Wanaotaka Muungano Uvunjike watoke kwanza Bungeni na BLW

Mwanakiji mbunge ana immunity mjengoni.Hawezi kushtakiwa kwa lolote atalosema mle ndani.
However me naona hawa jamaa waanze mbele,maana hata wanyamwezi wenzetu huko wanajiona superior.Wachukue time!!
 
Mimi siifikiriii kama kuna mtu anayetaka kuvunja muungano bali katika kuangalia mustakabali wa uchumi wa pande zote ikiwa pamoja na kero mbalimbali ambazo zimekuwa zinaongezeka siku hadi siku kwa kukosa majibu mujarabu kunapelekea ni bora kuvunja muungano ili kupunguza au kuondoa kabisa hizo kero.

nafikiri hilo halina mjadala. Muungano sio msahafu kuwa hauruhusiwi kujadiliwa na watu wapo huru kuujadili kwa kina sana ili kuondoa kabisa hayo manunguniko.


Wawakilishi au wabunge wana nafasi kubwa sana ya kuujadili kwa kina na ukiwezekana kuuvunja kama hawataridhishwa na maendeleo ya muungano huo.
 
Kwa mfano ikishauriwa ipigwe kura kupitia Bunge au Baraza la Wawakilishi kuhusu kuvunja Muungano na hao wabunge au wajumbe wameondoka nani atapiga kura hizo?Imeamuliwa Muungano ujadiliwe Bungeni au BLW nani ataujadili na wanaotaka kuujadili wamendoka?
 
Nadhani Kila mmoja wetu anafahamu swala la muungano limekuwa likiisumbua serikali zote Nne zilizowai kuwa madarakani na kama mnakumbuka G7!n.k.Lakini huu muungano siyo maisha ya watanzania Bara wala siyo maisha ya Wazanzibar,bali Muungano nikitu tu kipo ambacho kiliwekwa kwa ajili ya kuunganisha tamaduni zetu baina ya Bara na Visiwani,Lakini ukiangalia kwa umbali utaona tangu Muungano huu uwepo kumekuwepo na kasoro nyingi japo zimekuwa zikirekebishwa!Nazote zimekuwa zinarekebishwa kwa ajili ya kusaidia upande mmoja wa Visiwani!Kwa maana hiyo siku zote Hawajaridhika na marekebisho hayo! nakumbuka sisi tulikuwa tukienda Zanzibar na Passpoort,lakini wao wanakuja huku bila hata karatasi ya mjumbe!.Matokeo yake wamekuwa wakilalama na kutukebei juu ya Muungano wetu ulio anzishwa na Na wa asisi wa nchi hizi mbili Tanganyika na Zanzibar leo Tanzania!Kwa kasumba ya Wazanzibar hata mngewafanyiwa nini hawawezi kuridhika na kwakuwa wao ni wabinafsi ndiyo maana leo wewe toka hapa Tanzania bara nenda Tanzania visiwani huwezi kubata hata nyumba ya kupanga achilia kiwanja!.Mimi naona wauvunje huu Muungano hauitajiki kwa wa Zanzibar lakini wanasahau kama wao ndiyo wanaofaidika na Muungano huu! Kuanzia Kodi mpaka vyeo!Hivyo tusiendelee kukumbatia Nyuki wakati tuanaumia!!. Nasema Serikali ijue inaweza ikautaliki Muungano Tuachane na mabo haya alianzisha fulani hiyo nikudumisha Fkira za mwenyekiti ni mambo yaliyopitwa na wakati!!!
 
Kuna Wawakilishi na Wabunge ambao wamekuwa wakitoa lugha ya kuonesha kuchoshwa na Muungano na bila ya shaka wanazo sababu ambazo wanaamini zinawapa haki ya kutoa hisia hizo. Lakini wapo wengine kati ya hao ambao wanatoa matamshi yenye kuashiria kupigania kuvunjwa kwa Muungano. Wapo wawakilishi wa vyama vyote ambao wamekuwa na kauli hizo za kutishia kuvunja Muungano hasa katika Bunge lililopita na hili la sasa. Ndugu zangu, hawa wawakilishi hawawezi kutoa kauli za kutaka kuvunja Muungano na wakabakia wawakilishi halali wa wananchi kwani kwa kutoa kauli za kuvunja Muungano wanavunja Katiba iliyowaweka hapo.

1. Wawakilishi wote hawa walisimamishwa kugombea nafasi zao au kupata nafasi zao kwa kudhaminiwa na vyama vya siasa ambavyo viliandikishwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya Vyama Vingi. Katiba na Sheria zinakataza kabisa kuandikishwa chama chochote ambacho kinapigania kuvunja Muungano. Hivyo, wote walisimamishwa na vyama visivyopigania kuvunjwa kwa Muungano.

2. Kutokana na hilo la kwanza, hakuna Mbunge au Mwakilishi ambaye wakati anagombea aliwaahidi wananchi kuwa ataenda kupigania kuvunja Muungano kwa sababu au kisingizio chochote kile. Wasingeweza kufanya hivyo wakati wa kampeni kwa sababu Katiba inawakataza na Sheria ya Uchaguzi ingewabana na kuwaengua mara moja. Kama hakuna chama kilichoandikishwa kwa ajili ya kuvunja Muungano hawa wawakilishi wanapata wapi mandate ya kutoa hoja za kuvunja Muungano?

3. Waliposhinda uchaguzi au kupewa ushindi wa chee waliingia Bungeni/BLW na kabla ya kuanza majukumu yao walishika misahafu na kuapa. Waliapa kwanza kabisa "kulinda, kutetea na kuihifadhi Katiba Ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania". Ninataka kuamini kuwa walimaanisha viapo vyao. Kama walimaanisha walijifunga kuulinda Muungano siyo kuuvunja. Hivyo, kauli zozote za kutishia kuvunja Muungano au hata kuashiria kuwa "muungano uvunjike" ni kinyume na kiapo chao na hivyo ni kosa tosha kabisa la kumfanya Msajili aidha kukifuta chama cha siasa au kumtangaza huyo Mbunge/Mwakilishi kuwa amepoteza sifa za kuwa mwakilishi. Huwezi kuapa kulinda Katiba halafu ukasimama kutangaza kutaka kuivunja!

4. Kama 1,2 na 3 ni kweli basi Wabunge na Wawakilishi walioko kwenye nafasi zao sasa hawana haki, uwezo, madaraka wala mamlaka ya kuzungumzia kuvunja Muungano. Yote wanayoweza kufanya ni kuutetea na kuuenzi na kuulinda.

5. Kwa vile Katiba imeweka toka mwanzo kabisa (Ibara ya 1,2) kuwa Tanzania ni nchi moja na eneo lake ni eneo lolote la Tanzania Bara na Tanzania Visiwani na kuwa katika nchi hii moja kuna vyombo viwili vya utendaji yaani Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar kauli zozote za kubadilisha serikali hizi mbili aidha kwenda serikali moja au serikali tatu nayo ni kinyume na Katiba! Wabunge hawawezi na hawapaswi kuzungumzia kubadilisha Muungano kwani Katiba Inawakataza isipokuwa kama wametekeleza utaratibu wa Katiba wa kubadili Muungano. Wameapa kulinda Nchi Moja, Serikali Mbili! Ndio maana wengine tulipuuzia na kubeza kauli ya Rais Kikwete kuwa Zanzibar ni "nchi ndani ya nchi" kwani haina mantiki na ni kinyume cha Katiba!

6. Kama 1, 2, 3, 4 na 5 ni kweli basi wabunge na wawakilishi wetu wanaachiwa uchaguzi mmoja tu nao ni kutatua kero za Muungano, kuondoa matatizo yaliyopo na kuboresha ili kuufanya Muungano uzidi kuimarika. Hawapaswi kuudhoofisha wala kutoa kauli za kuwachochea watu kuchukua msimamo wa kuuvunja. Siyo wabunge tu wale wote walioapa kulinda Katiba na hivyo kulinda Muungano wanalazimishwa na Katiba hiyo kuulinda Muungano kwa nguvu zao zote.

Hii ina maana gani?
Kwamba, kama kuna Mbunge au Mwakilishi ambaye anaona kuwa Muungano haufai na hataki uwepo anaachiwa uamuzi wa kutakiwa kutoka Bungeni (ili asibanwe na kiapo) na kwenda kuanzisha harakati za kuvunja Muungano. Na kama kundi hili linaweza kupata wafuasi basi ni jukumu lao kutumia nguvu zao zote (na hapa neno ZOTE nalimaanisha) kupigania kuvunja Muungano na kwa kufanya hivyo wajue wameamkua kupambana na vyombo vilivyopo vyenye kulinda Muungano. Kama hoja yao inaweza kuwa na nguvu sana na kupata wafuasi wanaweza kujikuta hatimaye wanalazimisha Muungano kuvunjika aidha kwa njia ya amani au kwa vurugu. Kwa vile Muungano wetu haukuwa wa ku-annex Zanzibar ni wazi unaweza kuvunjwa kwa njia ya amani kabisa. Muungano wetu siyo kama ilivyokuwa Ethiopia na Eritrea au Sudan na Sudan Kusini au Russia na Georgia au Ukraine au zilizokuwa Jamhuri za Yugoslavia. Tanganyika haikuivamia Zanzibar na kuichukua kwa nguvu. Ulikuwa ni Muungano wa Hiari ambayo kusema ukweli ni vigumu sana kuuvunja licha ya majaribio ya baadhi ya watu kujaribu kuwafanya Watanganyika wajisikie kama waliivamia Zanzibar. Ni vigumu kuvunja Muungano wa hiari.

Hivyo, wale walioapa kulinda Katiba na Muungano na sasa wanataka kuvunja Muungano huo hawalindwi na kinga za Bunge wala Uhuru wa Mawazo kwani mwanafamilia hawezi kuja na dumu la mafuta ya petroli na kiberiti mkononi na kuanza kudai kuwa pale Nyumbani watu hawampendi na hawamjali na hivyo ameamua kuichoma nyumba moto na watu wasema ati "ni uhuru wa maoni". Pale Bungeni Mbunge hawezi kusimama na kupiga kelele "moto moto" halafu watu wakikurupuka kukimbia asema "analindwa na haki na kinga za Bunge kusema lolote Bungeni".

Waondoke kwanza Bungeni na BLW ili waanzishe hoja za kuvunja Muungano; hawawezii kufanya hivyo wakiwa bado wamefungwa na viapo vya kuulinda Muungano huo.


Mkuu Katiba ni maandiko yalioandikwa na watu na inaweza kubadilika. Articles of Union zilikwenda wapi kwani?

