Wanasheria Wetu Tanzania na Uzalendo Wao Kwa Taifa

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Wameelimika na wanajua mengi. Tunawategemea, kuwathamini na tungependa kuwaenzi. Lakini kabla hatujaanza kuwaenzi, labda tujiulize, hivi wengi wao na kampuni zao na jumuiya zao mbalimbali kweli wanathamini Taifa hili?

Najiuliza kama wanathamini uzalendo au wana uzalendo wowote ule kutokana na mlolongo wa madudu ya kifisadi kwenye mikataba mbalimbali nchi hii imepata kuingia na mashirika au kampuni mbalimbali za nje, haswa kwenye sekta ya madini na nishati.

Hivi kweli chi yetu inapokuwa inapunjwa kila pahala wako wapi hawa? Najua wanafahamu sehemu za kurekebisha na sehemu zenye makosa, wako privy na mambo mengi yanayotokea kwenye maslahi ya Taifa lakini kwanini wako kimya? Je kila mmoja anajali maslahi yake tu binafsi? Wana uzalendo wowote kweli hawa??!!!
 
Adui wako mwombee njaa...nafikiri
kwanza wana njaa,
Pili: uzalendo ni zao haki na usawa..kama wao wanaona wanasiasa wanaponda mali nao wanajinafasi,
Tatu: wananchi wanatakiwa wawasute hao wanasheria na technorat wengine wengi tu kwenye system...niliwahi kusema kwenye thread moja ya rev. kishoka nchi inaliwa na less than 10% of the population of 40 mil. people unfairly
Nne:Ondoa takataka inaitwa CCM madarakani overhaul the system..kwasababu msingi yetu tangu Nyerere, Mwinyi, Mkapa na JK ni pata potea...msingi mbovu nyumba haitasimama kila siku kutakuwa na nyufa..na kila mvua kubwa lazima uombe msaada kwa jirani..
 
Steve!!

Kuna mtu alisema ishara kubwa ya nchi iliyo corrupt na weak governance ni rich lawyers and poor clients

Huwezi ukawa na uzalendo ukiwa corrupt!!!
Think about it!!!
 
Steve!!

Kuna mtu alisema ishara kubwa ya nchi iliyo corrupt na weak governance ni rich lawyers and poor clients

Huwezi ukawa na uzalendo ukiwa corrupt!!!
Think about it!!!

Kwa kweli mimi naona hili tabaka kama anavyolisema Tumaini (haswa wanasheria) ni moja ya kikwazo kikubwa cha maendeleo ya nchi yetu iwapo tabaka hili linakuwa corrupt.

Wewe hebu fikiria tu: uwe na corrupt doctors mahospitalini, au uwe na corrupt soldiers, uwe na corrupt professors chuoni, etc, etc... hawa wote sidhani kama watafua dafu kama wanakamatwa na sheria inafuata mkondo wake.
Hivyo basi, wanasheria ni kiuongo muhimu sana cha Taifa hili lakini naona na ndicho kilichokuwa more corrupt kwa sasa kutokana na mambo yanavyoenda. Nipale wanasheria wanapokiuka maadili yao na kuendeleza tamaa zao binafsi ndipo hapo Taifa linapoangamia na haki kuonekana haipatikani au kutokuwepo kabisa.
 
Ninakubali. Kila scandal ya wizi wa fedha za umma, lazima mastermind ni mwanasheria. Mfano mzuri ni makala iliyochapishwa na The EastAfrican [few months ago] kuhusu Dr. Sinare kununua nyumba za NSSF kinyume na utaratibu. Huyu mwanazuoni akatoa tamko [press release or something] kukanusha hiyo taarifa na kuelezea uhalali wa deal kati yake na NSSF. Kimsingi hakuna alichoeleza zaidi ya kujikaanga. Na ukiliangalia hili swala utaona kuwa si rahisi kufanikisha mpango ule kama wewe si mwanasheria au kumuhusisha mwanasheria.

Mkereketwa mmoja aliandika barua kwa mhariri (The EastAfrican or Business Times) na kubainisha kuwa wanasheria wa nchi hii [akiwemo Dr. Sinare] ndio wanaorudisha maendeleo ya taifa hili nyuma. Wamesomeshwa kwa pesa za walipa kodi lakini matokeo yake wamegeuka na kuwasaliti waliowasomesha. Wanatuibia. Wanawezesha wizi kufanyika. Wanawatetea wezi mahakamani kwa kutumia maarifa waliyoyapata kupitia pesa za walipa kodi. The bottom line: katika fani ambazo ni adui wa maendeleo ya mtanzania ni uanasheria.
 
Ninakubali. Kila scandal ya wizi wa fedha za umma, lazima mastermind ni mwanasheria. Mfano mzuri ni makala iliyochapishwa na The EastAfrican [few months ago] kuhusu Dr. Sinare kununua nyumba za NSSF kinyume na utaratibu. Huyu mwanazuoni akatoa tamko [press release or something] kukanusha hiyo taarifa na kuelezea uhalali wa deal kati yake na NSSF. Kimsingi hakuna alichoeleza zaidi ya kujikaanga. Na ukiliangalia hili swala utaona kuwa si rahisi kufanikisha mpango ule kama wewe si mwanasheria au kumuhusisha mwanasheria.

Mkereketwa mmoja aliandika barua kwa mhariri (The EastAfrican or Business Times) na kubainisha kuwa wanasheria wa nchi hii [akiwemo Dr. Sinare] ndio wanaorudisha maendeleo ya taifa hili nyuma. Wamesomeshwa kwa pesa za walipa kodi lakini matokeo yake wamegeuka na kuwasaliti waliowasomesha. Wanatuibia. Wanawezesha wizi kufanyika. Wanawatetea wezi mahakamani kwa kutumia maarifa waliyoyapata kupitia pesa za walipa kodi. The bottom line: katika fani ambazo ni adui wa maendeleo ya mtanzania ni uanasheria.

Kuna pahala nilisoma, almost 2 years ago kwenye web, nimejaribu kutafuta hiyo document siipati, maana siku-save, na web yao wamebadilisha. Ilikuwa inahusiana na mission statement na dominance ya Rex Attorneys kwenye sector ya energy Tanzania. Walichokisema wakati huo open kabla ya scandal la Richmond halijatemesha watu Bungeni ilikuwa - wanahodhi karibia mikataba yote inayohusiana na sekta ya nishati pasipokuwa mkataba wa Richmond. Nilisita nakujiuliza, kwanini hawakujiingiza katika huu mkataba kama guarantors?! Nachelea kusema kuwa, lazima walijua madudu yaliyokuwemo mle. Na kama walijua, uzalendo wao upo wapi hawa watu wa kuliepusha Taifa hili na matatizo tunayoyaona hivi sasa? ...i really don't understand... may be kuungana kwao na mmoja wao kupelekwa ubalozini ni moja ya deal au fadhila???!
 
Back
Top Bottom