LINCOLINMTZA
JF-Expert Member
- Mar 15, 2011
- 1,640
- 516
Heshima zenu wote wanabodi wa vyama vyote, Kwa kweli nianze kukiri kwamba uwezo na muelekeo wa vijana katika siasa za Tanzania umekuwa ukikinzana sana na taaluma na maadili ya siasa yenyewe nchini na kutofautiana na wazee.
Ikumbukwe kwamba majuzi tu, vijana wa CCM wamekuja na kauli za kutaka umri wa uraisi urudishwe nyuma, yaani wagombeaji wawe waliozaliwa baada ya uhuru.
Hili suala lilileta hisia mbalimbali katika jamii ya kitanzania kwa kuzingatia kwamba kijana aliyesema hayo maneno ni kiongozi wa ngazi ya juu kabisa katika serikali. Kabla ya hapo, mwenyekiti wa BAVICHA mkoa wa Tanga naye amekuwa akijinadi kuwania uraisi bila hata kufuata taratibu za chama chake.
Kwa kuongezea, naibu katibu mkuu wa CDM naye amekuwa bega kwa bega na kauli yake ya kutaka kuwa raisi bila kujali katiba wala kanuni za chama chake.
Hii ni mifano michache sana katika vyama vya siasa nchini ambavyo vijana wajiaona kupevuka kwa sababu kwa vipimo vyao wenyewe na wala vya vyama au wananchi. Hii inapelekea wanasiasa wanaobwatauka tu bila kufikiria kabisa, wapiga kelele na wachumia tumbo tu.
Hii ndo inayopelekea vijana kukosa uvumilivu na mbinu za kukabiliana na changamoto za kisiasa nchini na kupelekea kurubuniwa kiraisi sana.Najua wanaJFs wana mifano mingi ya vijana wa namna hii katika siasa za nchi yetu.
Kwa hiyo, ninatoa wazo kwamba mwanasiasa yeyote kijana apewa mshauri/ msimamizi wake katika siasa ambaye atamshauri na kumlea katika harakati za kisiasa ili kuwajengea uwezo wa kupambanua mambo katika uwezo na uzoefu mkubwa.
Njia hii hutumiwa sana na chama cha ANC cha Afrika ya Kusini, kwa kuchukulia mfano, Julius Malema alikuwa chini ya uangalizi wa Winnie Madikizela-Mandela.
Nawakilisha wanabodi.
Ikumbukwe kwamba majuzi tu, vijana wa CCM wamekuja na kauli za kutaka umri wa uraisi urudishwe nyuma, yaani wagombeaji wawe waliozaliwa baada ya uhuru.
Hili suala lilileta hisia mbalimbali katika jamii ya kitanzania kwa kuzingatia kwamba kijana aliyesema hayo maneno ni kiongozi wa ngazi ya juu kabisa katika serikali. Kabla ya hapo, mwenyekiti wa BAVICHA mkoa wa Tanga naye amekuwa akijinadi kuwania uraisi bila hata kufuata taratibu za chama chake.
Kwa kuongezea, naibu katibu mkuu wa CDM naye amekuwa bega kwa bega na kauli yake ya kutaka kuwa raisi bila kujali katiba wala kanuni za chama chake.
Hii ni mifano michache sana katika vyama vya siasa nchini ambavyo vijana wajiaona kupevuka kwa sababu kwa vipimo vyao wenyewe na wala vya vyama au wananchi. Hii inapelekea wanasiasa wanaobwatauka tu bila kufikiria kabisa, wapiga kelele na wachumia tumbo tu.
Hii ndo inayopelekea vijana kukosa uvumilivu na mbinu za kukabiliana na changamoto za kisiasa nchini na kupelekea kurubuniwa kiraisi sana.Najua wanaJFs wana mifano mingi ya vijana wa namna hii katika siasa za nchi yetu.
Kwa hiyo, ninatoa wazo kwamba mwanasiasa yeyote kijana apewa mshauri/ msimamizi wake katika siasa ambaye atamshauri na kumlea katika harakati za kisiasa ili kuwajengea uwezo wa kupambanua mambo katika uwezo na uzoefu mkubwa.
Njia hii hutumiwa sana na chama cha ANC cha Afrika ya Kusini, kwa kuchukulia mfano, Julius Malema alikuwa chini ya uangalizi wa Winnie Madikizela-Mandela.
Nawakilisha wanabodi.