Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 9,446
- 19,227
huo upo mbeya huko na tunduma. unauza uhai wako kwa shetani na manake unakubaliana naye kwamba hata ukifa utaenda motoni moja kwa moja kwa raha chache za dunia hii. ndio maana kuku akidonoa punje moja, utaishi maisha ya pesa ndefu kwa mwaka mmoja na utapata kifo cha kushtukiza tu hata nafasi ya kutubu hutapata, watasikia tu umedondoka umekufa. wale wa Mbeya wanajua kilichompata yule jamaa wa kahotel golden city hotel pale sae. sitaki kuongeza neno.Nikiwa kwenye basi katika harakati za kuitafuta shs, tumesimama kuchimba dawa eneo linaonekana kama kijiji baada ya makambako kuelekea mafinga, ni eneo flani inaonekana kuna vyoo vya mtu binafsi ila abilia hatulipi na sijui nani anayehudumia hivyo vyoo!.
Nikiwa ndani ya chumba natoa oil chafu ya mwilini kwa nyuma nasikia majibizano makali tu kutoka kwa watu wawili, kutokana na majibizano yao nikagundua mmoja ni mganga na mwingine ni mteja.
Jamaa aliyekuwa anafoka alikuwa anadai inakuwaje jogoo akala punje 3 za mahindi kisha kuondoka wakati hakuwa na chakula kwa muda?, Sikusikia jibu kutoka upande wa pili ila baadaye jamaa inaonekana ni mteja akaomgeza "jogoo wangu niliyekuja naye mpaka sasa bado anakula punje za mahindi ila wako amekula 3 na kuondoka, kwa nini?"
Ila kwa sababu tulipewa dakika 5 za kuchimba dawa sikuweza kufuatilia au kujua kilichoendelea katika kujiuliza nimeileta ili wale wadau wa Jogoo na punje za mahindi mje mtujuze ni nini hiki?.
Niliwahi sikia utajiri wa punje za mahindi kuwa jogoo anapokula punje kadhaa basi huo ndiyo uhai wa utajiri wako kulingana na alivyokula but imekuwaje kukawa na jogoo wawili tofauti, yaani wa mteja na wa witchcraft. na huyo wa mganga akala tatu na kusepa ila wa mteja akaendelea kula?