BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Na Exuper Kachenje
05 June 2010
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)Rajabu Kiravu, akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya tume hiyo na viongozi wa vyama vya siasa Dar es Salaam jana. Kulia ni Makamu mwenyekiti wa Tume hiyo, Omar Makungu. Picha na Venance Nestory
WANASIASA wa vyama mbalimbali nchini jana waliibua mjadala mzito kwenye mkutano wao na Tume ya Uchaguzi (Nec) walipotoa hoja nzito za kutaka waruhusiwe kutumia lugha za makabila yao wakati wa kampeni kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Mkutano huo, uliofanyika jijini Dar es salaam, ulikuwa wa kujadili rasimu ya maadili ya uchaguzi, lakini ukatawaliwa na hoja hizo za lugha ya kutumia kwenye kampeni.
Mjadala huo mkali uliibuka katika baada ya mkurugenzi wa Nec, Rajab Kiravu kutoa mwongozo na kusoma mapendekezo na maoni yaliyotolewa na vyama hivyo pamoja na maoni ya Nec katika vipengere vya rasimu hiyo yenye kurasa 39.
Kipengere cha 2.1 (k) cha rasimu hiyo kinasema: "Kiswahili itakuwa ndiyo lugha pekee katika kampeni za Uchaguzi, pale ambapo Kiswahili hakieleweki na itakapolazimu, mgombea atazungumza Kiswahili na mkalimani atatafsiri katika lugha inayoeleweka katika eneo husika."
Kipengele hicho ndicho kilichoamsha hoja za wawakilishi hao wa vyama.
CCM, ambayo haikutuma mwakilishi, iliandika katika mapendekezo yake kuwa "mgombea anaweza kuzungumza Kiswahili na, au lugha inayoeleweka sehemu hiyo".
Lakini Chadema ilipingana na maoni hayo ikisema kuwa kutumia lugha ya sehemu hiyo ni ubaguzi wa lugha na au utamaduni, huku kikihoji sababu za Kiswahili kuwa lugha pekee kwenye kampeni.
Nec ilieleza katika maoni yake kuwa Kiswahili ndiyo lugha ya taifa inayoeleweka kwa Watanzania wote na kwamba kutumia lugha za kienyeji kutabagua watu wengine kwa kuwa hazifahamiki kwa Watanzania wote.
Ilieleza kuwa kuruhusu matumizi ya lugha hizo itakuwa ni kurudisha nyuma jitihada za serikali za kuleta umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania na kutaka kifungu hicho kibaki.
Lakini wadau hao, wengi wakiwa viongozi wa ngazi za juu wa vyama vya siasa, walipinga kwa nguvu huku Chama cha Wakulima (AFP) pekee kikiunga mkono matumizi ya Kiswahili.
"Hakuna ubaguzi katika kutumia lugha za makabila. Tusipotumia lugha za makabila ni sawa na kuukana Utanzania wetu ambao unaazia katika makabila yetu zaidi ya 120," alisema mwakilishi wa PPT Maendeleo.
Naye Julius Mtatiro kutoka CUF alisema: "Matumizi ya lugha za makabila hayaathiri maisha, wala uchaguzi. Ni vema wananchi waendelee kuongea lugha zao za makabila, mbona kiingereza tunaongea hata bungeni."
Tundu Lissu kutoka Chadema alisema: "Yapo maeneo watu hawawezi kuuliza swali kwa Kiswahili... sidhani kama ni dhambi ukienda wanapoongea Kinyaturu ukaongea Kinyaturu, haina maana kuongea Kiswahili wakati watu hawaelewi. Wananchi wapewe uhuru kutumia lugha zinazoeleweka maeneo yao."
Aliongeza kuwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza ibaki kama moja ya sharti kwa mgombea katika fomu za kuwania nafasi ya uongozi.
Hata hivyo, mkurugenzi wa Nec alikumbusha wajumbe wa mkutano huo kuwa suala la lugha lilijadiliwa kwa kina kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005 kwa kuwa inawezekana mgombea mmoja akawa si wa asili ya eneo hilo na kwamba sheria haizuii mtu kugombea mahali ambapo si asili yake.
Mkutano huo ulihudhuriwa na CUF, NLD, Chadema, TLP, NCCR, SAU, Tadea na AFP.
NEC imepanga tarehe nyingine ya kukutana na wadau hao kukamilisha mjadala huo kabla ya kutoa rasimu ya pili ya maadili hayo ya uongozi.
Mbali na mjadala wa lugha vyama vya siasa vilipinga kipengere cha 1.1.3 kinachoeleza wajibu wa kusaini maadili kikitaka kila chama cha siasa na kila mgombea kuwajibika kusaini maadili hayo na kwamba chama kitakachokataa kusaini maadili hayo na mgombea atakayefanya hivyo watakataliwa na kuondolewa kushiriki uchaguzi, wakisema kinakiuka katiba ya nchi.
Ufunguzi wa mkutano huo uliofanywa na makamu mwenyekiti wa Nec, Jaji Omar Makungu aliyeeleza kuwa wamepokea maoni kutoka vyama vinane vya siasa huku TLP ikiwasilisha maoni hayo jana asubuhi.