Hao Wawakilishi wetu wanasema kile tunachowatuma.

Wataondoka Bungeni, pale tu mkiondosha majeshi yenu ya uvamizi huko Zanzibar.

Zanzibar for Zanzibaris


“[President Nyerere] managed half the work of a python… He swallowed Zanzibar all right but he did not crush its fighting force first. The live animal is a long time digesting, and its kicks are being felt hurtfully, and possibly even fatally, deep inside Tanganyika’s body politic.”

- ‘The Perils of Nyerere’ in The Economist of June 1964

 
Katika sheria kila muungano unavunjika, hakuna muungano usiovunjika, labda ukose mwanasheria mbishi uzuri.

Hata hizo atoms zinazounganishwa kwa nuclear force naturally zinavunjika katika radioactivity, itakuwa hizi artificial man made entities ?

Cha kufanya hapa ni kuitisha country wide referrendum, ili muungano uendelee inabidi upate baraka za at least a simple majority kote bara na visiwani. Hili litakata mzizi wa fitina, watakaoutetea muungano watasema wanautetea kutokana na mandate ya watu.

Muungano uliopo umekuwa shoved down peopl'e throat, hakuna Mtanzania aliyeupigia kura au ku u endorse directly.

Hata kama mtu alikubali muungano, hili halina maana kwamba hana haki ya kubadili mawazo yake.
 
Katika sheria kila muungano unavunjika, hakuna muungano usiovunjika, labda ukose mwanasheria mbishi uzuri.

Hata hizo atoms zinazounganishwa kwa nuclear force naturally zinavunjika katika radioactivity, itakuwa hizi artificial man made entities ?

Cha kufanya hapa ni kuitisha country wide referrendum, ili muungano uendelee inabidi upate baraka za at least a simple majority kote bara na visiwani. Hili litakata mzizi wa fitina, watakaoutetea muungano watasema wanautetea kutokana na mandate ya watu.

Muungano uliopo umekuwa shoved down peopl'e throat, hakuna Mtanzania aliyeupigia kura au ku u endorse directly.

Hata kama mtu alikubali muungano, hili halina maana kwamba hana haki ya kubadili mawazo yake.

absolutely.. hii hapa si hoja; hoja siyo kama Muungano uvunjie au usivunjike au hata uhalali wa Muungano. Hoja ni kuwa waliapa kuulinda - tena hata leo Mbunge mwingine kazungumza hivyo hivyo Bungeni kusema "wakati umefika" Muungano uvunjwe. Well.. aidha walimaanisha walichoapa au hawakumaanisha. Rais wa Marekani kwa mfano au seneta wa marekani hawezi kuzungumzia "lets break up the union" na akaachwa hivi hivi.
 
absolutely.. hii hapa si hoja; hoja siyo kama Muungano uvunjie au usivunjike au hata uhalali wa Muungano. Hoja ni kuwa waliapa kuulinda - tena hata leo Mbunge mwingine kazungumza hivyo hivyo Bungeni kusema "wakati umefika" Muungano uvunjwe. Well.. aidha walimaanisha walichoapa au hawakumaanisha. Rais wa Marekani kwa mfano au seneta wa marekani hawezi kuzungumzia "lets break up the union" na akaachwa hivi hivi.

Kiapo nacho ni muungano, kinamuunga mtu na principle fulani.

Kama muungano unavyoweza kuvunjwa kwa sababu ni man made, kiapo nacho kinaweza kuwa nullified based on new info.

Swala ni kuuliza basis yao ku nullify kiapo. Mtu anaweza kusema ana nullify kiapo chake kwa sababu misingi ya muungano imekiukwa, nchi imeoza, etc.

Ni kama mtu aliyetoa confession kituo cha polisi, akatia saini, anaweza kwenda mahakamani akadai kwamba alitia saini under pressure.

Kwa hiyo kiapo si deal.
 
Nadhani Kila mmoja wetu anafahamu swala la muungano limekuwa likiisumbua serikali zote Nne zilizowai kuwa madarakani na kama mnakumbuka G7!n.k.Lakini huu muungano siyo maisha ya watanzania Bara wala siyo maisha ya Wazanzibar,bali Muungano nikitu tu kipo ambacho kiliwekwa kwa ajili ya kuunganisha tamaduni zetu baina ya Bara na Visiwani,Lakini ukiangalia kwa umbali utaona tangu Muungano huu uwepo kumekuwepo na kasoro nyingi japo zimekuwa zikirekebishwa!Nazote zimekuwa zinarekebishwa kwa ajili ya kusaidia upande mmoja wa Visiwani!Kwa maana hiyo siku zote Hawajaridhika na marekebisho hayo! nakumbuka sisi tulikuwa tukienda Zanzibar na Passpoort,lakini wao wanakuja huku bila hata karatasi ya mjumbe!.Matokeo yake wamekuwa wakilalama na kutukebei juu ya Muungano wetu ulio anzishwa na Na wa asisi wa nchi hizi mbili Tanganyika na Zanzibar leo Tanzania!Kwa kasumba ya Wazanzibar hata mngewafanyiwa nini hawawezi kuridhika na kwakuwa wao ni wabinafsi ndiyo maana leo wewe toka hapa Tanzania bara nenda Tanzania visiwani huwezi kubata hata nyumba ya kupanga achilia kiwanja!.Mimi naona wauvunje huu Muungano hauitajiki kwa wa Zanzibar lakini wanasahau kama wao ndiyo wanaofaidika na Muungano huu! Kuanzia Kodi mpaka vyeo!Hivyo tusiendelee kukumbatia Nyuki wakati tuanaumia!!. Nasema Serikali ijue inaweza ikautaliki Muungano Tuachane na mabo haya alianzisha fulani hiyo nikudumisha Fkira za mwenyekiti ni mambo yaliyopitwa na wakati!!!


Mkuu kwanza nikwambie kuwa mwandiko wako mbovu na mimi nimesoma kwa tabu kidogo.

Ni kweli hata hivyo kwamba huu "muungano" ulianza vibaya kwa sababu haukutokana kwa ridhaa ya wananchi. Sababu za kuja "muungano" huu nadhani mpaka sasa utakuwa unazielewa.

Ni kweli pia ujanja mwingi na ubabe umekua ukitumika kuusimamisha.

Ni kweli pia kuwa zimekuwa zikifanyika kupunguza makali yake kwa zile zinazoitwa kero. Bahati mbaya hakuna unafuu unaopatikana kwa sababu hakuna kitu kero za "muungano", bali "muungano" wenyewe ndio kero.

Umezungumzia paspoti kuja Zanzibar. Hilo lilifanywa ili kudhibiti uingiaji watu hovyo katika Visiwa vidogo kama vyetu. Kuna wengi walivuka kuja huku kukimbia kodi zenu za ichwa. Tanganyika pia imezungukwa na nchi nyingi ambazo baadhi ya wakazi wake wanazungumza Kiswahili vizuri tu na huwezi kuwajua kuwa hawatoki Tanganyika. Tokea paspoti kuondolewa, Zanzibar imeathirika sana, hasa kimila na utamaduni.

Kuhusu umiliki wa nyumba au kupanga Mkuu, hilo sio kweli kwani Zanzibar wako watu wengi kutoka bara na hawa hawalali nje.

Kwamba huu "muungano" hauna faida, sio kwenu tu bali hata sisi ni hivyo hivyo tu. Wanaofaidi ni wakubwa wachache wa pande zote mbili.

Wazanzibari walio wengi hawautaki "muungano" wa aina hii na hasa kutokana na mfumo uliopo. Wengi tunataka uvunjike jana na sio kesho

Tatizo ni Tanganyika ilioweka majeshi yake ya uvamizi Zanzibar. Kunga'ang'ania kwenu huko ndio kunakotufanya tuamini kuwa ni nyinyi mnaofaidi. Hilo sisi hatulikubali mpaka kieleweke.

"[President Nyerere] managed half the work of a python… He swallowed Zanzibar all right but he did not crush its fighting force first. The live animal is a long time digesting, and its kicks are being felt hurtfully, and possibly even fatally, deep inside Tanganyika's body politic."

- ‘The Perils of Nyerere' in The Economist of June 1964

Zanzibar for Zanzibaris

 
absolutely.. hii hapa si hoja; hoja siyo kama Muungano uvunjie au usivunjike au hata uhalali wa Muungano. Hoja ni kuwa waliapa kuulinda - tena hata leo Mbunge mwingine kazungumza hivyo hivyo Bungeni kusema "wakati umefika" Muungano uvunjwe. Well.. aidha walimaanisha walichoapa au hawakumaanisha. Rais wa Marekani kwa mfano au seneta wa marekani hawezi kuzungumzia "lets break up the union" na akaachwa hivi hivi.

Huyo wetu ndio kasema hivyo na hakuna mnachoweza kufanya na "muungano" huu hauna muda kwenda na maji.

Keep watching these pages Mkuu Mwanakijiji.
 
Kiapo nacho ni muungano, kinamuunga mtu na principle fulani.

Kama muungano unavyoweza kuvunjwa kwa sababu ni man made, kiapo nacho kinaweza kuwa nullified based on new info.

Swala ni kuuliza basis yao ku nullify kiapo. Mtu anaweza kusema ana nullify kiapo chake kwa sababu misingi ya muungano imekiukwa, nchi imeoza, etc.

Ni kama mtu aliyetoa confession kituo cha polisi, akatia saini, anaweza kwenda mahakamani akadai kwamba alitia saini under pressure.

Kwa hiyo kiapo si deal.

Kama kiapo si deal watu wasingekuwa wanashtakiwa kwa perjury or "lying under oath". Na kiapo cha ofisi ni tofauti na kiapo cha ushuhuda kwani kiapo cha ushuhuda kinahusiana na kusema kile ulichoshuhudia kwa ukweli wote. Kiapo cha ofisi kinahusiana na kukubali wajibu, madaraka, haki na kazi zinazotokana na kiapo hicho. Hivyo, kama Rais anakula kiapo cha ofisi ya Urais au Mbunge cha Ubunge maana yake hawa wote wanakubali majukumu yanayotokana na kiapo hicho.

Kiapo hicho cha kazi kinaitwa "Kiapo cha Uaminifu" na mtu kama Rais au Jaji anakula pia kiapo cha ofisi yake. Ndio maana basi kiapo hicho kinasema (as far as I can remember):

''Mimi (Mbunge atataja jina lake), naapa kwamba nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wangu wote, na kwamba nitaihifadhi, nitailinda na nitaitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyowekwa kwa mujibu wa sheria. Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.''

(Msisitizo wa kwangu)

Haya maneno yanaweza yasiwe na uzito au yakawa na maana na watu wakachukulia kirahisi rahisi tu; lakini ukiyaangalia yanafuta kabisa uwezekano wa mbunge huyo kutaka Muungano uvunje.
 
Wakuu hebu tuzingatiye, hivi Katiba yetu imetowa mwanya wowote wa kuukata Muungano, hivi ulikuwa muungano wakulazimishwa au wakhiyari, jee ilikuwa ni ndowa isio na TALAKA? pengine ndoa ya aina hiyo ni ngeni kwa wazenji au solution ni kufanya kama walivyotanguliya kwanza wasudan ya kusini?
 
Kama kiapo si deal watu wasingekuwa wanashtakiwa kwa perjury or "lying under oath". Na kiapo cha ofisi ni tofauti na kiapo cha ushuhuda kwani kiapo cha ushuhuda kinahusiana na kusema kile ulichoshuhudia kwa ukweli wote. Kiapo cha ofisi kinahusiana na kukubali wajibu, madaraka, haki na kazi zinazotokana na kiapo hicho. Hivyo, kama Rais anakula kiapo cha ofisi ya Urais au Mbunge cha Ubunge maana yake hawa wote wanakubali majukumu yanayotokana na kiapo hicho.

Kiapo hicho cha kazi kinaitwa "Kiapo cha Uaminifu" na mtu kama Rais au Jaji anakula pia kiapo cha ofisi yake. Ndio maana basi kiapo hicho kinasema (as far as I can remember):

''Mimi (Mbunge atataja jina lake), naapa kwamba nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wangu wote, na kwamba nitaihifadhi, nitailinda na nitaitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyowekwa kwa mujibu wa sheria. Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.''

(Msisitizo wa kwangu)

Haya maneno yanaweza yasiwe na uzito au yakawa na maana na watu wakachukulia kirahisi rahisi tu; lakini ukiyaangalia yanafuta kabisa uwezekano wa mbunge huyo kutaka Muungano uvunje.

Kiapo kimetolewa kwa misingi fulani, ukiweza kutoa argument kwamba misingi ya kiapo imevunjwa, kwa mfano nchi haifuati katiba, unaweza kuvunja kiapo.

Ndiyo maana nikasema kitu muhimu ni basis yao ya kutaka kuvunja kiapo/ muungano.

Hata ndoa ina legal na religious grounds for divorce.

Wewe unaongelea utakatifu wa kiapo? Kuna watu wana debate legitimacy ya idea nzima ya nchi -nchi yeyote ile-, achilia mbali muungano wa Tanzania na viapo vyake.

But that's a totally separate ballgame.
 
Kiapo kimetolewa kwa misingi fulani, ukiweza kutoa argument kwamba misingi ya kiapo imevunjwa, kwa mfano nchi haifuati katiba, unaweza kuvunja kiapo.

Ndiyo maana nikasema kitu muhimu ni basis yao ya kutaka kuvunja kiapo/ muungano.

Hata ndoa ina legal na religious grounds for divorce.

Wewe unaongelea utakatifu wa kiapo? Kuna watu wana debate legitimacy ya idea nzima ya nchi -nchi yeyote ile-, achilia mbali muungano wa Tanzania na viapo vyake.

But that's a totally separate ballgame.

Hoja ya legitimacy haipo; ndio maana hata sijaribu kuiangalia kwa sababu argument inayotolewa kuhoji legitimacy yake haina mshiko. Hata hivyo kama hao wabunge wangekuwa wanahoji "legitimacy" ya Muungano wasingeapa kuwa waaminifu kwa muungano huo. Kwa kukubali kula kiapo cha kuwa waaminifu kwa "jamhuri ya Muungano wa Tanzania" wameondoa uwezo wote wa kuhoji legitimacy yake.

Lakini hata kama kungekuwa na hoja ya legitimacy, bado kunaleta shida. Kwanini waliapa kuwa waaminifu kwa kitu ambacho wanamashaka na uhalali wake?

In both counts, hawa walioapa hawawezi kuwa wao ndio wanasimama na kusema tuvunje. Walioapa kulinda na kuhifadhi na kuwa waaminifu wanatarajiwa kusimamia kile walichoapa kukifanya. Kama wanaona kuwa hawawezi kuendelea (katika dhamira safi) na bona fide basi wajitoe kwanza Bungeni au BlW ili waweze kusema kweli wana matatizo na Muungano. As long as they are sworn to be faithful to the United Republic of Tanzania, the people have to hold them accountable to that oath. Shouldn't they?
 
Mwanakijiji nadhani kusema wabunge wanaotaka muudo tofauti ya muungano watoke ni sawa na majibu ya ndugagai alimwambia Halima mdee kuwa zile posho za wabunge zilivyopitishwa hakuwepo na ka kama hawazitaki basi warudishe zote.

Mbunge sio Rais.. Angekuwa ni Rais au Waziri naweza kukuelewa lakini kwa mbunge hana ulazima wa kuachia ubunge ili atetee muundo wa serikali ulio swa kwa mtazamo wake au wananchi anaowakilisha.

Sababu tunategemea wabunge waheshimu kanuni za bunge zikiwemo na kanuni za posho zilizopitshwa kihalali na bunge. Lakini kwa mbunge kuhoji na kukataa uhalai wa oposho haina maana anavunja kanuni za bunge.

Tunategemea wabunge wawe na uwezo wa kuichallenge hata katiba kama ni kwa maslahi ya wananchi.
 
Hoja ya legitimacy haipo; ndio maana hata sijaribu kuiangalia kwa sababu argument inayotolewa kuhoji legitimacy yake haina mshiko. Hata hivyo kama hao wabunge wangekuwa wanahoji "legitimacy" ya Muungano wasingeapa kuwa waaminifu kwa muungano huo. Kwa kukubali kula kiapo cha kuwa waaminifu kwa "jamhuri ya Muungano wa Tanzania" wameondoa uwezo wote wa kuhoji legitimacy yake.

Ukishasema "argument inayotolewa kuhoji legitimacy yake haina mshiko" maana yake kunaweza kuwa na argument yenye mshiko. Ukishakubali kwamba kunaweza kuwa na argument ya legitimacy yenye mshiko, unakubali kwamba hoja ya legitimacy - whether a valid argument or an invalid one- ipo. Kwamba tunaweza kuhoji uhalali wa kiapo kwa msingi wa legitimacy ya misingi ya kiapo.

Lakini hata kama kungekuwa na hoja ya legitimacy, bado kunaleta shida. Kwanini waliapa kuwa waaminifu kwa kitu ambacho wanamashaka na uhalali wake?

Kama yule mtu anayekwambia "ndoa hii si halali kwa sababu huyu mume tapeli, aliponioa aliniambia hana mke na mimi ni mke pekee" na akadai kwamba kiapo chake cha ndoa si halali, basi na hawa wabunge nao wanaweza kutoa argument kwamba walivyoapa waliapa kwa nia nzuri tu, baadaye wakaja kuona mi document kuhusu muungano wakaona wamepelekwa mkenge kuapa kutetea muungano ambao msingi wake ni deception. Kama mtu ana valid arguments hii ni valid reason ya kubatili kiapo.

In both counts, hawa walioapa hawawezi kuwa wao ndio wanasimama na kusema tuvunje. Walioapa kulinda na kuhifadhi na kuwa waaminifu wanatarajiwa kusimamia kile walichoapa kukifanya.

Inategemea na misingi ya kiapo hapo juu. Mfano wa kiapo cha ndoa una apply. Mke akiapa kudumisha ndoa ya mme/mke mmoja na penzi, kwa maelewano kwamba mume naye atafanya hivyo hivyo, baadaye mume akaenda kuoa mke mwingine, ingawa mke aliapa kudumisha ndoa, kitendo cha mume kuvunja kiapo kinampa mke grounds za kuvunja kiapo chake katika talaka.

Taking the same analogy further, Slaa alivyokuwa analipua mabomu kwa kuanika nyaraka za serikali hadharani alitishiwa kwamba anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kuanika nyaraka za siri za serikali. Yeye akatoa utetezi technical kwamba hizo sheria zinakuwa nullified na the fact kwamba yeye anaanika nyaraka za serikali si kwa malicious intent, bali kama whistleblower. Basi kelele zote za kumshitaki zikaisha kwa sababu alikuwa na point. Huezi kuogopa kufanya jambo jema eti kwa sababu kuna kiapo kinakuzuia. Inabidi upime pro and cons.

Kama mtu ana grounds za kuvunja kiapo anavunja vizuri tu.

Vivyo hivyo, wanaotaka kuvunja muungano wakiweza kuthibitisha kwamba misingi fulani ya kiapo chao imevunjwa, wanaweza kutumia hilo kama sababu nzuri tu ya kuvunja viapo vyao.

Kama wanaona kuwa hawawezi kuendelea (katika dhamira safi) na bona fide basi wajitoe kwanza Bungeni au BlW ili waweze kusema kweli wana matatizo na Muungano. As long as they are sworn to be faithful to the United Republic of Tanzania, the people have to hold them accountable to that oath. Shouldn't they?

Si lazima, ukibatilisha msingi wa kiapo, na kama una watu wa kutosha waliokuchagua katika contituency yako wana support kuvunja muungano, utakuwa huna haja ya kujiuzulu ubunge. Mbunge ni mtumishi wa wananchi, si wa serikali. Isitoshe, an argument can be made kwamba wananchi hawatakiwi kukaa bila uwakilishi, hata kama ni uwakilishi katika bunge la serikali batili, if that is the process to go to a more legitimate government.

Point yako inaweza kuwa valid kwa mtu aliye kwenye baraza la mawaziri. It is absurd kusema unaona serikali ya Muungano haina legitimacy wakati wewe mwenyewe umo katika serikali. Lakini hata huyu, kama anafanya kazi kuivunja serikali hii ili kuje kuwa na a more legitimate government, naye anaweza kupata utetezi katika hili.
 
Mwanakijiji nadhani kusema wabunge wanaotaka muudo tofauti ya muungano watoke ni sawa na majibu ya ndugagai alimwambia Halima mdee kuwa zile posho za wabunge zilivyopitishwa hakuwepo na ka kama hawazitaki basi warudishe zote.

Mbunge sio Rais.. Angekuwa ni Rais au Waziri naweza kukuelewa lakini kwa mbunge hana ulazima wa kuachia ubunge ili atetee muundo wa serikali ulio swa kwa mtazamo wake au wananchi anaowakilisha.

Sababu tunategemea wabunge waheshimu kanuni za bunge zikiwemo na kanuni za posho zilizopitshwa kihalali na bunge. Lakini kwa mbunge kuhoji na kukataa uhalai wa oposho haina maana anavunja kanuni za bunge.

Tunategemea wabunge wawe na uwezo wa kuichallenge hata katiba kama ni kwa maslahi ya wananchi.

Nadhani, somo hili la "oath" linahitaji kueleweshwa vizuri. Mimi sina tatizo kwa Mbunge kuhoji au kujaribu kuonesha kasoro mbalimbali za muungano au matatizo. Haya mambo yapo na si mageni. Lakini wabunge na wananchi wana njia nyingi za kuweza kufanya hivi bila kusimama na kutaka kuvunja Muungano.

a. Wanaweza kuchallenge the constitutionality ya sheria inayokatakaza vyama vyenye kutaka kuvunja Muungano kuundwa. Hili wanaweza kufanya kwa kutumia mahakama au kwa kuwataka wabunge (wa pande zote mbili za Muungano) kufanya mabadiliko ya Katiba ya Muungano kuruhusu hilo. - hawajafanya hili.

b. Wanaweza kwenda kufungua kesi ya kikatiba kudai mambo fulani fulani kwa mfano, watu wamekuwa wakidai kuwa mambo ya Muungano yaliongezwa kulinganisha na makubaliano ya awali. Well, waende mahakamani na kuhoji utaratibu uliofanyika hivyo kama haukufuata Katiba au haukuzingatia sheria.

c. Wanaweza kufungua kesi mahakamani kwenye mambo ambayo wanaona kuna kugongana kati ya SJMT na SMZ. Hapa US kesi za mahusiano kati ya State na Federal Government are as old as the union itself. Kuna kesi zinazohusu mambo ya usalama, immigration, trade n.k Lakini hawasimami kusema kwa vile kuna mgongano kati ya Texas na Feds basi tuvunje Muungano.


Lakini kwenye la kiapo nirudie hotuba ya Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere baada ya kuapishwa kama Rais wa Jamhuri ya Tanganyika Disemba 9, 1962. Alizungumzia hivi kuhusu 'kiapo' maneno ambayo yangeweza kurudiwa kwa kila kizazi:

Yesterday I took an oath. I swore that as President of the Republic of Tanganyika I would to my duty and carry out my work without fear or favor, affection or ill will towards anyone. That was no hollow formula, to be spoken and forgotten. It was a most solemn promise, made before Almighty God, that with His help I shall prove myself worthy of the responsibility which you- the people of Tanganyika - have entrusted me; that I shall strive to fufill the task laid upon me without permitting myself to be of my comfort or convenience. I say "I' sore, but in actual fact it is true say that "we" swore; for I took that oath on your behalf. Every citizen of Tanganyika, whether he be the President, or a politician, a civil servant, a farmer, a teacher, or the lowest -paid worker in the land, every single one of us has an equal duty to give of his best. Every one of us has an equal duty to do the work entrusted to him - whatever that work may be - as if he too had taken a solemn oath to devote himself, without thought for his own advantage, to building our new Republic of Tanganyika".
 
Ninavyowasoma ndio ninaona tuna tatizo kubwa; mtu ameapa kufanya kitu hafanyi kwa sababu zake halafu tunashindwa kumbana kwa sababu tunafikiria kuwa ana uhuru wa kutokufanya. Viapo (oaths) ni vitu vizito sana. Tukikubali wabunge waape kulinda Katiba halafu tukasema wasisimamie kiapo chao kwanini tuamini watu wanaoitwa mahakamani na kulishwa kiapo watarajiwe kusema kweli kama hawamaanishi kiapo chao?

Rais amekula kiapo cha kazi ya Urais na ndani ya kiapo hicho cha kwanza ni kulinda Katiba. Sasa Rais huyo huyo akianza kuvunja Katiba kwa kisingizio cha "maoni tofauti" ataweza vipi kuendelea kuwa Rais? Kama tunamkubalia avunje kiapo chake kwenye jambo moja kwanini tusimkubalie kwenye mambo mengine? Wabunge wamekula kiapo kulinda Katiba, sasa wasipoilinda tusiwaulize? Maana kama viapo havina maana ni bora kutokuvishika, sivyo?

Au tuwape uchaguzi wanapokula viapo - wachague ni mambo gani wataapa kuyalinda ili tusipate shida ya kuwaliza. Kwa mfano, wabunge wanapoapa wasema "Naapa isipokuwa kwenye kulinda Muungano"...

Mwanakijiji,mazoea ujenga tabia na tabia ugeuka desturi na desturi ugeuka sheria,huo ndio ukweli katika uhalisia [REALITY] katika kulijadili swala hili la MUUNGANO.

Ukitizama wachangiaji wengi wa thread hii,wengi awatambui wala kuthamini msingi mkuu wa hoja yako kuwa KITENDO CHA MWAKILISHI/MBUNGE kujadili tu SWALA LA KUVUNJA MUUNGANO NI KOSA,kwake kwa kuwa WAKATI ANAINGIA NDANI YA BUNGE HILO,ALIAPA KUWA ATAILINDA NA KUITETEA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO.

Sasa kwa KUWA MBUNGE AU MWAKILISHI YUKO NDANI YA JAHAZI KAMA MMOJA WA MANAHODHA na fulsa hiyo hiyo huyo huyo MWAKILISHI AU MBUNGE ndie anashiriki tena kuitoboa jahazi au mashua hiyo basi kwa namna nyingine ANAISALITI mashua hiyo na kuwa adui wake namba moja.
Ndio maana Mwalimu kwa kujua swala hili kufikishwa bungeni zama zile chini ya Mzee John Marecela, ni kupitia hatua hizi kuwa yeye kama Waziri Mkuu hakustahiki hata kidogo kukubaliana na hoja hiyo ya wana G5 kwa kuwa inakuwa ni kinyume na KATIBA.

Kwa kuwa KIAPO [OATH] kwa Watanzania KINAONEKANA KUTHAMINIWA NA KUJULIKANA TU KWENYE SHERIA MAHAKAMANI,lakini kwa watendaji wa SERIKALI na vyama vya SIASA [haswa chama cha Mapinduzi] kimekosa maana.Maana Mwanachama wa CCM,wakati anapewa au anakabidhiwa KADI yake,mojawapo ni jukumu lake ni KIAPO kuwa ATATENDA HAKI daima na FITINA KWAKE Mwiko.

Ukiwatafuta wanachama hao leo ukawauliza kiapo hicho sidhani kama wanakikumbuka kiapo hicho kikoje.Na kwa kuwa ni tabia hiyo imeenda mpaka Serikalini, kwa KUWA KIAPO chochote,wapokea kiapo wameona au wanachukulia kama ni TARATIBU TU [FORMALITY] na kisha mambo mengine yanaendelea kama kawaida.Tabia hiyo imeendelea kuona kiapo kama ni kamchakato ka kufuatwa tu kama USTAARABU ambao ni lazima ufuatwe tu kisha mambo mengine yaendelea kama jana kama leo.

Hivyo kiapo kimeendelea kuwa hivyo na kuzalisha watu wenye kiapo wasiojua umuhimu wa kiapo haswa inapokuwa sio MAHAKAMANI,AU KWA MWANASHERIA ambako mtoa kiapo anawajibika kwa kiapo chake [Responsible].Hivyo naona kwa watendaji ambao wana athali kwa jamii kama Wabunge/Wawakilishi ,madiwani,wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa wanapokula KIAPO, basi waape mbele ya KIONGOZI HUYO ANAEPOKEA KIAPO LAKINI ANAEMWAPISHA AWE HAKIMU AU MWANASHERIA ALIYEVAA JOHO LA KISHERIA.kama vilevile RAIS anavyo HAPA MBELE YA JAJI MKUU.Yote hayo yatawakumbusha kuwa siku alipo APA aliapa mbele ya kiongozi wa SHERIA,hivyo anawajibika kisheria.

Kwa Watanzania wengi na kwa DESTURI zao,wanajua KIAPO,KIPO KWA RAIS,NA VIKOSI VYA ULINZI NA MAHAKAMANI NA VYOMBO VYA SHERIA TU na SIO kwa RAIA Wengine.

Hivyo basi swala la muungano imekuwa ni ugonjwa ambao unahitaji BUNGE MAALUMU.Na kwa kuwa mambo ya uendeshaji wetu YAMEGEUKA KUWA DESTULI imetishia UHAI WA MUUNGANO HUU,ambao Watawala wetu HAWANA MAARIFA YA KUUTETEA MUUNGANO HUU,kama MWALIMU ALIVYOKUWA NA HOJA ZA KUUTETEA.

KWA UJUMLA WANANCHI WAMECHOKA WANGEPENDA KUIONA ZANZIBAR IKIJITOA KAMA AMBAVYO IMEKUWA IKIKUSUDIA.LAKINI KWA KUWA NI SWALA LA KIKATIBA,WABUNGE AU WAWAKILISHI WANAOTAKA MUUNGANO UVUNJWE WATOKE KWANZA BUNGENI WAJE NJE KUFANYA HARAKATI ZAO.TOKA HAPO MCHAKATO WA KATIBA MPYA ITAWAPA FULSA NJEMA YA KUTIMIZA HOJA YAO HIYO.

Mimi kwa upande wa Sheria nimekuwa nikikwazika sana,lakini kwa kuwa ni jambo la kisheria na kikatiba sina budi kuliangalia katika sura hiyo nikisubilia mchakato wa KATIBA MPYA.Kwa ukweli Wanzanzibar na CHOKOCHOKO ZAO ningetamani tuwaweke PEMBENI kwa muda japo miaka KUMI TU [10] watafika wapi huku, jicho letu likiwa karibu wasije wakatuundia SOMALIA ya jirani nyingine, na kuanza kufuga maharamia [PILATES].

Mwalimu nae alichukia visiwa hivi alitamani kama angeweza angevisukuma huko katika ya bahari [Deep See] vikapotea mbele ya uso wa macho yetu,Lakini ndio hivyo mungu aliviweka hapa karibu nasi ili tuishi navyo hivi hivi na kutupa changamoto zao za kutufanya kuwa ni jukumu la maisha yetu ya kila siku kama wanadamu pamoja na hizo kero zao.Kwa ujumla wazenj wanachafua kama unamoyo mwepesi unaweza ukafanya maamuzi ya kukurupuka na baadae yakakugharimu.Utamaduni wao wa kuwa watu wasiotabilika na wenye kuwa na maamuzi tofauti na maamuzi waliyoyafanya jana inawagharimu na kutupatia wakati mgumu katika kuishi ndani ya muungano huu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom