Uchaguzi 2020 Wanasheria, Tusaidieni. Je, kuna uwezekano wa Tundu Lissu kuenguliwa na NEC kugombea Urais kwa kutumia kigezo cha Uadilifu wa Mke wa Kaisari?

Wakati unamshauri agombee hakuwa na hizo kesi unavosema. Kwani NEC na mahakama kwa mujibu wa sheria nani zaidi maana kuna kifungu kinasema NEC haiwezi kuhojiwa sasa kwanini iogope mahakama ambayo haiwezi kuihoji NEC inayo mamlaka yote ya kumpitisha kwakuwa yenyewe haiwajibiki kwa mahakama yoyote hapa Tanzania.

Hoja nyingine sheria imetamka wazi kabisa sababu zinazoweza kumfanya mgombea kutokuwa na Sifa na haijasema endapo atakuwa ameshitakiwa kwa kosa la jinai sasa hiyo sababu ambayo haipo kisheria itatumikaje kumuengua mgombea. Ni ukweli kabisa kuwa kama NEC itaamuwa kutofuata sheria ya uchaguzi na kumuengua Lisu ili kufurahisha mgombea wa CCM itakapotokea taharuki yoyote NEC ifahamu kuwa ndiyo itakuwa imesababisha The Hague itawahusu wahusika.
 
Tena ameshazoea. Niwashauri wapenda mabaduliko wote kuwa ikitokea Lisu kaenguliwa, tuanze na yeye kabla yakumfuata Kaijage.
Wewe unatumika siyo bure!
Waache kumuengua anayegawa rushwa hadharani waje wamuengue Lissu?
Hakuna ushindi wa mezani hapa, kila kura lazima ipiganiwe!

Mods this is a malicious thread iondolewe
Huyu anataka kuset tune kwa watawala wafanye udhalimu kama alivyoset tune Kabendera akapata matatizo
Naomba hii mada ya kichawi iondolewe hapa!
 
Umeongea kweli kabisa, coz hizo kesi zote ni za uchochezi na sio za mauaji au ujambazi

Me naona uchaguzi huu ulikuwa ni mzuri Sana kuisafisha ccm kwamba haibebwi

Walitakiwa kumake sure lissu anagombea na anashindwa kwenye kura

But kama wakifanya any how italeta sura mbaya Sana kwa jamii
 
Sidhani kama kuna wanasheria genuine wanaweza kufanya reasoning hii ya namna yako. Hii ni reasoning ya watu waliosomea sheria bila kujua sheria.

Na kama hilo unalolisema, wote wangekuwa na low reasoning kama hii uliyoileta, nchi nyingi za Kiafrika, wapinzani wangekuwa wanaenguliwa tu. Hawa viongozi wetu wahodhi madaraka wangekuwa wanawatuhumu tu watu, kisha unaondolewa kuwa mgombea.

This very low Pascal. You deserve better than this.

Tungekuwa na Tume huru, na tukawa na nchi inayozingatia sheria, Magufuli angeenguliwa kuwa mgombea. Nashani unafahamu kwa namna ambavyo mara kadhaa amekiuka kanuni.
 
Ccm wanachekesha sana, kama lisu wakimzuia kugombea niitaongeza hasira kwa wananchi natutaenda na "KAZI NA BATA"
Kama mpaka sasa hawajajifunza namatokea ya kuiua CUF basi mtakua nisikio lakufa
Wakimuengua na Membe utaenda kwa nani
 
CCM wakifanya hivo nitawadharau Sana. Approach waliyoichagua ya kupiga kimya ime work out. Lissu ni Kama anafukuza upepo kila anachojaribu kinabuma, Watanganyika ni Kama hawamuoni na unaweza kuona yeye na wafuasi wake wameanza kupaniki, hawapati response waliyotegemea Sasa wanaanza kutumia nguvu kubwa ikiwemo hata humu.
Isipokuwa tu Serikali inapaswa kuwa makini baada ya watu kuonekana kutokumtilia manani anaweza kufanya chochote kibaya ili mradi kutafuta millage na huruma. Jana alisema anatishiwa, wenye akili wanajua what he is going to do next!
Hata kabla ya kushambuliwa alisema kuwa anafuatiliwa, cha ajabu nini akisema leo anatishiwa.
 
Sidhani kama kuna wanasheria genuine wanaweza kufanya reasoning hii ya namna yako. Hii ni reasoning ya watu waliosomea sheria bila kujua sheria.

Na kama hilo unalolisema, wote wangekuwa na low reasoning kama hii uliyoileta, nchi nyingi za Kiafrika, wapinzani wangekuwa wanaenguliwa tu. Hawa viongozi wetu wahodhi madaraka wangekuwa wanawatuhumu tu watu, kisha unaondolewa kuwa mgombea.

This very low Pascal. You deserve better than this.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani ungemsaidia kisheria kama kichwa cha habari kinavyojionyesha kuliko kum'attack'. Si rahisi kumuelewa Paskal.
 
inaonekana TL anawapa tabu sana, sasa si mseme wazi tu kuwa hataruhusiwa kumchalenji jiwe na hivyo atangazwe mshindi kuliko kutuhadaa
 
1. ikiwa haya unayoyasema ni kweli, basi ni sahihi kuwabambikia kesi wote wanaotishia baadhi ya nafasi za uongozi ili kuwanullfy. Njia kama zile walizotumia watendaji wa kata kwenye uchaguzi wa mitaa naona hazijakata kiu yako.

2. nilidhani umewaelewa wajumbe. wajumbe wa CCM walikupiga chini kwa sababu unajipendekeza sana kwa tamaa ya kupewa madaraka.

sijawahi ona mtu ana mashaka na umahiri wako. Tatizo umahiri wako unautumia kwa kujipendekeza, kuchongea watu wanaoikosoa serikali, kusifia hata visivyofaa kusifia nk.
wakumbuke wajumbe.
 
Uzi unachosha. Unauliza swali mara unajibu mwenyew rubbish. Lissu is a suspect ni mpk mahakama itakapo mkuta na hatia. Na je ukimuengua na akashinda haki yake ya kuchagulia itakuwa wapi na mda ulishapita. Huo ni upuuzi mkubwa
 
Wazo la kipumbavu na hatari kwa usalama wa Taifa hili. Ulistahiki kushindwa Ubunge. Huna Hekima wala Busara.

Nani alikwambia mshitakiwa hana haki kugombea katika nafasi yoyote katika uchaguzi wowote ule? Unadhani walioweka kipengele cha mpaka utiwe hatiani na uhukumiwe hawakuwa na akili?
Mwandishi gani mwenye mawazo ya hovyo namna hii?

Nyie ndo watu ambao mpo tayari kwa lolote ilimradi matumbo yenu yamejaa.

Serikali, CCM wala NEC hawawezi kufuata ushauri wa kijinga kama huu.

Matatizo yatakapojitokeza, watu kama wewe sio mtakaowajibika, na pengine ndio sababu mpo tayari kutumia kalamu zenu kujaribu kuleta uchochezi kwenye Taifa hili.

Hakuna njia nyingine halali unayoweza kuitumia kupata unachokitafuta kuliko kutumia mawazo haya haramu kwa usalama wa Nchi?
Unaelewa matokeo yake?
 
Ulichokiandika ni fikirishi, Chadema kweli wanahitaji kuchukua hatua.

Lakini nakushauri katika uandishi wako kutokuweka pamoja alama ya mshangao (!), alama ya kiulizo (?) na alama ya kituo (.) au alama ya kituo kidogo (,) katika sentensi zako.
 
Back
Top Bottom