Wanasheria msaada: Haki ya mgawo wa mali ilichumwa mume au mke kwenye ndoa

Mbilipili

Member
May 25, 2011
17
3
Wanasheria tunaomba ufumbuzi wa utata wa kisa hiki.
Mama mmoja (mfanyakazi ya kuajiriwai) alifiwa na mumewe (hakumwachia watoto) ila aliachiwa kiwanja ambacho kilikuwa kimejengwa uzio wa ukuta tu bila jengo lolote ndani yake. Baada ya miaka miwili mama huyo aliolewa na bwana mwingine mfanya biashara, kwa ndoa ya kikristo. Mama huyo akiwa na huyo bwana mpya akajenga nyumba ( kwa hela yake) kwenye kiwanja alichoachiwa na marehemu mumewe kisha wakahamia kwenye nyumba hiyo yeye na mumewe mpya. Wamebahatika kuzaa watoto watatu na huyo bwana. Baada ya kuishi na huyo bwana kwa miaka miwili na kuona mumewe anayumba kibiashara akamshauri aende shule ( bwana alikuwa std VII), bwana akakubaliana na mkewe akaanza shule (secondari ya Miaka 2), akafaulu kiasi chake, akaenda kozi akamaliza na akajiriwa. Wakati huo wote mama ndiye alikuwa anagharamia shule ya mumewe mpaka kupata kazi. Wakati huohuo yule mama akiwa na huyo mumewe amejenga nyumba na kununua gari kwa mikopo ambayo anakatwa kwenye mshahara wake.
Baba kaanza mapepe na vurugu kwenye ndoa, mama kaamua kuomba kutengana ambapo itapelekea kupeana talaka. Je, mumewe ni nini chake katika ndoa hiyo baada ya kutengana?
 
Wanasheria tunaomba ufumbuzi wa utata wa kisa hiki.
Mama mmoja (mfanyakazi ya kuajiriwai) alifiwa na mumewe (hakumwachia watoto) ila aliachiwa kiwanja ambacho kilikuwa kimejengwa uzio wa ukuta tu bila jengo lolote ndani yake. Baada ya miaka miwili mama huyo aliolewa na bwana mwingine mfanya biashara, kwa ndoa ya kikristo. Mama huyo akiwa na huyo bwana mpya akajenga nyumba ( kwa hela yake) kwenye kiwanja alichoachiwa na marehemu mumewe kisha wakahamia kwenye nyumba hiyo yeye na mumewe mpya. Wamebahatika kuzaa watoto watatu na huyo bwana. Baada ya kuishi na huyo bwana kwa miaka miwili na kuona mumewe anayumba kibiashara akamshauri aende shule ( bwana alikuwa std VII), bwana akakubaliana na mkewe akaanza shule (secondari ya Miaka 2), akafaulu kiasi chake, akaenda kozi akamaliza na akajiriwa. Wakati huo wote mama ndiye alikuwa anagharamia shule ya mumewe mpaka kupata kazi. Wakati huohuo yule mama akiwa na huyo mumewe amejenga nyumba na kununua gari kwa mikopo ambayo anakatwa kwenye mshahara wake.
Baba kaanza mapepe na vurugu kwenye ndoa, mama kaamua kuomba kutengana ambapo itapelekea kupeana talaka. Je, mumewe ni nini chake katika ndoa hiyo baada ya kutengana?

ndugu yangu naona upo biased sana kutaka kumpa haki mwanamama.

Lakini naomba nikuulize. Unaposema walifunga ndoa ya Kikristo, una maana yule mama alikuwa muislam ila alibadilisha dini na kuona kwa mujibu wa ndoa za kikristo au vipi?

lakini pia ni lazima walikuwa na makubaliano yao ndani ya ndoa? je wayajua hayo?

Je hicho kiwanja kilichonunuliwa kilinunuliwa kwa jina la nani? na kile cha kwanza kina jina la nani? na vile vile hilo gari lina jina la nani?

Tunaomba majibu yako
 
Ndugu yangu huyo mama hajaweka wazi kama kkuna makubaliano yoyote katika ndoa yao, na ni mkristo toka kuzaliwa. Ila kuhusu kiwanja mara ya kwanza kilikuwa na jina la mumewe marehemu(offer letter), alipopewa na ndugu wa marehemu akabadilisha jina na kuandaa hati(title deed) ya miaka 33 kwa jina lake (mwanamke). Na mali zote alizonunua kwenye ndoa ya pili ameandika jina lake mwenyewe mwanamke.
 
Back
Top Bottom