commonmwananchi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 3,377
- 1,952
Hello members JF!
Nawaheshimu na nitaendelea kuwaheshimu wale tutakaoweza kuheshimiana.
Moderator naomba usiniunganishe popote na hii topic yangu.
Hapo kabla,humu jukwaani palikuwa mahali huru na penye heshima ya kila mtu kuchangia kwa uhuru wake na kwa kiasi cha upeo wake.Lakini pia kwa utashi wa uhuru wake wa kuamini na kuchagua lile ambalo analisimamia katika imani yake iwe kisiasa,kidini au hata kielimu nk.
Na bila kuvunja kanuni na vifungu vya kikatiba ya JMT.
Lakini baadae na kwa taratibu,jukwaa hili likaanza kuvamiwa na watu ambao wanataka kuligeuza kama platform yenye mlengo mmoja wenye nia moja,na pia wenye kusudio moja.
Nalo ni kuwa kama tawi la wanaharakati na wanasiasa wenye mlengo tofauti na serikali.Na imegeuka kuwa yeyote yule anaye changia mawazo yake huru,na akaonekana kuwa upande wa serikali,basi huyo ataonekana humu kama mtu anayestahili matusi,kejeli au hata kuitwa majina ya ajabu ajabu tu.(moderators mpo na mko kimya).
Na humu mnataka kuligeuza jukwaa la watu wa mlengo wa anti-goverment.
Wakati mkilaumu serikali ya CCMkuwa inaminya demokrasia nchini.
Nyinyi humu mnaminya demokrasia ya uhuru wa watu wengine kutoa maoni yao.mnatukana watu ovyo bila hata kuwa na staha.
Wakati mkifanya hayo,bila kujua kwamba wengi wa wachangiaji humu,sio na wala hawajawahi kufanya siasa kuwa njia ya kuwapatia kipato cha kimaisha.(kama ambavyo wengi wa wanasiasa Tanzania mlivyo).
Wengi mlichokisomea na kufeli mitihani sio mnachokifanya(sio wanasiasa wote)kuna wanasiasa vijana wazuri na wanafanya siasa nzuri na wanastahili pongezi,ila kuna hili kundi ambalo mliingia kwenye short cut za siasa kupitia ubishi wenu mkiwa vyuoni na mkaishia kufeli masomo kwa kuendekeza aidha uwaziri,unaibu rais wa majukwaa na jumuia mbalimbali vyuoni(ambazo si za kitaaluma rasmi).kubishana na taasisi za uongozi rasmi vyuoni.
Sasa mmeshindwa siasa za kwenye ulingo wa siasa,aidha kwa kutotimia kwa malengo yenu kupitia ubanwaji wa vyanzo vya mapato kupitia nyadhifa za kisiasa(kutokana na sera za JPM).
Sasa JF inageuka taratibu kuwa likichaka la watu waliojawa na hasira za majeruhi mbalimbali kama vile vyeti hewa,mishahara hewa,wabunge na wafuasi fulani fulani wanaochukia misimamo ya Mheshimiws Rais JPM,wale ambao walikuwa wategemezi wa ndugu na jamaa zao au hata wazazi wao ambao wamekutana na rungu la JPM mahali fulani.na kuwatibulia ndoto zao kutokana na pato haramu.
Lakini pia lipo kundi la wakosa uteuliwa na watumbuliwa na ndugu zao pia.
Sasa kwa sababu humu ni hidden identity mnakuja huku mkiwa mmejaa sumu kama Cobra,mnatukana ovyo,huku mkijiaminisha kwamba kutoona members wengi kuwafuatilia basi eti hiyo ni ticket ya popular majority of the wining
Mnajidanganya,
Ukweli ni kwamba watu wengi siku hizi wanapotezea kiaina,kwa kuchoshwa na utumbo unaolazimishwa humu ndani,matusi na kejeli humu JF.
lakini pia mod's pia wamekuwa kama marefarii wa mechi za mchangani.(ushahidi ni avatar utitiri zinazojirudia rudia humu au kufunguliwa na kupotea baada ya muda mfupi).
