Wanasimba tutakaoishangilia ZESCO kutoka Zambia siku ya Jumamosi tukutane hapa

Siku ya Jumamosi timu ya Zesco kutoka Zambia itacheza na Yanga Sports Club kwenye dimba la Mkapa.
Timu ya Zesco ndipo anapochezea kaka wa triple C kiungo mahiri wa clab ya Simba Adrian Chota Chama (ACC)

Adrian ni beki wa kutumainiwa wa kikosi cha ZESCO ambacho wakati wowote kitawasili nchini kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Yanga ambao utapigwa Jumamosi

Familia na Mzee Chota imebarikiwa kuwa na vijana hao ambao wana vipaji vya hali ya juu katika kusakata kabumbu

Ntakuwa taifa jukwaa pendwa la wanamsimbazi ndani ya uzi wa Zesco.
Tupo Mkuu,
Tupo kabisa TeamZesco.
Lazima Vyura wakae jumamos
 
Nyie wa kuja ndio mnafanya huo umama..born here here hatuwezi kwenda mechi ya Simba Taifa
Born here here from Indian ocean ocean to Mwanalumango, soon mtajikuta Moro au Lindi teh teh teh.....
Narudia tena mashabiki wa Yanga tikiti zimeshatua taifa wahi tecket msijekuta uwanja umejanzwa na matajiri Simba sports club
 
Born here here from Indian ocean ocean to Mwanalumango, soon mtajikuta Moro au Lindi teh teh teh.....
Narudia tena mashabiki wa Yanga tikiti zimeshatua taifa wahi tecket msijekuta uwanja umejanzwa na matajiri Simba sports club
Matajiri mnaokula hadi rambirambi za wachezaji?
 
Akili zako haziko sawa: Hivi aliyekuokoa usishuke daraja leo unamwambia pambana na hali yako? Je, Yanga nao wangesema pambana na hali yako ungekuwepo? Si ungekuwa kama Nyota nyekundu Fc, unaijua?
Ahahahaha umebebwa kucheza Klabu bingwa wakati wewe si bingwa.
Saizi jitegemee msaada tunauhamishia Zesco. We pambana na hali yako.
 
Akili zako haziko sawa: Hivi aliyekuokoa usishuke daraja leo unamwambia pambana na hali yako? Je, Yanga nao wangesema pambana na hali yako ungekuwepo? Si ungekuwa kama Nyota nyekundu Fc, unaijua?
Kuna mwamba pale Zesco anaitwa Kapumbu ,ili povu litakuwa kubwa zaidi jumamosi
 
Baada ya game ya Jumamosi nafikiri vyura mtashika adabu siku timu ya Taifa Simba sports club itakapokuwa inacheza.
 
Akili zako haziko sawa: Hivi aliyekuokoa usishuke daraja leo unamwambia pambana na hali yako? Je, Yanga nao wangesema pambana na hali yako ungekuwepo? Si ungekuwa kama Nyota nyekundu Fc, unaijua?
We ndo hamnazo, mana unachoongea ukienda Kwenye documentary za TFF hakipo. Ni umbea na kule kutaka kujiona.
Je, wewe unapocheza Klabu bingwa we ni bingwa wa nchi gani?
 
Tupo Mkuu,
Tupo kabisa TeamZesco.
Lazima Vyura wakae jumamos
Ushauri wa bure kwa timu za Simba na Yanga: Namna fanisi zaidi ya kuivunja moyo timu ya watani zenu ni kukaa kimya au kuishangilia. Kwa sababu kitu kimojawapo kinachoisukuma timu ya mtani kufanya vizuri inapoingia uwanja ni kuchelea kuchekwa na mahasimu zao. Kwa sababu kwa utamaduni wa timu mbili hizi, wapenzi wao hubaki kimya uwanjani timu zao zikitangulia kufungwa, hasa kwa idadi ya mabao zaidi ya moja. Hamasa pekee wanayoipata watani walio dimbani kuanzia hapo ni zomeazomea ya wapinzani, ambayo ni msaada kwao kwa sababu watataka kuwanyamazisha mahasimu hao lakini pia watapata kujua mchezo wao unaendeleaje kwa kupima kiwango cha ongezeko au punguo la zomea yenyewe. Hata maji machafu, au majitaka kwa wengine, yanatosha kuzimia moto.
 
Siku ya Jumamosi timu ya Zesco kutoka Zambia itacheza na Yanga Sports Club kwenye dimba la Mkapa.
Timu ya Zesco ndipo anapochezea kaka wa triple C kiungo mahiri wa clab ya Simba Adrian Chota Chama (ACC)

Adrian ni beki wa kutumainiwa wa kikosi cha ZESCO ambacho wakati wowote kitawasili nchini kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Yanga ambao utapigwa Jumamosi

Familia na Mzee Chota imebarikiwa kuwa na vijana hao ambao wana vipaji vya hali ya juu katika kusakata kabumbu

Ntakuwa taifa jukwaa pendwa la wanamsimbazi ndani ya uzi wa Zesco.

Sawa...shangilieni tu...siyo kitu cha ajabu kwa Simba kwani historia inaonesha kuwa ndiyo klabu ya kwanza chini kwa kushangilia timu ngeni...ilianza miaka ya 1969 na 1970 wakati Young Africans ilipokuwa ikiiwakilisha nchi kwa kucheza na Asante Kotoko ya Ghana na baadaye Enugu Rangers ya Nigeria...
 
Back
Top Bottom