MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,639
- 33,414
Wakuu,
Naomba leo niseme na mabaraza yote na kila umoja wa Kikristo hapa Tanzania. Lipo jambo ambalo limemea hapa Tanzania na pengine halipo kwingine na ni aibu kwa Ukristo ingawa tunaweza kuona ni dogo.
Wakristo kuna madhehebu mengi sana lakini pamoja na tofauti zetu kubwa yapo mambo mengi pia ambayo hatutofautiani kwa wengi wetu. Ni ngumu kuondoa hizi tofauti lakini tofauti zingine ni za kijinga mno! Hivi kwanini tumebariki kuonesha TUMSIFU YESU KRISTO na Bwana YESU ASIFIWE zitumike kutugawa?
Najua kila upande unaweza kufafanua mantiki ya salamu yao lakini ni ujinga kutumia salamu hizi kuonesha utofauti wa madhehebu. Tofauti za madhehebu zipo wazi hazihitaji salamu kutofautisha.
Wenzetu Waislamu pamoja na tofauti zao lakini si kwenye salamu ambayo haina mantiki kutofautiana zaidi ya kuonesha ipo roho chafu zaidi ya tofauti zetu.
Natoa mwito kwa umoja wa madhehebu yote utoe tamko kuwa viongozi wote na wanasiasa watumie salamu moja wapo inatosha na inawakilisha UKRISTO. Kama mtu akisikia TUMSIFU YESU Kristo bila Bwana YESU asifiwe akanuna huyo anamtindio wa ubongo
Lakini pia kwenye hadhara ambayo si ya kidini nafikiri hizi salamu hazihitajiki hata kama viongozi wa dini wapo. Wanasiasa rekebisheni mazoea ya hizi salamu kwenye maeneo ambayo si lazima. Kwanza salamu zenyewe zinatugawa tu maana dini si mbili tu hapa Tanzania.
Tuachieni hizi salamu makanisani na misikitini
Naomba leo niseme na mabaraza yote na kila umoja wa Kikristo hapa Tanzania. Lipo jambo ambalo limemea hapa Tanzania na pengine halipo kwingine na ni aibu kwa Ukristo ingawa tunaweza kuona ni dogo.
Wakristo kuna madhehebu mengi sana lakini pamoja na tofauti zetu kubwa yapo mambo mengi pia ambayo hatutofautiani kwa wengi wetu. Ni ngumu kuondoa hizi tofauti lakini tofauti zingine ni za kijinga mno! Hivi kwanini tumebariki kuonesha TUMSIFU YESU KRISTO na Bwana YESU ASIFIWE zitumike kutugawa?
Najua kila upande unaweza kufafanua mantiki ya salamu yao lakini ni ujinga kutumia salamu hizi kuonesha utofauti wa madhehebu. Tofauti za madhehebu zipo wazi hazihitaji salamu kutofautisha.
Wenzetu Waislamu pamoja na tofauti zao lakini si kwenye salamu ambayo haina mantiki kutofautiana zaidi ya kuonesha ipo roho chafu zaidi ya tofauti zetu.
Natoa mwito kwa umoja wa madhehebu yote utoe tamko kuwa viongozi wote na wanasiasa watumie salamu moja wapo inatosha na inawakilisha UKRISTO. Kama mtu akisikia TUMSIFU YESU Kristo bila Bwana YESU asifiwe akanuna huyo anamtindio wa ubongo
Lakini pia kwenye hadhara ambayo si ya kidini nafikiri hizi salamu hazihitajiki hata kama viongozi wa dini wapo. Wanasiasa rekebisheni mazoea ya hizi salamu kwenye maeneo ambayo si lazima. Kwanza salamu zenyewe zinatugawa tu maana dini si mbili tu hapa Tanzania.
Tuachieni hizi salamu makanisani na misikitini