05 June 2010
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)Rajabu Kiravu, akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya tume hiyo na viongozi wa vyama vya siasa Dar es Salaam jana. Kulia ni Makamu mwenyekiti wa Tume hiyo, Omar Makungu. Picha na Venance Nestory
WANASIASA wa vyama mbalimbali nchini jana waliibua mjadala mzito kwenye mkutano wao na Tume ya Uchaguzi (Nec) walipotoa hoja nzito za kutaka waruhusiwe kutumia lugha za makabila yao wakati wa kampeni kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Mkutano huo, uliofanyika jijini Dar es salaam, ulikuwa wa kujadili rasimu ya maadili ya uchaguzi, lakini ukatawaliwa na hoja hizo za lugha ya kutumia kwenye kampeni.
Mjadala huo mkali uliibuka katika baada ya mkurugenzi wa Nec, Rajab Kiravu kutoa mwongozo na kusoma mapendekezo na maoni yaliyotolewa na vyama hivyo pamoja na maoni ya Nec katika vipengere vya rasimu hiyo yenye kurasa 39.
Kipengere cha 2.1 (k) cha rasimu hiyo kinasema: "Kiswahili itakuwa ndiyo lugha pekee katika kampeni za Uchaguzi, pale ambapo Kiswahili hakieleweki na itakapolazimu, mgombea atazungumza Kiswahili na mkalimani atatafsiri katika lugha inayoeleweka katika eneo husika."
Kipengele hicho ndicho kilichoamsha hoja za wawakilishi hao wa vyama.
CCM, ambayo haikutuma mwakilishi, iliandika katika mapendekezo yake kuwa "mgombea anaweza kuzungumza Kiswahili na, au lugha inayoeleweka sehemu hiyo".
Lakini Chadema ilipingana na maoni hayo ikisema kuwa kutumia lugha ya sehemu hiyo ni ubaguzi wa lugha na au utamaduni, huku kikihoji sababu za Kiswahili kuwa lugha pekee kwenye kampeni.
Nec ilieleza katika maoni yake kuwa Kiswahili ndiyo lugha ya taifa inayoeleweka kwa Watanzania wote na kwamba kutumia lugha za kienyeji kutabagua watu wengine kwa kuwa hazifahamiki kwa Watanzania wote.
Ilieleza kuwa kuruhusu matumizi ya lugha hizo itakuwa ni kurudisha nyuma jitihada za serikali za kuleta umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania na kutaka kifungu hicho kibaki.
Lakini wadau hao, wengi wakiwa viongozi wa ngazi za juu wa vyama vya siasa, walipinga kwa nguvu huku Chama cha Wakulima (AFP) pekee kikiunga mkono matumizi ya Kiswahili.
"Hakuna ubaguzi katika kutumia lugha za makabila. Tusipotumia lugha za makabila ni sawa na kuukana Utanzania wetu ambao unaazia katika makabila yetu zaidi ya 120," alisema mwakilishi wa PPT Maendeleo.
Naye Julius Mtatiro kutoka CUF alisema: "Matumizi ya lugha za makabila hayaathiri maisha, wala uchaguzi. Ni vema wananchi waendelee kuongea lugha zao za makabila, mbona kiingereza tunaongea hata bungeni."
Tundu Lissu kutoka Chadema alisema: "Yapo maeneo watu hawawezi kuuliza swali kwa Kiswahili... sidhani kama ni dhambi ukienda wanapoongea Kinyaturu ukaongea Kinyaturu, haina maana kuongea Kiswahili wakati watu hawaelewi. Wananchi wapewe uhuru kutumia lugha zinazoeleweka maeneo yao."
Aliongeza kuwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza ibaki kama moja ya sharti kwa mgombea katika fomu za kuwania nafasi ya uongozi.
Hata hivyo, mkurugenzi wa Nec alikumbusha wajumbe wa mkutano huo kuwa suala la lugha lilijadiliwa kwa kina kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005 kwa kuwa inawezekana mgombea mmoja akawa si wa asili ya eneo hilo na kwamba sheria haizuii mtu kugombea mahali ambapo si asili yake.
Mkutano huo ulihudhuriwa na CUF, NLD, Chadema, TLP, NCCR, SAU, Tadea na AFP.
NEC imepanga tarehe nyingine ya kukutana na wadau hao kukamilisha mjadala huo kabla ya kutoa rasimu ya pili ya maadili hayo ya uongozi.
Mbali na mjadala wa lugha vyama vya siasa vilipinga kipengere cha 1.1.3 kinachoeleza wajibu wa kusaini maadili kikitaka kila chama cha siasa na kila mgombea kuwajibika kusaini maadili hayo na kwamba chama kitakachokataa kusaini maadili hayo na mgombea atakayefanya hivyo watakataliwa na kuondolewa kushiriki uchaguzi, wakisema kinakiuka katiba ya nchi.
Ufunguzi wa mkutano huo uliofanywa na makamu mwenyekiti wa Nec, Jaji Omar Makungu aliyeeleza kuwa wamepokea maoni kutoka vyama vinane vya siasa huku TLP ikiwasilisha maoni hayo jana asubuhi.