Wanasiasa wetu mnatuangusha, eti mnafuata uchawi Tanzania

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,514
47,736
Huu ni ujinga ambao umenikera hadi basi, taarifa kwamba baadhi ya wanasiasa wetu wanakwenda Tanzania kutafuta nguvu za kishirikina ili kuwawezesha kushinda uchaguzi. Laana ya ovyo hii na maeneo mengine ya nchi yetu yataendelea kuwa nyuma miaka yote.
Bora ningeskia mnavuka mpaka kwenda kujadili uashirikiano wa kibiashara na mengineyo maana, mtailemaza nchi hadi lini, maeneo kama Migori ambayo yanaongoza kwa huu upuzi bado yapo nyuma kiuchumi.

-----------------------------------------------------------------------------------------------------------

mganga.jpg


Vifaa vya uchawi. Picha/MAKTABA
Na ELISHA OTIENO

Imepakiwa - Monday, May 22 2017 at 17:40
Kwa Mukhtasari

HUKU siku ya Uchaguzi Mkuu ikizidi kukaribia, idadi ya wawaniaji kutoka kaunti za Migori na Homa Bay wanaosafiri hadi Tanzania kusaka huduma za waganga imeongezeka lengo likiwa moja; kutwaa ushindi baada ya Agosti 8.

Wanasiasa hao wanaowania viti mabalimbali wamekuwa wakisafiri hadi miji ya Tarime, Musoma na Mwanza kutafuta usaidizi wa 'nguvu za kiza’ kuwawezesha kupata ushindi bila jasho.



Inadaiwa waganga hao wamekuwa wakiwapa wanasiasa hirizi ili kuwapokonya wapinzani wao wapiga kura. Wengi wa wawaniaji hao walianza kumiminika nchini Tanzania mwezi Februari kabla ya michujo kufanywa.



Ripoti ya 'Taifa Leo’ inaonyesha kuwa wanasiasa hao wanaamini kuwa waganga wana uwezo wa kuwahakikishia ushindi katika kinyang’anyiro cha Agosti.



“Wengi wa wawaniaji wanaamini kuwa hawawezi kupata ushindi bila usaidizi wa nguvu za kishetani. Tumekuwa tukiwaona wengi wao wakipitia hapa na kuingia Tanzania,” akasema Bw George Ogwang’, wakala wa ukaguzi wa mizigo katika eneo la mpakani la Isebania.



“Ninamjua mmoja wa wanasiasa ambaye alipokea huduma za waganga hao na bado akabwagwa kwenye mchujo,” akaongeza.



Bw Mohammed Yaya ambaye ni mganga wa mjini Tarime aliambia 'Taifa Leo’ kwamba ni kawaida kwa biashara kunoga kila mara Kenya inakaribia Uchaguzi Mkuu.



“Wao huja kupata huduma zetu na wanalipa pesa zozote ambazo tunawaitisha,” akasema.



Wasaidizi wa karibu wa wanasiasa mbalimbali walikiri kuwa waajiri wao huamini usaidizi wa waganga.



Itakuchukua saa nne kusafiri kutoka Migori hadi Mwanza lakini ni dakika 50 tu kwa gari la kibinafsi kusafiri hadi Tarime.



Bw Yaya alisema kuwa wanamtoza mwnasiasa pesa kulingana na kiti ambacho anawania lakini kiasi cha pesa hizo huweza kujadiliwa na kuafikiana.



Utumizi wa waganga ulianza wakati wa demokrasia iliyoruhusu vyama vingi nchini na visa hivi vimekuwa vikiripotiwa katika kanda zote za nchi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu.



Mnamo Novemba 1994, waziri wa zamani Musikari Kombo alipoteza kiti chake cha Ubunge wa Webuye baada ya mahakama kumpata na hatia ya kutekeleza kosa la uchaguzi kwa kusaka huduma za waganga.



Kiongozi huyo wa zamani wa chama cha Ford-Kenya alishtakiwa kwa kuwalipa waganga wawili ili kuwapa wapiga kura kiapo kinachojulikana kwa lugha ya Kibukusu kama 'khulia silulu’ (kinamaanisha kula kitu chenye uchungu).



Kicheko kilizuka mahakamani wakati maelezo ya jinsi kiapo hicho kilipeanwa yalitolewa mbele ya majaji watatu waliosikiza kesi hiyo.



Maaskofu na makasisi wakiongozwa na kasisi wa kanisa la Deliverance Mark Kariuki wamewaonya wanasiasa dhidi ya utumizi wa uchawi, uganga na nguvu za kishetani katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti.



Walisema baadhi ya wanasiasa husafiri mataifa ya Kusini na Magharibi ya Afrika kutafuta hirizi.


Wanasiasa Wakenya wamiminika Tanzania kusaka ushindi Agosti
 
Hamna tatizo kwa mtu kwenda kwa mtaalamu. Mbona hamsemi watu wanaoenda kuombewa makanisani na misikitini? Waafrika mmekuwa brainwashed na wazungu na waarabu, mtu akivaa rozari ama tasbihi haina shida kwenu lakini mtu akivaa hirizi mnamuona wa ajabu.

Kila mtu ana imani yake, sio lazima kila mtu afuate imani zenu za kigeni.
 
Hamna tatizo kwa mtu kwenda kwa mtaalamu. Mbona hamsemi watu wanaoenda kuombewa makanisani na misikitini? Waafrika mmekuwa brainwashed na wazungu na waarabu, mtu akivaa rozari ama tasbihi haina shida kwenu lakini mtu akivaa hirizi mnamuona wa ajabu.

Kila mtu ana imani yake, sio lazima kila mtu afuate imani zenu za kigeni.
Hahaha...I see your point.
 
Hamna tatizo kwa mtu kwenda kwa mtaalamu. Mbona hamsemi watu wanaoenda kuombewa makanisani na misikitini? Waafrika mmekuwa brainwashed na wazungu na waarabu, mtu akivaa rozari ama tasbihi haina shida kwenu lakini mtu akivaa hirizi mnamuona wa ajabu.

Kila mtu ana imani yake, sio lazima kila mtu afuate imani zenu za kigeni.

Makes alot of sense mkuu, tunafwata imani na miungu wa kigeni ilhali tamaduni zetu na mila tunaziona za kishamba na kishirikina, asante kwa jibu lako.
 
Unashindwa Kuwashangaa wale wanao kwenda kuua Watoto wasio jua lolote kisa tu baba mwanasiasa!!

Wewe hili la kuuawa kwa watoto umelichangamkia utadhani ni zile mada za alshabaab huwa zinakupa raha, unalitaja taja kwa raha sana. Kufikia sasa imebainika mjomba wa hao watoto ndiye alikua na kisasi binafsi cha kifamilia na alituma hadi SMS, tulia uchunguzi ukamilike.
Hawa hawakuuawa kama wale watoto walemavu wa albino ambao huwa mnawaua huko kwenu eti muwe matajiri na mshinde uchaguzi, ni mambo ya kinyumbani ambapo mshukiwa tayari yupo korokoroni.
 
Hamna tatizo kwa mtu kwenda kwa mtaalamu. Mbona hamsemi watu wanaoenda kuombewa makanisani na misikitini? Waafrika mmekuwa brainwashed na wazungu na waarabu, mtu akivaa rozari ama tasbihi haina shida kwenu lakini mtu akivaa hirizi mnamuona wa ajabu.

Kila mtu ana imani yake, sio lazima kila mtu afuate imani zenu za kigeni.

Hehehehe!! Haya bwana, ila nyie noma kwenye hiyo taaluma sasa mbona msiitumie katika kuifanya nchi iwe kwenye dunia ya kwanza.
 
Ushirikina ndio nini? Kama mtu anatumia njia za Kiroho za Kiafrika kukabili maisha yake ya kila siku we inakuuma nini? Waganga wa huku kwetu wanasajiliwa na Wizara inayohusika na Ustawi wa Jamii na wanalipa mafungu serikalini, its kind of official business sir...
 
ndio watz wanaojua sana...wataalam kwel kwel kwa mambo ya uganga...nakumbuka habari za yule mzee wa Loliondo zilizojaa Kenya...this is the number one export from tz to kenya...uchawi...nakubaliana nawe MK254...hili ni jambo la kipuuzi sana...heri kafiri kuliko mshirikina...
 
Wewe hili la kuuawa kwa watoto umelichangamkia utadhani ni zile mada za alshabaab huwa zinakupa raha, unalitaja taja kwa raha sana. Kufikia sasa imebainika mjomba wa hao watoto ndiye alikua na kisasi binafsi cha kifamilia na alituma hadi SMS, tulia uchunguzi ukamilike.
Hawa hawakuuawa kama wale watoto walemavu wa albino ambao huwa mnawaua huko kwenu eti muwe matajiri na mshinde uchaguzi, ni mambo ya kinyumbani ambapo mshukiwa tayari yupo korokoroni.

Kwa taarifa yako visa vya mauaji vimeongezeka si hao watoto pekee
 
Waendelee kuja tu kwa wingi, sio kila siku waende Nigeria au DRC!

Uzuri hiyo hela wanayotoa kwa waganga sisi tunapata kodi, maana mganga Tanzania lazima awe na kibali na analipia kodi kwa hiyo kazi yake
 
Ushirikina ndio nini? Kama mtu anatumia njia za Kiroho za Kiafrika kukabili maisha yake ya kila siku we inakuuma nini? Waganga wa huku kwetu wanasajiliwa na Wizara inayohusika na Ustawi wa Jamii na wanalipa mafungu serikalini, its kind of official business sir...
Waendelee kuja tu kwa wingi, sio kila siku waende Nigeria au DRC!

Uzuri hiyo hela wanayotoa kwa waganga sisi tunapata kodi, maana mganga Tanzania lazima awe na kibali na analipia kodi kwa hiyo kazi yake

Hapa mnazungumzia waganga miti shamba ama hawa wa kufanya mazingaombwe? There is difference btwn the two.

Hapa Kenya, waganga miti shamba is completely legal mradi tu uwe na cheti cha serikali. Na kuna wakati walikuwa wakidemand kutoitwa waganga mbali madaktari miti shamba.

Ule aina mwingine ya uganga is illegal, it is prosecutable by law.
 
Unashindwa Kuwashangaa wale wanao kwenda kuua Watoto wasio jua lolote kisa tu baba mwanasiasa!!
Tulia, ile haikuwa mauaji ya kisiasa, bali ugomvi ya kifamilia. Hapa Kenya kukiwa na such bitter rivalry ya kisiasa, most likely it is the rival candidates themselves who may be attacked and even killed, not their families.
 
Hapa mnazungumzia waganga miti shamba ama hawa wa kufanya mazingaombwe? There is difference btwn the two.

Hapa Kenya, waganga miti shamba is completely legal mradi tu uwe na cheti cha serikali. Na kuna wakati walikuwa wakidemand kutoitwa waganga mbali madaktari miti shamba.

Ule aina mwingine ya uganga is illegal, it is prosecutable by law.
Hao wanaokuja kupata hiyo huduma ndo wanatakiwa kutuweka sawa, kwamba wanaenda kwa wapi btn the two!
 
Hao wanaokuja kupata hiyo huduma ndo wanatakiwa kutuweka sawa, kwamba wanaenda kwa wapi btn the two!
Hujaelewa swali langu. Bila shaka hawa wanasiasa wanaenda kwa washirikina, sasa kwa hoja mlizotoa hapo juu, ni kweli serikali ya Tz inarecognize waganga wa aina hii mpaka kuwapa licence ya biashara?
 
Ushirikina/uchawi hauna recognition na serikali ya tz! Hapa tunatambua tiba mbadala na hawa ndio wanapewa vibali, na huwa mtu akithibitika kuwa huenda huwa anajihusisha na ushirikina kwa namna iwayo yote, mara moja hunyang'anywa kibali chake na anaweza kukutana na sheria kwa kukiuka mkataba!

Na ndio maana hata hao mnaosema wanakuja wanajificha kwa kuwa wanafanya kitu illegal!
 
Hamna tatizo kwa mtu kwenda kwa mtaalamu. Mbona hamsemi watu wanaoenda kuombewa makanisani na misikitini? Waafrika mmekuwa brainwashed na wazungu na waarabu, mtu akivaa rozari ama tasbihi haina shida kwenu lakini mtu akivaa hirizi mnamuona wa ajabu.

Kila mtu ana imani yake, sio lazima kila mtu afuate imani zenu za kigeni.
Ukweli mchungu na wazungu ndiyo wachawi haswa! Tumegundua! Hawana nguvu tena za kutufanya mazezeta!
 
Ukweli mchungu na wazungu ndiyo wachawi haswa! Tumegundua! Hawana nguvu tena za kutufanya mazezeta!

Uchawi gani zaidi ya kutafuna minofu ya albino, miafrika tumelaaniwa.
 
Uchawi gani zaidi ya kutafuna minofu ya albino, miafrika tumelaaniwa.
NAOMBA TAFADHALI SANA SEMA MIKENYA MMELAANIWA MAANA MTU ANAYE DHARAU KWAO NI MWENDAWAZIMU MTUMWA WA HALI YA JUU YEYE NA KIZAZI CHAKE MILELE YOTE, hakika umelaaniwa milele yote MK254!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom