Jibaba Bonge
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,246
- 401
Huko nyuma wakati wa uongozi wa Mwl. Nyerere watu wote tuliitana ndugu; raisi aliitwa ndugu raisi, Spika ndugu spika, mbunge ndugu mbunge, waziri ndugu waziri na watu wasiokuwa na cheo chochote cha kisiasa pia waliitwa ndugu ndugu fulani.
Wabunge wetu kwa kutumia kodi zetu wakajadili mswaada bungeni na kupitisha (sijui kwa faida ya nani na kwa tija ipi?) kuwa wao (wabunge, Spika, mawaziri n.k) waitwe waheshimiwa na raisi aitwe mtukufu!!! eti Mheshimiwa mbunge fulani, mtukufu raisi!!
Ikiwa hizo title za mheshimiwa na mtukufu ni za hao wanasiasa je wale wasio katika makundi hayo ya kisiasa walipewa title gani? Kama hao waliotajwa ndiyo waheshimiwa na watukufu basi wasiokuwepo katika makundi hayo ya kisiasa hawaheshimiwi na wala siyo watukufu!
Pamoja na title kubwa kubwa walizo jipa wameendelea kufanya madudu katika uongozi wa nchi yetuHali hii imeleta matabaka makubwa kati ya waheshimiwa na wasioheshimiwa na kuwafanya watu watafute kuitwa waheshimiwa kwa gharama yoyote.
Hivi Title ya ndugu kwa wanasiasa ilikuwa na mapungufu gani?
Wabunge wetu kwa kutumia kodi zetu wakajadili mswaada bungeni na kupitisha (sijui kwa faida ya nani na kwa tija ipi?) kuwa wao (wabunge, Spika, mawaziri n.k) waitwe waheshimiwa na raisi aitwe mtukufu!!! eti Mheshimiwa mbunge fulani, mtukufu raisi!!
Ikiwa hizo title za mheshimiwa na mtukufu ni za hao wanasiasa je wale wasio katika makundi hayo ya kisiasa walipewa title gani? Kama hao waliotajwa ndiyo waheshimiwa na watukufu basi wasiokuwepo katika makundi hayo ya kisiasa hawaheshimiwi na wala siyo watukufu!
Pamoja na title kubwa kubwa walizo jipa wameendelea kufanya madudu katika uongozi wa nchi yetuHali hii imeleta matabaka makubwa kati ya waheshimiwa na wasioheshimiwa na kuwafanya watu watafute kuitwa waheshimiwa kwa gharama yoyote.
Hivi Title ya ndugu kwa wanasiasa ilikuwa na mapungufu gani?