Wanasiasa mnatulazimisha kuwasaidia siasa

Unaponishangaza ni hapo unaposema eti 2020 hakuna mtu atasimama kwenye Foleni ya uchaguzi.



Mkuu Kama dunia ingekua na watu wanaofikiri na kukata tamaa hivyo dunia bado ingekua kwenye shimo la Giza totoro.

Kumbuka Mgurugenzi ni binadam kama wengine.
Asipodhibitiwa na kupata machungu atajiinua na kuangalia maslahi yake badala ya sheria kwa kuumiza wengine ili familia yake ishibe.
Eye with eye!
Kwenye mpira Refa aliyezoea kubeba timu yake , akijua kuwa timu pinzani wanajua kupigania haki yao na mashabiki wake wanajulikana kuwa hawana uvumilivu wa kuhujumiwa ni lazima refa afuate kanuni kuokoa pumzi yake.

Usifikirie hao CCM wanaofurahiya wizi wa kura hawajui kua kuiba kura ni kinyume na Vitabu vya duni,sheria za nchi na hata maadli ya binadam waliostarabika. Wanajua sana Ila wanachoangalia ni maslahi.
Mfamo Spika alituambiwa TL Mbunge kwa Mwaka mmoja amelipwa zaidi ya mil. 200 tena akiwa kitandani.
Chama tawala wanajua utam wa kushika funguo za hazina. Wanajua utam wa kushika dola.
Wapinzani bado wanashangaa shangaa wakati wenzao wanapambana.
Kila unayemuona anapambana kufa na kupona kutetea ugali wake.
Ukimuona anayegawa fomu anapigania ugali .Mlinzi anapigania ugali wake, anayegombea hasa wa chama tawala anataka agawiwe ugali wake kwa namna yoyote. Kama utakua na mgombea wa upinzani ambaye anasubiri apewe haki Mezani atapata makombo.

Usione watu wanahujumu wapinzani ni feza babu .
Wajipange kukabiliana na uovu wa kuhujumu zoezi la uchaguzi kwa namna yoyote mana wao ndio wanaotafuta nafasi za ubunge zenye maslahi na familia zao.

Kama mtu unapeleka mke wako kliniki Marekani halafu unalala kama ndezi uibiwe kura na vibaka halafu unabaki kulia badala ya kumliza mwizi ,utakua hujui umuhimu wa nafasi unayoitafuta.

Mtu unarudisha form peke yako barabarani halafu eti wanatokea vibaka wanakupora na wewe unabaki ukigaragara Chini kama mwehu badala ya kutafuta vijana wa kukusindikiza tena wakiwa na viberiti ili akijitokeza kibaka mporaji wa form basi anavuna anachopanda kama vibaka wengine.

Kila mtu alinde anachokitafuta kama ana uhakika wa kukipata.

Ni wazi kuwa Chama Kikongwe wamekua kama kundi la wapigaji wanaojipanga muda wote kufa na kupona ili tu washike nafasi za kuweza kuwapatia fedha za walipa kodi kwa UDI na uvumba. Hawa hawaangalii ubinadam wala sheria wanachojali ni kugawana nafasi za kupata hizo pesa.
Wakiachwa wanageuka kuwa kama wahalifu alimradi wapate nafsi hizo za ubunge ambazo zina maslahi makubwa.

Ww unaongea nadharia za kutokukubali hujuma, mimi nakuambia uhalisia. Kwa taarifa yako sina uoga hata chembe, nazungumzia jamii inayopaswa kuungana kuzuia hujuma. Jamii ni kama imeridhika, na wapinzani wenyewe wamechangia huu ukondoo kuingia kwenye jamii. Siwezi kwenda kupanga mstari na kuhatarisha usalama wangu kisha ninayemchagua anakwenda kuungana na waliohatarisha usalama wangu. Jamii itakapoamka na kuona inaumia itachukua hatua japo kwa machungu. Kwa sasa hapa jamii forums ndio uwanja wangu wa mapambano na ushahidi wa hiyo vita ni kilio cha huyu mleta uzi.
 
Ile 1.6 Bil ilipotelea enzi za kikwete au JPM.Huu ni umama.Halafu hakuna hoja.Wewe kimshahara chako unataka kufanana na mbunge?
Kwa mbunge inabidi ukope 1bil+.Huwezi ukamaliza ubunge na kuja kuuza kahawa vijiweni.Lazima uwe na mahali pa kujishika penye heshima.
Mawazo ya kimaskini yaishie kwako na familia yako.
Siwezi kujibu mmoja mmoja kwa sababu ninayo majukumu mengine,ili kuhakikisha familia yangu inapata haki yake.

