Kirchhoff
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,347
- 7,561
Pascal Mayalla he kuongelea kesi zilizopo mahakamani Ni kosa kisheria? Ili ukamatwe chap chap na kutiwa hatiani.
Yaan anachanganya mambo huyu mzee Pascal, Ni bora angesema yeye ni mwanaCCM na angependa Tundu Lissu aondolewe tu ..!!Ukichagua kuwa mgombea urais, uanaharakati unauweka pembeni, you speak, talk and behave like a president in waiting!, huwezi kusema hovyo, huwezi kutukana watu, huwezi kutoa tuhuma bila ushahidi, huwezi kuibagaza nchi yako kwenye media za mabeberu, halafu ukategemea utapitishwa tuu hivi hivi kugombea urais!.
Mbona kama umeshahukumu?
Huu uzi unachochea chuki kwenye jamii. Ni uzi uliojaa nia ovu.
Nitashangaa sana kama Lissu hataenguliwa na NEC kwa kigezo cha kuwa na kesi mahakamani. Najiuliza tu kwenye fomu zake za kugombea uraisi atajaza nini kwenye kipengere kinachohusu kuwahi kushitakiwa na kuwa na kesi mahakamani.
Ok tuvute subira, tutapata majibu muda si mrefu.Kesi zote za Mahakamani hazimzuii Kuwa Rais wa JMT. Ambacho watu wengi hwakijui ni Kwamba Lissu mwenye ni Mwanasheria Mashuhuri, Hawezi endelea kupoteza muda wake wakati anajua fika kesi zake zitamzuia.Hivyo hivyo CCM walidai Lissu angeweza kukosa kuchukua Fomu za kugombea Urais 8/8/ Kwa sababu ilikua ni siku kuu ya Wakulima kitaifa na Ofisi za Tume zingekua Zimefungwa.Lakini Lissu alichukua Fomu za Kugombea nafasi ya juu katika Nchi siku hiyo kwa sababu Lissu alikua na Taarifa kuhusu Ofisi ya Tume.Hivyo Lissu anayajua yote hayo ndio maana anajiamini kuliko wenye Mamlaka.
Kumuengua Tundu Lissu kugombea uraisi wa JMT ndio njia pekee ya ccm kushinda uchaguzi huu. Na watalisimamia hilo ili litimie.
Ila Mungu si wa ccm; ni wa wote.
Paskalli analifahamu hili akiwa kama mwanasheria na mwandishi sasa jiulize kipi kimemkumba hadi kuandika alicho andika. Ni juzi juzi tu kwenye uzi wake mmoja alituambia yeye hana chama na mara ghafla bin vuu huyo anapambana na wajumbe. Tumemuuliza kadi ya CCM kaipata lini hadi kesho hajajibu.Mahakama ndio chombo pekee cha kumtia mtu hatiania. Kabla ya hapo presumption ya innocence ndio kiongozi!! Kwa kuwa mpaka anachukua form na kabla ya kupitisha wagombea - mahakama ilikuwa haijamtia hatiani, hakuna jambo linaweza kufanywa kwa kufikirika tu.
Sasa Paskali unaenda mbele na kurudi nyuma? Kwamba wewe ndio ulimshauri agombee urais halafu unakuja tena kuleta hoja za kuenguliwa kwake. Hujioni kama ni mnafiki fulani hivi mahiri ambaye unataka kuwa Mr. Nice upendwe na kila mtu?
Declaration yako kuwa "kwa sasa ni kada wa ccm", inalenga nini?
Yaan anachanganya mambo huyu mzee Pascal, Ni bora angesema yeye ni mwanaCCM na angependa Tundu Lissu aondolewe tu ..!!
Et sijui kuingilia uhuru wa mahakama, tume iamue kumuondoa, sasa huko si ndo kuingilia mahakama ..!! Sijui kwanin wanajikomba kupita kiasi
JF sasa inamtambua Paskalli wa kweli ni nani. Alifanya uanachama wake wa CCM kuwa siri na sasa si siri tena. Bahati mbaya anajifanya kupuliza huku akiuma. Hana nia nzuri na Lissu FULLSTOP. Katika hili amejivuruga mwenyewe. Tungekuwa na kura ya kupoteza imani (Vote of no confidence) kura yangu ingemkataa.Yeye atoke na kusema anataka Tundu Lisu aenguliwe kwa vifungu kadhaa, maana anajua fika Magufuli hawezi kushindana na Lisu, hivyo amtetee atakayeweza kumpa ulaji. Paskali hana uzalendo wowote, bali ni mtu aliyeshuka daraja, huku umri ukiwa umetupa mkono.
Kwa sasa anafosi kingi. Ameamua kuomba nafasi kwa sauti ya juu maana hakuna anayemuona tangu alipoambiwa Mayala kwa Kisukuma maana yake ni njaa . Sonona ya mama yake Kabendera haitamuacha salama.JF sasa inamtambua Paskalli wa kweli ni nani. Alifanya uanachama wake wa CCM kuwa siri na sasa si siri tena. Bahati mbaya anajifanya kupuliza huku akiuma. Hana nia nzuri na Lissu FULLSTOP. Katika hili amejivuruga mwenyewe. Tungekuwa na kura ya kupoteza imani (Vote of no confidence) kura yangu ingemkataa.