimwengu. Hapo utaishia kupata kwa uchache
 
Yani kupata alietimiza vigezo vyote hivo siyo rahisi,hakuna mkamilifu hata m1 katika huu ulimwengu. Hapo utaishia kupata kwa uchache

nani amewaambia mtu mkamilifu ndio ana vigezo hivyo?MBONA KUNA MAMBO MENGINE HAYAPO HAPO AMBAYO HAYAONDOI MAPUNGUFU YA KIBINADAMU
 
Mke/mme mwema mtu hupewa na Bwana. Utakayempata kubali ndiye huyo then rekebishaneni migongano inapojitokeza.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Dah! hii kali, vigezo vimezidi aiseeee! Na ukimtaka mtu kwa vigezo unavyojiwekea wewe kichwani unaweza usimpate milele. Ndoa ni suala la makubaliano tu.
 
Mke/mme mwema mtu hupewa na Bwana. Utakayempata kubali ndiye huyo then rekebishaneni migongano inapojitokeza.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
mke mwema hatoki kwa bwana< tumepewa akili na bwana tuzitumie na ndio tunachambua mambo hapa< tungekuwa tunasubiri tu aletwe tena tungekuwa tunaletewa hata kutoka mabara mengine kama china<india<ujeru< nk lakini nashangaa eti mnaletewa walewale tu waswahili
 
sidhan kama kuna mwanaume dunian alishawahi kuoa mwanamke mwenye sifa zote ulizozitaja, labda awe malaika, hakuna binadamu aliyekamilika kila idara (kwa ufahamu wangu huu mdogo). mambo mengine ni kuelekezana tu
mbona hao wapo jamani <mimi mwenyewe ni miongoni kwa upande wa wanaume<sema nimewahiwa tu<hivi vigezo sio vigezo vya mtu aliyekamilika kila idara< mimi hapo mbona ninafiti na wapo wadada wengi wanafiti hapa
 
Kwa nini unafikiri vigezo vyako vinafaa? Vinamfaa nani?

Wewe utasema mwanamke awe mdogo, mtu mwingine atasema anataka kuoa kama bwana mtume kutafuta kumfuata vizuri, aoe mama wa makamo.

Kwa huyo udogo so kivutio.

Huwezi kuwa na kigezo kimoja kwa watu wote.

Waingereza wanasema "one man's meat, is another man's poison".
 
Kwa nini unafikiri vigezo vyako vinafaa? Vinamfaa nani?

Wewe utasema mwanamke awe mdogo, mtu mwingine atasema anataka kuoa kama bwana mtume kutafuta kumfuata vizuri, aoe mama wa makamo.

Kwa huyo udogo so kivutio.

Huwezi kuwa na kigezo kimoja kwa watu wote.

Waingereza wanasema "one man's meat, is another man's poison".
na wewe kwa nini unafikiri havifai?
huoni nimeeleza kundi la watu ambao vigezo hivi vinawafaa?
hapo hujaaona ama hata kuhesabu umeshindwa?hapo kuna vigezo 26.
this man's meat was not intended to those who see this as their poison.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom