DocJayGroup
JF-Expert Member
- Jan 17, 2020
- 1,654
- 3,319
Hata mimi pia mkuu. Nilipitia hio experience. Bahati nzuri baada ya kupoteza kila kitu nilikuja pata nafasi nyingine na kupata hela nzuri zaidi sasa kwa kutumia mafunzo niliyojifunza hapo mwanzo sikurudia kosa tena nikaweka mambo sawa. Tatizo ni kwamba kwa bahati mbaya mtu mwingine akishafilisika hapati nafasi tena kama ya mwanzo. Kwa hio ameshajifunza somo lakini opportunity unakuta hairudi tena.Sawa nimekuelewa kwa asilimia zote coz kuna kipindi nilibahatisha visenti basi ghafla nilipata wapambe hata walikotoka hapakujulikana.
Utakuta mmekaa bar mnaongea akipita demu mkali wanakutongozoea ghafla analetwa mezani.
Mara akipita muuza viatu au suti anaitwa halafu wanaanza kukuchagulia huku wanaisifia,hii suti kali sana mkuu ni kwa ajili ya watu wa level zako,anavaaga JK hii.
Nilivyofirisika waliyeyuka wote,ila nimeanza kuzichanga tena sasa hivi sitaki mazoea na mtu na bahati nzuri umri wangu bado haujaenda sana niko below 35.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa 35 uko sawa kabisa. Afadhali umeshapitia hio, na utapata mahela mengi sana na sasa utajua cha kufanya bila kukosea.