Wanasiasa Siku zingine msirudie tena hili Kosa kwani mnatuchosha na kuanza kutufanya tuwaone hamna tena jipya

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,865
Ni Ombi langu tu Kwenu Wanasiasa wote nchini Tanzania kwamba muwe mnajitahidi pale mkiwa mnaitisha ' Press Conferences ' zenu kuzungumzia mambo fulani / jambo fulani muwe mnatuambia Watanzania vile Vitu ' vizito vizito ' na ' muhimu ' Kwetu na siyo kutuambia vile Vitu ambavyo wengine tumekuwa tukivisikia tokea tukiwa Shule za Msingi hadi leo.

Halafu na kama mnajijua kabisa kuwa huwa mnakuwa hamna jipya na la maana basi acheni kuwapotezea muda Watanzania kwa kuwapa hamu ya Kujua jambo geni Kwao halafu baadae wanakuja kuyasikia yale yale ambayo wameshayasikia na wameyazoea. Mnatukera na kutufanya sasa tuwaone ni kama vile mmeishiwa Kisiasa.

Kuna haja gani ya Wewe / Nyie Kuitisha ' Press Conference ' kisha unakuja Kutueleza Watanzania jambo lile lile ambalo pengine Mwanasiasa mwenzako ambaye nae alikuwa katika hiyo hiyo ' situation ' kama yako au hata alikuzidi kidogo nae alishawahi Kutuelezea? Na nyie Waandishi wa Habari muwe mnajiongeza kwani kama mkiwa mnawaona hawa Wanasiasa wa Kitanzania wanawaita halafu wanaenda Kuongea kile kile acheni kuwa mnatuhabarisha kwani mnatuchosha kama siyo mnatuboa.

Namalizia kwa Kusisitiza kuwa Wanasiasa wa Tanzania acheni kuwafanya Watanzania ni Mambumbumbu / Mbayuwayu na Kutaka Kujipatia ' Kiki ' kupitia mambo ambayo mnayapitia ambayo mengineyo yamewagharimu kutokana na ' Upuuzi ' wenu halafu baadae mnatafuta huruma. Watanzania wa leo tunataka Kusikia au Kuambiwa mambo yenye Tija na Mantiki halafu yawe mazito hasa na siyo Utoto Utoto na Kulialia tu.

Uzi wangu huu uende kwa Wanasiasa na Vyama vyao vyote vya Kisiasa ambavyo wanaviwakilsha.

Nawasilisha.
 
Mkuu mambo hayo yalikuwa enzi za Jakaya!

Kipindi kile ukisikia Dr. Slaa kaitisha press conference ujue kuna bomu ambalo ccm nzima hadi ikulu inabaki kushngaa hili limetokaje?

Na linabaki kuwasumbua mwaka mzima

Sent using Jamii Forums mobile app
1.5 Trillioni mpaka leo haina majibu unataka watu waongee nini?

Ndio maana miradi ya world bank ya DMDP pesa wamewapa wakandarasi straight na wanasimania wenyewe miradi, hizi pesa wangepewa mchwa wa Lumumba zingepangiwa matumizi mengine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sure! Hawezi summary kabisa, headings zake zote ndefu, thread ndeeefu for nothing! Huu uzi ungeweza kuwa na paragraph moja tu!

Bado nawauliza Wewe na hao ' Wapumbavu ' Wenzako ambao Kutwa huwa mnasumbuka na kuhangaika na GENTAMYCINE kama mmeshajua Headings zangu huwa ni ndefu na wapo Watu ambao mnawajua wana Headings fupi kama Vibolo na Visimi vyenu sasa kwanini msiwe mnaachana na Mimi na muwe mnawasoma hao lakini Kutwa tu mnahangaika na Mimi? Narudia tena kusema kuwa siyo Kosa lenu Kupenda Kunifuatafuata bali najua kinachowateseni Kwangu ni hiki Kifuatacho...." Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer " na kwakuwa tayari nimeshajua kuwa kuna ' Wapumbavu ' wengi wakiongozwa na Wewe huwa hamlali na mnapata taabu na Mimi hivyo sasa nafanya Makusudi ' Kuwaudhi ' ili mpandwe na Hasira nami zaidi hadi mpasuke na nawahaadi nitawateseni na kuwasumbueni mno tu hapa.
 
Kenge kweli wew,ungesema wapinzani tu!Maana hapo unawasema wapinzani kwa mwamvuli wa vyama vyote!!!!Shwain,kama kwako si habari kwa wengine ni habari!!!!!!

Nionyeshe ni wapi nimevitaja Vyama vya Upinzani hasa hicho chako amacho Kimejaa ' Wapumbavu ' watupu kama alivyosema Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Mkapa viwanja wa Jangwani mwaka 2015. Maelezo yangu yapo wazi kabisa kuwa nimevitaja Vyama vyote vya Siasa nchini Tanzania kikiwemo hapa kile ambacho nakishabikia hivyo yoyote yule ambaye labda atahisi kuwa nimeanzisha huu ' Uzi ' kuwasema Wanasiasa fulani au Chama fulani cha Kisiasa basi atakuwa ni ' CERTIFIED IDIOT ' wa Kutukuka kabisa.
 
Back
Top Bottom