Lakini hakika jiwe langu limewapata wengi wenu.
Kama kawaida ya dunia,ni vigumu kuwaridhisha binadamu wote kwa wakati mmoja.

Hili lilishindikana hata kwa enzi za mitume na manabii waliotutangulia,tunasoma katika vitabu vyote vya dini.ndio maana mpaka leo tunaomba kuendelea kusamehewa kila siku katika madhabahu na mimbari ya nyumba za ibada.

Wengi mlioko humu hamtetei wananchi kama mnavyojinadi,bali nyinyi na washirika wa mafanikio yenu.
Humu kuna kundi kubwa la wenye visasi zaidi kuliko wanasiasa wenye maslahi mapana na mwananchi wa kawaida.

Kuna mliozowea kuitumia siasa kama njia rahisi ya kufikia mafanikio kimaisha.
Ndio maana leo mbunge anathubutu kukopa milioni zaidi ya mia sita as if bunge ni saccos ya mikopo.
Hivi unamfikiriaje mbunge anayeingia bungeni na kukopa milioni zaidi ya mia sita?

Huyu atautumia muda wake mwingi kuhangaikia namna ya kutafuta vyanzo vya kumuwezesha kuipata hiyo milioni 600,ndani ya kipindi chake cha miaka mitano.

Je wananchi walimtuma akakope hiyo hela bungeni?
Au akawawakilishe wapiga kura wake kwa maslahi mapana ya jimbo lake!

Kwa hiyo na kwa sasa nimalizie hapo,kwa kuendelea kusema tuna wanasiasa na wanaharakati wengi humu JF,ambao hakika ni wasakatonge! Narudia tena ...wasakatonge hawana nafasi katika utawala wa JPM,iwe wako CCM,CHADEMA,ACT,CUF NCCR,nk.
Mheshimiwa magufuli (Hon president of URT)
Will stand for presidency 2020-2025.

#Tunasimama na JPM,2020-2025....

Asiyetaka ajitundike.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hakuna jiwe hapo.kuna biskuti tu na kwa kiburi hatuli bali tunazikanyaga.
kama hupendi kaanzishe forum yako halafu wanaoipinga serikali unawapiga ban kama kule fb na wasap.Huku ni hoja.unataka tusapoti ujinga wa akina Magonjwa mtambuka,stroke na wapuuzi wengine kama wewe,?hujui kusapoti upuuzi ni dhambi hata kwenye vitabu vya dini?

NB:jiulize kwa nini ID fake nyingi ni za kuisafisha serikali?zikishindwa zinapotea.
Narudia tena wengi wenu mmefika kwenye giza jiwe langu limewafikia na mtaendelea kupigwa mawe mengine na wengine kama mimi humu ndani?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo wewe unataka watu watekwe ,wafungwe kwenye viroba ,wauawe ,wafukuzwe kazi bila kufuata sheria na taratibu ,mikutano ya kisiasa izuiwe ,wabunge wa upinzani wabambikiwe kesi ,matilioni ya pesa yaibiwe tena kwa voti namba ishirini ya ikulu ,wafanyakazi wanyimwe nyongeza yao ya mishahara iliopo kisheria ,wanyime kupandishwa madaraja ,wafanyabiashara waporwe fedha zao kwenye maduka ya kigeni ,watu wafunguliwe kesi za uhujumu uchumi za uonezi ,uteuzi mbovu ,upendeleo ,ukabila ,kuvunjia watu nyumba zao ,kwa hiyo were mleta mada unataka tushangilie huu uoza wrote tusikosoe kiss anajenga reli na standard gauge hebu tumia akili wanaokosoa sio wajinga wanaakili zao timamu .Nyinyi mods mnapozuia hii post labda mnijulishe nimekosea wapiau nimemtukana nani? au ndio mmeungana na mleta mada poamoja na oppressors .
 
Hello members JF!

Hapo kabla,humu jukwaani palikuwa mahali huru na penye heshima ya kila mtu kuchangia kwa uhuru wake na kwa kiasi cha upeo wake.Lakini pia kwa utashi wa uhuru wake wa kuamini na kuchagua lile ambalo analisimamia katika imani yake iwe kisiasa,kidini au hata kielimu nk.
Na bila kuvunja kanuni na vifungu vya kikatiba ya JMT.

Sent using Jamii Forums mobile app
Bado JF ni jukwaa huru na ndio maana hata wewe umeandika hicho ulichoandika, japo unadai kwamba una msimamo "huru".

Hivi kwa nini unadhani serikali hii inapenda sana kuwanyang'anya watanzania uhuru wao? Maana ukiangalia yale magazeti ambayo hayaandiki msimamo wa serikali, yanaandamwa sana na hata kufungiwa kwa muda au kufutwa kabisa. Redio na TV ndio hivyo, zinatishwa kweli kweli, na nyingi zimenunuliwa ili ziongee na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa sana Dokta Profesa Magufuli. Badala yake yameibuka magazeti mengi sana yanayounga mkono juhudi. shida yake unaijua? watanzania wala hawahangaiki nayo!!! yanaishia kukausha bajeti za serikali sababu hayarudishi gharama. yanayonunuliwa zaidi ni yale ambayo yanaandika UKWELI na HAKI.

Sasa hivi hata bungeni watu wanatishwa wasitumie haki yao ya kisheria na kikatiba ya kutoa mawazo yao. mwangalie Spika Ndugai. bila aibu anaonesha chuki kwa waandishi wanaoamua kuondoka Bungeni na kuwafuata Wabunge wa upinzani wanaotoka nje. analia wivu kwamba wanaacha "mambo ya maana" na kufuata umbeya huko nje! Hivi toka lini Ndugai alisomea uandishi wa habari? Mwandishi ndiyo anajua kipi ni bora na kipi ni pumba. Yaani hata waandishi wanawakimbia mnawalazimisha tena kwa vitisho, wabaki bungeni na wabunge wa CCM?

Sasa na wewe umeangalia umeona kwamba pamoja na serikali ya CCM kuwaweka humu tena kwa malipo, bado mnazidiwa na umma wa watanzania ambao wala hawahitaji kulipwa chochote kusimamia mapambano ya kudai haki. mnashangaa kweli na inawauma sana mnapoona watanzania wapo tayari kumchangia mtu fedha ya matibabu, aliyenyimwa fedha za matibabu na serikali na sasa hivi kanyimwa mshahara. Yaani wivu wa chuki umewajaa, hadi mlikuwa mnakamata waliokuwa wanajitolea kuchangia damu, siyo kwa ajili ya kupeleka Nairobi kumtibu Tundu Lissu, bali kama ishara ya kufidia damu aliyoongezewa mpambanaji huyo. Yaani pamoja na shida kubwa ya damu tuliyonayo, watu wengi wanapoteza maisha kwa kukosa damu, mkasema potelea mbali!!! WAUWAJI WAKUBWA NYIE.

JF ni jukwaa huru, linapokea kila mtu, hata wewe unayelipwa ili kuitetea serikali. Huyo Magufuli kama anapendwa hivyo, mbona anazuia watu kuonesha MAHABA yao kwa wale wawapendao?????
 
Hello members JF!

Nawaheshimu na nitaendelea kuwaheshimu wale tutakaoweza kuheshimiana.

Moderator naomba usiniunganishe popote na hii topic yangu.

Hapo kabla,humu jukwaani palikuwa mahali huru na penye heshima ya kila mtu kuchangia kwa uhuru wake na kwa kiasi cha upeo wake.Lakini pia kwa utashi wa uhuru wake wa kuamini na kuchagua lile ambalo analisimamia katika imani yake iwe kisiasa,kidini au hata kielimu nk.
Na bila kuvunja kanuni na vifungu vya kikatiba ya JMT.

Lakini baadae na kwa taratibu,jukwaa hili likaanza kuvamiwa na watu ambao wanataka kuligeuza kama platform yenye mlengo mmoja wenye nia moja,na pia wenye kusudio moja.
Nalo ni kuwa kama tawi la wanaharakati na wanasiasa wenye mlengo tofauti na serikali.Na imegeuka kuwa yeyote yule anaye changia mawazo yake huru,na akaonekana kuwa upande wa serikali,basi huyo ataonekana humu kama mtu anayestahili matusi,kejeli au hata kuitwa majina ya ajabu ajabu tu.(moderators mpo na mko kimya).

Na humu mnataka kuligeuza jukwaa la watu wa mlengo wa anti-goverment.
Wakati mkilaumu serikali ya CCMkuwa inaminya demokrasia nchini.
Nyinyi humu mnaminya demokrasia ya uhuru wa watu wengine kutoa maoni yao.mnatukana watu ovyo bila hata kuwa na staha.

Wakati mkifanya hayo,bila kujua kwamba wengi wa wachangiaji humu,sio na wala hawajawahi kufanya siasa kuwa njia ya kuwapatia kipato cha kimaisha.(kama ambavyo wengi wa wanasiasa Tanzania mlivyo).

Wengi mlichokisomea na kufeli mitihani sio mnachokifanya(sio wanasiasa wote)kuna wanasiasa vijana wazuri na wanafanya siasa nzuri na wanastahili pongezi,ila kuna hili kundi ambalo mliingia kwenye short cut za siasa kupitia ubishi wenu mkiwa vyuoni na mkaishia kufeli masomo kwa kuendekeza aidha uwaziri,unaibu rais wa majukwaa na jumuia mbalimbali vyuoni(ambazo si za kitaaluma rasmi).kubishana na taasisi za uongozi rasmi vyuoni.

Sasa mmeshindwa siasa za kwenye ulingo wa siasa,aidha kwa kutotimia kwa malengo yenu kupitia ubanwaji wa vyanzo vya mapato kupitia nyadhifa za kisiasa(kutokana na sera za JPM).

Sasa JF inageuka taratibu kuwa likichaka la watu waliojawa na hasira za majeruhi mbalimbali kama vile vyeti hewa,mishahara hewa,wabunge na wafuasi fulani fulani wanaochukia misimamo ya Mheshimiws Rais JPM,wale ambao walikuwa wategemezi wa ndugu na jamaa zao au hata wazazi wao ambao wamekutana na rungu la JPM mahali fulani.na kuwatibulia ndoto zao kutokana na pato haramu.
Lakini pia lipo kundi la wakosa uteuliwa na watumbuliwa na ndugu zao pia.

Sasa kwa sababu humu ni hidden identity mnakuja huku mkiwa mmejaa sumu kama Cobra,mnatukana ovyo,huku mkijiaminisha kwamba kutoona members wengi kuwafuatilia basi eti hiyo ni ticket ya popular majority of the wining

Mnajidanganya,
Ukweli ni kwamba watu wengi siku hizi wanapotezea kiaina,kwa kuchoshwa na utumbo unaolazimishwa humu ndani,matusi na kejeli humu JF.
lakini pia mod's pia wamekuwa kama marefarii wa mechi za mchangani.(ushahidi ni avatar utitiri zinazojirudia rudia humu au kufunguliwa na kupotea baada ya muda mfupi).

Siku hizi ukitaka ugombaniwe na vyama fulani fulani,wewe tafuta bifu na kiongozi yeyote yule wa CCM.
Au ukitaka uteuliwe kugombea vyama fulani basi jitowe muhanga hata ugongwe na gari la mwenyekiti wa wilaya wa CCM,(kama urajeruhiwana kupona)hapo utakuwa lulu humu JF.
Hata ticket ya ndege utakatiwa ili utibiwe vizuri ukirudi utapewa ugombea.
Nasema haya kwa kuzingatia ninayoyaona kwenye siasa uchwara za kitanzania sasa hivi.

Hivyo bila kujua taratibu watu makini wanasepa humu na kuendelea na maisha yao ya kawaida.
Wakati huo mnajiaminisha mko top,lakini ukweli ni kwamba watu makini wanakiona kinachoendelea kufanywa na serikali hii,na wanasubiri uchaguzi ili wampe huyu mzee JPM haki yake hadi 2025

Wananchi walikuwa wakiomba huduma bora za kijamii kama haki yao ya kikatiba,kutokana na kodi wanazolipa.
Na huo ndio msingi mkuu wa JPM na sio haki za kuandamana,uhuru wa vyombo vya habari na siasa za majukwaani.
Hivyo vitu ni muhimu lakini sio kipaumbele cha common mwananchi.

Ni kipaumbele cha wanasiasa na wanufaika wa vyanzo mbalimbali vitokanavyo na mapato husika ya taasisi zao,kulingana na taasisi zinazowafadhili.

Hivyo msiwalazimishe watanzania woote kulia kilio cha kisiasa.
Mnapopata nyafhifa zenu,wengi wenu hunufaisha ndugu na jamaa zenu,huku mkitulambisha asali kwa ncha ya kisu.
Ndio maana mnapokosa kilio kinatokea pande nyiingi,lakini sio pande zoote.
Nawakilisha ukweli wangu,mkitukana shauri yenu lakini nasimama na # Magufuli 2025#




Sent using Jamii Forums mobile app
Nashukuru tuko wengi tunaliona hilo ,asante,na huo ndio ukweli wenyewe,acha wapunguze maumivu,ila watabiki wao siku moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom