Wanasheria nisaidieni, Baba Mzazi anazidi kuuza mali

Unafikiri kachanganyikiwa!?

Hapana!

Anaona kuna uzembe FULANI kwa WATOTO kutotafuta Chao,anatoa akili kichwani Ili muanze kupambana!!
 
Habarini za asubuhi, naomba niende moja kwa moja kwenye mada baada ya baba angu kuuza nyumba yake ya kwanza week 3 zilizopita na kubakisha nyumba moja maeneo ya huku Sinza Mori ambayo ndio tunakaa sasa hivi nayo anataka kuuza, wakati bado watoto wake sisi bado tupo hai tena ususani mtoto wake mimi bado kijana mdogo hata umri wa miaka 50 sijafika ndio kwanza nina 42, na cha kushangaza huyu mzee baada ya kuuza nyumba ya kwanza bado hajanipa mgao wowote wa pesa mpaka niliamua kwenda kumshtaki ofisi ya kata na jana nimeenda kufungua kesi polisi na Jumatatu ya tarehe 24 tunaenda mahakamani kwa kesi kusikilizwa.

Cha kushangaza leo ameamka na kuanza kusema anauza nyumba hii pia, jamani wanasheria naombeni mnisaidie maana huyu baba anateketeza mali zote na mimi kama mtoto wake sijaambulia chochote mpaka muda huu, nahisi uenda mzee wangu akawa amechanganyikiwa, nataka nieleze mahakama hiyo jumatatu hoja yangu hii kama huyu mzee wangu huenda amechanganyikiwa ili niweze kupatiwa pesa zake zote nizihifadhi sehemu nzuri na salama.

Haiwezekani mimi mtoto wake nipo na nina elimu nzuri tu na kubwa sana ya degree ya marketing kutoka chuo kikubwa kabisa cha university of dar es salaam, na nina umri wa kijana ninayejitambua kabisa wa miaka 42 ashindwe kunipatia hizo pesa nizihifadhi au kama hataki anipe mgao wangu kabisa nikatafute maisha yangu.

Leo ananiambia kwa jeuri eti kama nimeamua kwenda mahakamani basi nitakuwa nakula na kulala mahakamani ila sio hapa kwake, nikamuambia hapa sio kwako hapa ni kwetu maana wewe ni baba yangu na mahakama inatambua umuhimu wa mtoto kwenye ishu ya urithi wa mali, anasema anaenda kutafuta dalali na muda huu ameondoka

Wanasheria naombeni mshikamane na mimi kwenye ili wakuu ili nipate haki yangu ya mali. Na alivyo na jeuri ananiambia ananipa siku mbili niwe nimeshatoa begi langu la nguo ndani niwe nimeondoka jamani mpaka namshangaa huyu mzee.

Nawasilisha
I'm nachekesha
 
Habarini za asubuhi, naomba niende moja kwa moja kwenye mada baada ya baba angu kuuza nyumba yake ya kwanza week 3 zilizopita na kubakisha nyumba moja maeneo ya huku Sinza Mori ambayo ndio tunakaa sasa hivi nayo anataka kuuza, wakati bado watoto wake sisi bado tupo hai tena ususani mtoto wake mimi bado kijana mdogo hata umri wa miaka 50 sijafika ndio kwanza nina 42, na cha kushangaza huyu mzee baada ya kuuza nyumba ya kwanza bado hajanipa mgao wowote wa pesa mpaka niliamua kwenda kumshtaki ofisi ya kata na jana nimeenda kufungua kesi polisi na Jumatatu ya tarehe 24 tunaenda mahakamani kwa kesi kusikilizwa.

Cha kushangaza leo ameamka na kuanza kusema anauza nyumba hii pia, jamani wanasheria naombeni mnisaidie maana huyu baba anateketeza mali zote na mimi kama mtoto wake sijaambulia chochote mpaka muda huu, nahisi uenda mzee wangu akawa amechanganyikiwa, nataka nieleze mahakama hiyo jumatatu hoja yangu hii kama huyu mzee wangu huenda amechanganyikiwa ili niweze kupatiwa pesa zake zote nizihifadhi sehemu nzuri na salama.

Haiwezekani mimi mtoto wake nipo na nina elimu nzuri tu na kubwa sana ya degree ya marketing kutoka chuo kikubwa kabisa cha university of dar es salaam, na nina umri wa kijana ninayejitambua kabisa wa miaka 42 ashindwe kunipatia hizo pesa nizihifadhi au kama hataki anipe mgao wangu kabisa nikatafute maisha yangu.

Leo ananiambia kwa jeuri eti kama nimeamua kwenda mahakamani basi nitakuwa nakula na kulala mahakamani ila sio hapa kwake, nikamuambia hapa sio kwako hapa ni kwetu maana wewe ni baba yangu na mahakama inatambua umuhimu wa mtoto kwenye ishu ya urithi wa mali, anasema anaenda kutafuta dalali na muda huu ameondoka

Wanasheria naombeni mshikamane na mimi kwenye ili wakuu ili nipate haki yangu ya mali. Na alivyo na jeuri ananiambia ananipa siku mbili niwe nimeshatoa begi langu la nguo ndani niwe nimeondoka jamani mpaka namshangaa huyu mzee.

Nawasilisha
Hakuna kosa lolote la lisheria mtu kuuza Mali zake.
 
Back
Top Bottom