Wanasiasa waliosingiziwa sana ni Kawawa, Lowassa na Ridhiwani pia wanasiasa waliosingizia sana ni Dr Slaa na Tundu Lissu!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,840
141,765
Moja kwa moja kwenye pointi ni kwamba kama kuna wanasiasa waliosingiziwa sana kwa habari za uongo nchi hii basi ni Kawawa rip wakati wa chama kimoja na mzee Lowassa na Ridhiwani Kikwete wakati wa vyama vingi.

Na wanasiasa wanaoongoza kwa kuwasingizia wenzao habari za uzushi ni Dr Slaa na Tundu Lisu na hasa baada ya kusimama pale Mwembeyanga na kuwashushia tuhuma za kutunga tu wanasiasa zaidi ya 10.

Sikushangaa pale Rais mstaafu Kikwete aliposema Chadema ni kiwanda cha uwongo.

Maendeleo hayana vyama!
 
Ridhiwani alisingiziwa nini na yeye ni mtoto sana kwenye siasa? Pengine kuwa alikuwa anajishuhulisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya!!!
 
Moja ya thread za kijinga sana kupata kujadiliwa JF.
Ukisingiziwa unakuwa umevunjiwa hadhi yako (defamation) na kwa sheria za nchi unayo nafasi kufungua shauri mahakamani ili aliyekusingizia awajibishwe na kukufidia.
Kwa nini walio singiziwa hawakwenda mahakamani hadi mtoto wao johnthebaptist aje awasafishe JF?
Mwizi ukimwita mwizi na kusema kaiba ng'ombe 10 wakati aliiba 4 hawezi shtaki kwani ukiambiwa udhibitishe utaishia ng'ombe wanne na hilo halimuondelei kosa la wizi wala wewe uliyetaja 10 halikuhukumu kwani bado yule ni mwizi ila ulikosea kiwango cha wizi wake!
 
Dr Slaa huwezi kumweka kundi moja na tundu by all means. Slaa is a man of integrity huweza kumlinganisha na huyo chokolaa tundu.

..Dr.Slaa alidai Mkapa alijaribu "kumhonga" nafasi ya ubalozi UN akakataa.

..miaka michache baadae Dr.Slaa amekubali nafasi ya ubalozi Sweden ambayo ni nafasi ya chini kulinganisha na kuwa balozi UN.
 
Kwani unadhani hivyo vitu HANA?
si ulimuona kwenye msiba wa Subhash Patel?
Riziwani alikuwa na majengo ,mahotel ,kampuni za.mafuta ,mabasi daaah yote hayo alipewa na wanachi enzj za babake akiwa rais

Ila wakati babake anastaafu tu wakampokonya Kila kitu wanamuachia ubunge
 
Moja ya thread za kijinga sana kupata kujadiliwa JF.
Ukisingiziwa unakuwa umevunjiwa hadhi yako (defamation) na kwa sheria za nchi unayo nafasi kufungua shauri mahakamani ili aliyekusingizia awajibishwe na kukufidia.
Kwa nini walio singiziwa hawakwenda mahakamani hadi mtoto wao johnthebaptist aje awasafishe JF?
Mwizi ukimwita mwizi na kusema kaiba ng'ombe 10 wakati aliiba 4 hawezi shtaki kwani ukiambiwa udhibitishe utaishia ng'ombe wanne na hilo halimuondelei kosa la wizi wala wewe uliyetaja 10 halikuhukumu kwani bado yule ni mwizi ila ulikosea kiwango cha wizi wake!
Hizi ndizo hoja za GT
 
Riziwani alikuwa na majengo ,mahotel ,kampuni za.mafuta ,mabasi daaah yote hayo alipewa na wanachi enzj za babake akiwa rais

Ila wakati babake anastaafu tu wakampokonya Kila kitu wanamuachia ubunge
Naona kuvuli cha mtu anayetaka kusafishwa, hii 2025 itatuchafulia majukwaa
 
Moja ya thread za kijinga sana kupata kujadiliwa JF.
Ukisingiziwa unakuwa umevunjiwa hadhi yako (defamation) na kwa sheria za nchi unayo nafasi kufungua shauri mahakamani ili aliyekusingizia awajibishwe na kukufidia.
Kwa nini walio singiziwa hawakwenda mahakamani hadi mtoto wao johnthebaptist aje awasafishe JF?
Mwizi ukimwita mwizi na kusema kaiba ng'ombe 10 wakati aliiba 4 hawezi shtaki kwani ukiambiwa udhibitishe utaishia ng'ombe wanne na hilo halimuondelei kosa la wizi wala wewe uliyetaja 10 halikuhukumu kwani bado yule ni mwizi ila ulikosea kiwango cha wizi wake!
Lowassa alisafishwa na mwanasheria mkuu wa Chadema mh Tundu Lisu mnamo mwaka 2015 pale viwanja vya jangwani.

Tundu Lisu ndiye aliyeandaa ile orodha ya mafisadi iliyosomwa na Dr Slaa pale Mwembe Yanga!
 
Hujamkuta Kambona na Nyerere wewe...
Yani Kambona aliimbiwa hadi nyimbo za chekechea...
Idd Amin na Nyerere.. hadi leo kuna watu hawamjui Amin lakini wanamchukia..

Siasa za uongo na propaganda ni za dunia nzima toka vizazi
Shuleni enzi hizo kwenye mchakamchaka tuliimba,,.....

.Amin Ana mimba ya dume la nyani aeeeee. Ya dume la nyani.....

Kweli uzushi ulikuwepo enzi na enzi kwenye siasa.
 
Back
Top Bottom