Siku hizi ukitaka ugombaniwe na vyama fulani fulani,wewe tafuta bifu na kiongozi yeyote yule wa CCM.
Au ukitaka uteuliwe kugombea vyama fulani basi jitowe muhanga hata ugongwe na gari la mwenyekiti wa wilaya wa CCM,(kama urajeruhiwana kupona)hapo utakuwa lulu humu JF.
Hata ticket ya ndege utakatiwa ili utibiwe vizuri ukirudi utapewa ugombea.
Nasema haya kwa kuzingatia ninayoyaona kwenye siasa uchwara za kitanzania sasa hivi.
Hivyo bila kujua taratibu watu makini wanasepa humu na kuendelea na maisha yao ya kawaida.
Wakati huo mnajiaminisha mko top,lakini ukweli ni kwamba watu makini wanakiona kinachoendelea kufanywa na serikali hii,na wanasubiri uchaguzi ili wampe huyu mzee JPM haki yake hadi 2025
Wananchi walikuwa wakiomba huduma bora za kijamii kama haki yao ya kikatiba,kutokana na kodi wanazolipa.
Na huo ndio msingi mkuu wa JPM na sio haki za kuandamana,uhuru wa vyombo vya habari na siasa za majukwaani.
Hivyo vitu ni muhimu lakini sio kipaumbele cha common mwananchi.
Ni kipaumbele cha wanasiasa na wanufaika wa vyanzo mbalimbali vitokanavyo na mapato husika ya taasisi zao,kulingana na taasisi zinazowafadhili.
Hivyo msiwalazimishe watanzania woote kulia kilio cha kisiasa.
Mnapopata nyafhifa zenu,wengi wenu hunufaisha ndugu na jamaa zenu,huku mkitulambisha asali kwa ncha ya kisu.
Ndio maana mnapokosa kilio kinatokea pande nyiingi,lakini sio pande zoote.
Nawakilisha ukweli wangu,mkitukana shauri yenu lakini nasimama na # Magufuli 2025#
Sent using Jamii Forums mobile app
Nawaheshimu na nitaendelea kuwaheshimu wale tutakaoweza kuheshimiana.
Moderator naomba usiniunganishe popote na hii topic yangu.
Hapo kabla,humu jukwaani palikuwa mahali huru na penye heshima ya kila mtu kuchangia kwa uhuru wake na kwa kiasi cha upeo wake.Lakini pia kwa utashi wa uhuru wake wa kuamini na kuchagua lile ambalo analisimamia katika imani yake iwe kisiasa,kidini au hata kielimu nk.
Na bila kuvunja kanuni na vifungu vya kikatiba ya JMT.
Lakini baadae na kwa taratibu,jukwaa hili likaanza kuvamiwa na watu ambao wanataka kuligeuza kama platform yenye mlengo mmoja wenye nia moja,na pia wenye kusudio moja.
Nalo ni kuwa kama tawi la wanaharakati na wanasiasa wenye mlengo tofauti na serikali.Na imegeuka kuwa yeyote yule anaye changia mawazo yake huru,na akaonekana kuwa upande wa serikali,basi huyo ataonekana humu kama mtu anayestahili matusi,kejeli au hata kuitwa majina ya ajabu ajabu tu.(moderators mpo na mko kimya).
Na humu mnataka kuligeuza jukwaa la watu wa mlengo wa anti-goverment.
Wakati mkilaumu serikali ya CCMkuwa inaminya demokrasia nchini.
Nyinyi humu mnaminya demokrasia ya uhuru wa watu wengine kutoa maoni yao.mnatukana watu ovyo bila hata kuwa na staha.
Wakati mkifanya hayo,bila kujua kwamba wengi wa wachangiaji humu,sio na wala hawajawahi kufanya siasa kuwa njia ya kuwapatia kipato cha kimaisha.(kama ambavyo wengi wa wanasiasa Tanzania mlivyo).
Wengi mlichokisomea na kufeli mitihani sio mnachokifanya(sio wanasiasa wote)kuna wanasiasa vijana wazuri na wanafanya siasa nzuri na wanastahili pongezi,ila kuna hili kundi ambalo mliingia kwenye short cut za siasa kupitia ubishi wenu mkiwa vyuoni na mkaishia kufeli masomo kwa kuendekeza aidha uwaziri,unaibu rais wa majukwaa na jumuia mbalimbali vyuoni(ambazo si za kitaaluma rasmi).kubishana na taasisi za uongozi rasmi vyuoni.
Sasa mmeshindwa siasa za kwenye ulingo wa siasa,aidha kwa kutotimia kwa malengo yenu kupitia ubanwaji wa vyanzo vya mapato kupitia nyadhifa za kisiasa(kutokana na sera za JPM).
Sasa JF inageuka taratibu kuwa likichaka la watu waliojawa na hasira za majeruhi mbalimbali kama vile vyeti hewa,mishahara hewa,wabunge na wafuasi fulani fulani wanaochukia misimamo ya Mheshimiws Rais JPM,wale ambao walikuwa wategemezi wa ndugu na jamaa zao au hata wazazi wao ambao wamekutana na rungu la JPM mahali fulani.na kuwatibulia ndoto zao kutokana na pato haramu.
Lakini pia lipo kundi la wakosa uteuliwa na watumbuliwa na ndugu zao pia.
Sasa kwa sababu humu ni hidden identity mnakuja huku mkiwa mmejaa sumu kama Cobra,mnatukana ovyo,huku mkijiaminisha kwamba kutoona members wengi kuwafuatilia basi eti hiyo ni ticket ya popular majority of the wining
Mnajidanganya,
Ukweli ni kwamba watu wengi siku hizi wanapotezea kiaina,kwa kuchoshwa na utumbo unaolazimishwa humu ndani,matusi na kejeli humu JF.
lakini pia mod's pia wamekuwa kama marefarii wa mechi za mchangani.(ushahidi ni avatar utitiri zinazojirudia rudia humu au kufunguliwa na kupotea baada ya muda mfupi).
Siku hizi ukitaka ugombaniwe na vyama fulani fulani,wewe tafuta bifu na kiongozi yeyote yule wa CCM.
Au ukitaka uteuliwe kugombea vyama fulani basi jitowe muhanga hata ugongwe na gari la mwenyekiti wa wilaya wa CCM,(kama urajeruhiwana kupona)hapo utakuwa lulu humu JF.
Hata ticket ya ndege utakatiwa ili utibiwe vizuri ukirudi utapewa ugombea.
Nasema haya kwa kuzingatia ninayoyaona kwenye siasa uchwara za kitanzania sasa hivi.
Hivyo bila kujua taratibu watu makini wanasepa humu na kuendelea na maisha yao ya kawaida.
Wakati huo mnajiaminisha mko top,lakini ukweli ni kwamba watu makini wanakiona kinachoendelea kufanywa na serikali hii,na wanasubiri uchaguzi ili wampe huyu mzee JPM haki yake hadi 2025
Wananchi walikuwa wakiomba huduma bora za kijamii kama haki yao ya kikatiba,kutokana na kodi wanazolipa.
Na huo ndio msingi mkuu wa JPM na sio haki za kuandamana,uhuru wa vyombo vya habari na siasa za majukwaani.
Hivyo vitu ni muhimu lakini sio kipaumbele cha common mwananchi.
Ni kipaumbele cha wanasiasa na wanufaika wa vyanzo mbalimbali vitokanavyo na mapato husika ya taasisi zao,kulingana na taasisi zinazowafadhili.
Hivyo msiwalazimishe watanzania woote kulia kilio cha kisiasa.
Mnapopata nyafhifa zenu,wengi wenu hunufaisha ndugu na jamaa zenu,huku mkitulambisha asali kwa ncha ya kisu.
Ndio maana mnapokosa kilio kinatokea pande nyiingi,lakini sio pande zoote.
Nawakilisha ukweli wangu,mkitukana shauri yenu lakini nasimama na # Magufuli 2025#
Sent using Jamii Forums mobile app