Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Chama cha Mapinduzi-CCM kimesema mwanachama yeyote wa chama hicho aliyeshindwa katika uteuzi wa wagombea ubunge na udiwani anayeona ni vizuri akahamia chama kingine cha siasa, anaruhusiwa kufanya hivyo, imeelezwa.
Chama hicho kimesema hakitaathiriwa na hatua ya wanachama wake wasioridhika na uamuzi wa vikao vyake vya juu na hivyo kinatoa baraka zote.
Akizungumza na gazeti hili jana akiwa Dodoma, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, alisema iwapo kuna mwanachama anayetaka kuhama kwa kisingizio cha kushindwa kuteuliwa na afanye hivyo na ikiwezekana chama kitamsindikiza.
"Waende … waacheni waende nasi tutawasindikiza. Kwanza kuondoka kwao ni sawa na kuchota ndoo moja au mbili za maji Mto Rufiji, kwani maji yake kamwe hayatapungua, yatabaki vilevile kwa hiyo waende tu," alisema Msekwa.
Source: Habari Leo
My take; Ina maana CCM imetosheka kiasi hicho hata haioni hasara kuondokewa na wanachama wake kama huku si kufuru ni nini. Nafikiri kazi mojawapo ya chama ni kuongeza wanachama naona hapa Msekwa kateleza kidogo.
Chama hicho kimesema hakitaathiriwa na hatua ya wanachama wake wasioridhika na uamuzi wa vikao vyake vya juu na hivyo kinatoa baraka zote.
Akizungumza na gazeti hili jana akiwa Dodoma, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, alisema iwapo kuna mwanachama anayetaka kuhama kwa kisingizio cha kushindwa kuteuliwa na afanye hivyo na ikiwezekana chama kitamsindikiza.
"Waende … waacheni waende nasi tutawasindikiza. Kwanza kuondoka kwao ni sawa na kuchota ndoo moja au mbili za maji Mto Rufiji, kwani maji yake kamwe hayatapungua, yatabaki vilevile kwa hiyo waende tu," alisema Msekwa.
Source: Habari Leo
My take; Ina maana CCM imetosheka kiasi hicho hata haioni hasara kuondokewa na wanachama wake kama huku si kufuru ni nini. Nafikiri kazi mojawapo ya chama ni kuongeza wanachama naona hapa Msekwa kateleza kidogo.