Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

huwezi kujua how correct uko kwenye hili. Msidhani wao watapigana hivyo vita shauri Mzee Mwanakijiji mimi nakubaliana kabisa na mawazo yako umeeleza vizuri sana kuwa vita si lelema lakini katika hali iliyofikiwa kuwa Mawalawi walikuwa tayari wamegawa blocks " vitalu"katika eneo lote la ziwa wakati wakijua wazi mazungumzo yalikuwa yanaendelea ni uchokozi ni tangazo la vita.Hivi unapovamia mipaka ya nchi nyingine unategemea nini kwa viongozi walie wanune au wacheke? Wamalawi walionesha kuyapuuza mazungumzo yaliyokuwa yanaendelea. Hi sawa na jamaa kukuchukulia mke wako na kwenda naye huku wewe ukiendelea kumchekea kuwa atamrudisha tu hapo baada au utazungumza nae ile hapa baadaye aache hilo halikubalini.Unapochokozwa si lazima wakati mwingine ujiandae unaweza kutumia nguvu uliyonayo kupambana na huyo mchokozi hata kama anakuzidi nguvu.Mimi naungana na Sitta, Membe na Lowasa katika kukemea hili.Uoga wetu utakuja kuuza nchi./QUOTE]
 
Sharti mojawapo ni lazima hawa watatu watoe watoto wao wa kiume kuwa mstari wa mbele ktk vikosi ikiwa tutaingia vitani. Vita si mchezo!

ha ha..Ningependa niwaone wale watoto wanajiita wenyewe kuwa ni watoto wa vigogo na wamekuwa na tabia ya kuchomoa ha hata kupiga risasi katika matukio ya sehemu za starehe wakigombea mademu.nadhani hiki ndicho kipindi chao cha kuonyesha si kwa mademu zao tuu bali kwa watanzania hamu yao ya kutumua bastola na kubwa zake.
 
Siungi mkono vita na siungi mkono nchi yetu kudharauliwa na taifa jingine kwa namna yoyote ile. Kauli za lowassa na sitta zinaweza kuonekana ni za kichochezi lakini zinatoa assurence kwamba usalama wetu na uhuru wetu unaweza kulindwa hata ikiwezekana kwa mtutu wa bunduki. Tukiongelea diplomacy tu, wamalawi watavimba vichwa na kuendelea kutuchokonoa usoni.
 
Right combination ya threat na diplomacy inaweza saidiana kuwa divide enemies.Wapo watu waliwahi survive majambazi(wakiwa na mapanga) katika mazingira ya kuogofya . I have a guy aliyekutwa na dhoruba la majambazi akiwa hata hana silaha na lipohisi kuwa walikuwa wakitaka kumua anyway hata kito auhsirikiano.Alichofanya ni kusoma mood ya lile kundi na kufahamu mwenye comand na aka predict results ya atakachofanya.Kwa mjumuiko wa hofu na kusema liwalo na liwe alipandisha sauti na kumpiga kiongozi kwa haraka na kwa nguvu zote, haakumini jinis alivyoweza lichukua lile panga na kunfanya aonekane kama katoto .Coincidence ni kwamba wale jamaa wengine walikuwa wakiamini kuwa kiongozi wao ni shupavu sana kiasi ,kwamba hata wote kwa pamoja hawawezi mshinda katika mpambano, na hivyo walichokiona kiliwafanya waone kuwa yule jamaa ni mara nyingi ya kiongzoi wao.So game liliisha kabla ya kuanza kwani wengine walikuwa kona, akabaki kiongozi wao pekee huku silaha yake ikiwa kwa adui.So jamaa kwa huruma alimwachia aondoke , huku akiwa nahofu kuu pengine akijiapiza kuwa akifika huko gheto jamaa zake walitosa watamkoma.

Personally naona kama serikali itajibahave kama grown up group of leaders, hakutakuwa na vita wala mgogoro na jumuia za kimataifa.Tunahitaji tumia parmaters nyingi kuwabana wamalawi.Lazima tu instigate fear kwa raia na viongozi wao tukiwa nyuma ya mlango, na diplomacy tukiwa hadharani.Lazima Pia tuwaweke mataifa muhimu katika state ya kuona bright future kuwa rafiki nasi pia kuwashindanisha kutugombea.Pia ni lazima tuwekeze kuwa na mamluki kwa kila level ndani ya malawi ili wawe koloni letu la kudumu.Bahati yao akina mangi wa rombo na Kibosho hawaongei lugha za huko?Tungewapa tender za kuenda nzisha bar za kila aina, ili no.1 wazinywe wenyewe hadi wapunguze nguvu na uzalendo wao.
 
Kinachofanyika ni kitu cha kawaida kabisa kwenye medani za siasa za kimataifa.Kauli kama hizi zina detterence effect.
Pia hii ni siasa ya kimataifa na tunakosea sana pale tunapoamini kwamba diplomasia inaweza kufanikiwa bila shinikizo.Suala la kuweka majeshi chini au kutoongelea millitary strength pia tutakosea na watu hawaelewi kwamba hata wakati wa vita Diplomasia bado inafanyika
Kutatua migogoro kwa njia ya kidiplomasia kuna:
-Kushawishi kabla ya kufikia hatua ya kutishana
-Kukirimu/kuhonga kwa ushawishi wa raslimali au mamlaka
-Lobbying ya kutafuta sapoti kwa jumuiya ya kimataifa
-Shinikizo la kijeshi au shinikizo la vikwazo vya kiuchumi(coercion)
-Ama vyote kwa pamoja

Pia kinachofanyika ni kuondoa sasa hofu wananchi na kuongeza ari ya jeshi na kama nilivyosema kuleta detterence effect kwa nchi hasimu.Hii ni propaganda ya kidiplomasia na haiepukiki

Malawi imeanza lini kuwa nchi hasimu hadi kuzungumza hii lugha ya vita?
 
Fisadi amepata pakutokea anaropoka 2 anfikiria vita ni sawa na ufisad wanaoufanya

mtu kama LE na mafisadi wenzake wanafikiria tender za ku-supply vifaru,AK 47,mabomu na silaha zingine bei na mauaji kama richmond
 
Back
Top Bottom