Wanasayansi wa kiafrika ndio wanaoikuza Amerika na Ulaya, kwanini wasiikuze Afrika yao?

Haiwezekani na ikiwezekana dunia haitatawalika na hapo utakua mwisho wa dunia..angalia kwenye mabomu ya nuclear wanavyovutana
 
Mataifa makubwa yanawapa thamani bora waende tu huko nje wakibaki tutawapa dharau ya juu na kuwaita wachawi na watoa kafara kila watakapofanya ugunduzi wao, na wakituzidi sana kiakili tutawahoji kwanini wao? tukishindwa kuwaloga tutawanyamazisha tu sehemu.

Wengine walishafanyiwa mambo mbaya.........ikiwa tu wapo masomoni n.k kwa hiyo nasisitiza ni akheri uende ulaya kama umeshajiona una kipaji sisi hatutweza kuenzi such bright people we cant afford to have them.

Tutataka watutumikie bure, wasitupelekeshe na wasijifanye wanajua saana...........

Chuki na Wivu havijawahi kuiacha Afrika salama.
 
Kuna vitu km 4 vinarudisha nyuma Africa
1.umasikini...hao woteukiangalia wamesoma nje ya Africa
2.lack of technology....Africa haina maabara kubwa km za wenzetu...kumbuka wenzetu hawawezi kipa kipaombele kitu ambachohakiwapi manufacturer
3.Leadership....hapa hatauwe nauwezo km walivyohawa jamaa....lkn we have no good leaders wakiweza endeleza project kubwa km za wenzetu.
4.money...hao wooote kulewanalipwa mkwanja mrefu mno...maisha mazuri very thing is well planned.
 
TATIZO VIONGOZI WENGI WA KIAFRIKA NDIYO SABABU UNAKUTA KIONGOZI HATA KAMA ANAFANYA UPUUZI UNATAKIWA UMSIFIE SASA VICHWA KAMA HIVI BORA WAISHI HUKO WATAHESHIMIWA, HEBU FIKIRIA RAIS ANASEMA HAKUNA KULIPWA MSHAHARA HUU KWANI WEWE NANI? SASA UNAKUTA MTU KAMA MO IBRAHIM ANGEPATA WAPI MABILION ALONAYO KAMA ASINGETUMIKIA UGHAIBUNI WANAKOTHAMINI UTAALAMU? LAZIMA TUKUBALI KUWA MUNGU ALITUUMBA TOFAUTI KUNA WATU WANAZIFAIDISHA NCHI FULANI KWA MABILIONI YA DOLLAR KUTOKANA NA AIDHA PRODUCTS AU UTAALAMU FLANI ZINAZOZALISHWA KWA MAARIFA YAKE.
SASA HUKU KWETU UTAKUTA MWANASIASA ANESHINDA KWA WAGANGA KUCHANJWA KILA KONA YA MWILI WAKE ANALAZIMISHA MSHAHARA WAKE USIZIDIWE NA RAIA MWINGINE SASA NANI MWENYE AKILI ATAKAA HUKU NGOJA TUENDELEE KUISOMA NAMBA.
 
Roho za korosho Mkuu kwamba wakiweka mazingira mazuri ya kuwavutia walio nje basi watafaidi sana.

Angalia suala la uraia pacha kwa magnolia Tanzania ambalo nchi jirani zote zimeruhusu kwa kuona faida yake lakini hapa kwetu sababu za kipuuzi sana kama vile wataiba hawa kisha kukimbilia huko walikochukua uraia lakini cha kushangaza majizi na mafisadi Serikalini hawana uraia pacha na wanaiba trillions hawakimbii nchi na mkono wa sheria hauwagusi hao majizi na mafisadi.

ufike wakati nchi zetu ziwe na sera nzuri zitakazowavutia wataalamu wetu kurudi nyumbani lakini sisi Africa tumekomaa na blah blah tu
 
Nani aliyekuambia wanasayansi wa kiafrika ndo walioikuza ulaya na marekani?

Hao waafrika wamekwenda huko washakuta ulaya na marekani zimeendelea
Waafrika wamepelekwa Marekeni nchi ikiwa changa mno bado haikuwa na maenedeleo ya kujivunia. Na kuhusu mtu mweusi kuvumbua vitu vinavyochangia ustaarabu wa leo ni vingi sana . Mafano wa hivyo vitu kuvitaja vichache: friji isingekuwepo kama isingekuwa engineer mweusi kugundua, namna ya kuhifadhi damu kwa ajili ya matumizi subitali ni doctor mweusi ndo aligundua, lift za kuendea juu maghorofani ni mweusi pia, open heart suggery ya kwanza ilifanywa na daktari mweusi, neumatic brakes za magari ni fundi mweusi ndo katuletea, automatic transmition gear kwenye magari ni black, train kutumia umeme ni cheusi mangala na mengine mengi tu mzee
 
2. Je tukisema waafrica wanatamaa ya pesa na si wazalendo wa nchi zao tunakosea? unafikiri hawa wanasayansi wangefanya kazi kwenye mabara yao africa tungekuwa bado maskini?
WAAFRICA weusi heee!!! kwanza unaanza kurogwa na, Mama mdogo, baba la wapi sijui! yana vinyongo vya wazi kabisa! shangazi yako wote hwa ni kutoka kijijini kwenu, wivu tu!! ili tu usivuke kimaisha!!........ Ok! labda mama ako kajitahidi weee!! ukavuka

kazini wafanya kazi wenzako, mke nae, Boss!! anakuonea Donge usivuke!! .....bado unajitahidi kusoma Jiwe anakuja na zake wewe ni hewa ! Mwanasayansi unaitwa majina mara hewa mara fake sasa kwa hali hii mtavuka kweli?

Ukienda kwa weupe kwanza ukiiba sayansi ukaileta nchini kwako wewe ni kidume utapendwa na kusaidiwa vizazi vyote! hukuo afica ya bongo unaitwa majina mabaya eti jizi, fake litoro! mwee!

Ulaya kwanza wao wazungu wanakugundua wao kuwa weye una kitu kichwani!! wanaanza kubembeleza unasoma kwa raha!! misaada unapewa yaani wewe maisha usumbuliwi sijui chakula, watoto hilo ni jukumu lao wewe ni kuwaza tu kazi zako!

yeyote unaempenda wewe ni jukumu lao!! sasa utarudi africa kwa binamu yako mchawi? au Rais kimeo km jiwe? Sarungi alijiroga karudi huyo hapo ana chakaa tu! na Elimu yake kuubwa ile! aliye mjali saana ni nyerere tu!!

mpaka wanae wamechanganyikiwa siku hizi wamekosa hata nauri ya kurudi kwa wajomba zao Ulaya! huyu angetunzwa mpaka na vitukuu sababu ana kitu cha kutupatia watanzania idara ya Tiba! lkn sababu ya kuhangaikia maisha yuko wapi unamsikia!

Waacheni hao wawe na tamaa!! km kuna mtu hapendi maisha mazuri ni chizi!! pia ile dhambi ya kuwauza ndg zenu utumwani bado inawatafuna!!!!=== mnalia lia nini waacheni wale maisha wakija huku watakufa na stress!!

hata ungekuwa wewe! utakubali kufa kizembe na utaalamu wako? hata mie naenda vizuri tu tena nawaambia kabisa msinijue! na Bongo yenu ya vibaka hiyo! Majiwe!

Mie nina uwezo wa kujengea watanzania wote nyumba nzuri za kisasa kuelekea juu! na nafasi kuubwa za kuishi huko, na sehemu hizo ni moja moja tu! yaani wabongo wote mnakaa mipakani, ili hapa kati mlime! na kufuga lkn wazo langu walilipinga!

sasa naenda lifanyia Ulaya na cotract nimepata! waacheni hao jamaa wale maisha sababu wazungu wanajua kula na vipofu! Nyerere, Mkapa, Gesase, mabingwa wengi tu kina Masana Hosp. wali kufa wakiwa bado wadogo tuna wahitaji. yoote hayo ajili ya stress!

Angalia sasa Kambona aliishi vizuri Ulaya karudi tu! Bongo kwenye uchawi !kufa! mifano ipo mingi ila sasa...... watu gani mnatembea na vinyongo tena hata kwa madaktari wanao wasaidia afya zenu? mweee!!
 
HII NI LIST YA WANASAYANSI KUTOKA AFRICA NA KAZI WANAZOZIFANYA KWENYE MATAIFA MAKUBWA

EGYPT
1. Euclid of Alexandria
huyu ni founder wa geometry ni mzaliwa wa egypt
amefanya kazi katika European Space Agency's (ESA) na ameunda euclid space craft
220px-Euklid-von-Alexandria_1.jpg


2. Sameera Moussa
huyu ni ni mwanafizikia aliyebobea kwenye maswala ya nyukilia na ni mzawa wa egypty ana doctorate ya atomic radiation na alifia huko California, united state
220px-SameeraMoussa.jpg


3.Ahmed Hassan Zewail
Huyu ni wa Egypt ni mwanzilishi wa femtochemistry anafanya kazi amerca
185px-Ahmed_Zewail_HD2009_Othmer_Gold_Medal_portrait.JPG


Eritrean
1. Haile Debas
huyu ni mfanya sugery, mwanafizikia na ni academic adminstrator katika chuo kikuu cha California ni mzawa wa africa

Carthage
1. Abbas Ibn Firnas
huyu ni mwanafizikia mchemia na engineer alifanya kazi huko spain ila ni mzawa wa carthage africa

Morocco
1. Rachid Yazami
huyi ni morocan alifanya research kuhusu lithium battery na graphite anode anafanya kazi katika French National Centre for Scientific Research (CNRS) ni wa kwaza kugundua intercalation ya lithium kwenye graphite katika electrochemical cell
220px-Rachid_Yazami_2011.JPG

Ethiopean

1. Sossina M. Haile

huyu ni profesa na mchemia pia ni mwanafizika na ni mhandisi anafanya kazi california instute of technology huyu aligundua solid acid fuel cells

2. Kitaw Ejigu
Ethiopian engineer and Chief of Spacecraft and Satellite Systems engineer at NASA.
KENYAN
1. Calestous Juma
Huyu ni professor pia ni mfanya kazi katika havard university ni mzawa wa kenya

MALI
1. Cheick Modibo Diarra
Huyu ni aerospace engineer amechangia kukamilika kwa mission nyingi za NASA mfano kupatikana kwa njia ya kwenda kwenye sayari ya mars , galileo space craft na kuchunguza sayari ya mars
NIGERIAN
1. John Uzo Ogbu
huyu ni professor alikuwa anachunguza maswala ya intelligence kuendana na rangi ya ngozi (race) inasemekana alikuwa na IQ kubwa ni mzawa wa nigeria lakini alikuwa anafundisha na kuishi California

2. Bisi Ezerioha

huyu ni professor, engeneer huyu ndie mgunduzi na mtengenezaji wa honda pia ameshiriki katika utengenezaji wa Hyundai Motor America mhshimiwa huyu pia anatengeneza injini za magari pia
220px-Bisi_before_a_race-_2013-09-24_11-08.jpg


SOUTH AFRICA

1. Aaron Klug
Huyu ni mchemia na biophycist alijishindia tuzo kwa kugundua crystallographic electron microscopy pia amegundua structure ya tobacco mosaic virus huyu ni director wa maabara ya molecular biology huko cambridge

2. Sydney Brenner
huyu amebobea kwenye genetic alipata tuzo noble prize kwenye phsiology or medicine anafanya kazi kwenye maabara ya molecular biology huko cambridge england pia ni mwanzilishi na mmiliki wa California instute of molecular bilology kwa kipindi cha maisha yake

3. Christiaan Barnard
huyu ni mpasuaji bingwa wa moyo pia alifanikiwa kuhamisha moyo kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa mara ya kwanza duniani hajareportiwa sehemu aliyokuwa anafanyakazi nnje ya africa lakini alionekana kuondoka sana africa na alikufa mwaka 2001

SUDANI
1. Mohammed Ibrahim
Huyu engineer na ni billionaire pia aliwahi kuishi british na kufanya kazi huko katika vitengo vya telecomunication aliajiriwa na british telecom huyu ni mwanzilishi wa mtandao wa celtel
220px-Mo_Ibrahim.jpg


2. Ali M. El-Agraa
huyu ni mwanauchumi bingwa amefanya kazi british, usa, na japan nchi ambazo sasa zinaonekana kukua kiuchumi mno

200px-Editing_Ali_M._El-Agraa.JPG


3. Mohamed Osman Baloola
huyu ni biomedical engineer pia ni mtafiti na mwendesha research kuhusu diabetes anafanya kazi uarabuni katika Ajman University of Science and Technology

220px-Mohamed_Osman_baloola.jpg

TANZANIA
1. Felix A. Chami
Felix A. Chami is an archaeologist from Tanzania. He is a professor at Dar es Salaam University. Dr. Chami discovered, on the island of Mafia and Juani, artefacts that revealed East Africa as being integral to the Indian Ocean trade huyu yupo africa na anafanya kazi africa alichogundua imebidi nikiweke kwenye lugha ya fumbo ili mjiulize kwanini kabaki africa
220px-Professor_Felix_Chami.jpg

UGANDA
1. Kwatsi Alibaruho
Huyu ni director wa kurusha vifaa vya anga anafanya kazi National Aeronautics and Space Administration (NASA) alishadirect human spaceflight mwaka 2005 pia anahusika kumanage na kucarry space shuttle flight
220px-Kwatsi_Alibaruho_-_flight_director.jpg

AFRICA TUNA LIST YA WANASAYANSI WENGI AMBA O NI WAZAWA WA AFRICA LAKINI SASA WANAYATUMIKIA MATAIFA MAKUBWA BADALA YA TAIFA LAO PIA WENGINE WANAONEKANA KUTAFUTA URAIA KWENYE MATAIFA HAYO

1. Je hii ni akili na wanasababu mdhubuti kufanya hivyo? je kuna watu wa mataifa makubwa kama amerca wanakuja kulitumikia tafa dogo africa?

2. Je tukisema waafrica wanatamaa ya pesa na si wazalendo wa nchi zao tunakosea? unafikiri hawa wanasayansi wangefanya kazi kwenye mabara yao africa tungekuwa bado maskini?

3. Je unafikiri hawa wanasayansi wangefanya kazi africa kungekuwa na mgogoro mkubwa na mataifa makubwa na huenda wangefanikiwa kuwaua?

4. je wanasayansi wa africa wanalazimishwa kufanya kazi kwenye mataifa makubwa na kutishiwa kuuliwa hivyo wanaogopa kufa


ILA NIMEGUNDUA WANASAYANSI WENGI WA KIAFRICA WANAOJULIKANA DUNIA NA NI WAZAWA WA SOUTH AFRICA BADO WANAFANYA KAZI SOUTH AFRICA JAPO SIJAWAWEKA KWENYE LIST HAPO

UMEGUNDUA NINI? africa tunajiona tuna wanasayansi wengi lakini wanaofahamika ulimwenguni pote ni wachache mfano kwa tanzania anafahamika mmoja kwani tunamaporofesa wangapi kwenye vyuo vyetu je wametendewa haki kutotajwa kwenye hii list?


nawasilisha


Nani atawalipa??
Huko wapo kwasababu nchi walizopo zinajali maslahi yao pia yaan ni WIN WIN situation


Huku kwetu WIN LOSE situation
Nchi ipate ila kukujali ww mwananchi ndo sahau
 
Africa hatuna tabia ya kulinda, kuheshimu na kutoa nafasi Kwa wanasayansi ambao kazi zao ndo mwanzo wa ajira na utengenezaji wa mabilioni nakumbuka prof Wambura wa SUA alipogundua chanjo ya kuku TATUMOJA alipewa nishani yake huko ughaibuni Cha kushangaza aliporudi hakukua na yeyote pale airport zaidi ya familia yake lakini makoñda, Kibajaji, mwin'jaku, mwigulu ndiyo wanaoshangiliwa sasa unadhani Nini kitatokea?
 
Yupo mtaalam mmoja wa kabila langu ni aviation engineer na ni designer wa helicopter rotter blade anafanya kazi CANADA mara chache akija kusalimia akitua dsm hukodiwa chopper na kampuni yake na Kuna wazungu huwa anakuja nao hawamwachii kizembe Kisha wanaruka nae north America ni zamani tu aliwahi kuja peke yake sasa hivi hakuna lazima aje na watasha ana miradi kama yote lakini akibaki hapa bongo Ili aonekane wa maana lazima awe chawa Kwanza tena chawa wa Ole sabaya
 
Mataifa makubwa yanawapa thamani bora waende tu huko nje wakibaki tutawapa dharau ya juu na kuwaita wachawi na watoa kafara kila watakapofanya ugunduzi wao,
Kuna mtu kafanyiwa kila aina ya ushenz na ndugu, kapelekwa jela mwaka na nusu kwa kesi ya kusingizia baada ya kumaliza 6, kesi ikafutwa baada ya kukosa ushahidi, baada ya kutoka kafanya juu chini kaenda chuo 5yrs baada ya kumaliza 6, kamaliza chuo kapata kazi, ndugu walipoona anataka kutoboa na anamraidia sana mama yake ambaye ndo alikuwa faraja yake, wakaenda mpaka kazini kwake kumuaribia kuwa anaiba sana, kasimamishwa kazi uchunguzi kufanyika hana kosa karudishwa ila baada ya mkataba kuirha hakupewa tena mwingine kwa jinsi ndugu walivomsiliba kule kazni, faraja yake ikatangulia mbele ya haki, ndugu wakavuruga mpaka ndoa yake, kwa sasa wanataka kumnyang'anya urithi wake wamrithishe mdogo wao wa kike, hii ngoz nyeus tabu tupu.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom