Wanaotafuta kazi kwenye NGO eleweni hili

Habari zenu,

Kama unatafuta kazi kwenye hizi NGO's ziwe za Local au International kuna usanii mkubwa sana kwenye kuajili au kwenye ajira zao.

Yani wanajifanya wanatangaza kazi na kuita watu kwenye usaili kumbe wana Mtu wao mapema yupo na kazi ashaanza wanaita na kukufanyia usaili wakiwa wanakuenjoy tuu.

Mfano mimi.

1. Niliitwa kwenye usaili Morogoro kwenye NGO moja hivi tukiwa wanne tuu wakatufanyia usaili ila kabla ya usaili walitupatia chai kumbe aliyekuwa anatusavia chai ndio mwenye nafasi hiyo akawa anatuenjoy tuu

2. Niliitwa kwenye usaili Mbeya nako tukawa tunafanya usaili na anayetufanyia usaili ndio mwenye nafasi wajinga sana wale jamaa harafu ni shirika la dini

3. Kwenye shirika ninalofanya kazi japo ni international nako tumewafanyia watu usaili jana tarehe 7 wakati watu wameajiliwa toka tarehe 2/1/2019 yani mwendo ni ule ule tuu mie nimeumia kweli

N.B .
Wasaka ajili kwenye haya mashirika eleweni hivyo japo siyo mashirika yote yana upumbavu huo ila mengi ndio mtindo wao.

OMBI LANGU KWA MA HR na Ma-Director General

1. Acheni kusumbuwa watu kama mnavindugu vyenu au wapenzi wenu mnavipachika tuu basi sio manajifanya mnatangaza harafu mnnawapotezea watu mda na nauli zao

2. Acheni unafiki wa kuwafanyisha watu usaili wakati mshaajili na mkiulizwa mshaajili mnajibu bado tuta tuma email kumbe unafiki mtupu

3. Kama mnajuwa mshawaweka jamaa zenu jengeni utaratibu wa kuwarudishia watu nauli,, yani mtu anatoka kigoma anakuja kwenye usaili hewa hapa dar, mngejuwa safari ya dar to kigoma ni noma

ASANTENI

By. Akili Mbili
Duh hatari sana mkuu ,
Sasa tusiokuwa na hizo connection tufanyaje? 🤔🤔
 
Ila na nyie mnapoomba kazi kwenye hizi NGO make sure you meet all the qualifications walizozitangaza otherwise hautakuwa shortlisted kama unamis even one qualification

Mfano, mbali na job description lakini kuna zile qualifications common ambazo huwa tunaziangalia kwa macho yote
1. Experience with USG funded projects in similar position...hii kama huna sahau kupata kazi kwenye NGO ya mmarekani...lazima uwe umeshapata experience from other NGO's ambazo zinafadhiliwa na serikali ya marekani...tena uwe umefanya kwenye similar posigion, unless iwe ni positions ndogondogo kama za udreva au reception unaweza kupata ila senior position huwezi kupata bila hii qualification

Pili: kama wameandika 5 yrs experience make sure you have those 5 yrs tena kwenye similar position, sasa mgu anaaply experience yake ni miaka miwili au ni miaka tisa, hapo kupata sahau

Tatu,unaweza ukawa umemeet hivyo vigezo vyote lakini ukashindwa kujitetea kwenye interview...mfano kuna mtu tulimwita kwenye interview nafasi ya clinical manager, alikua na vigezo vyoteee na alikua anafanya kazi kwenye hospitali ya rufaa mbeya, cha ajabu kila tulichokua tunamuuliza anajibu please jump to another question this one is too long, i wont finish to answer it today, ukienda kwenye swali jingine ameshindwa hata kuelezea challanges anazokutana nazo kwenye mazingira ya Kazi na anazitatua vipi, kiykweli inasikitisha maana watumishi wetu wanaotutumikia huko serikalini hawajitambui, CV imeshiba ila kujieleza hawezi hata kidogo

Mtu kama huyo hata bure hatumwajiri abaki tu huko serikalini ndo panamtosha

Ni changamoto ila ndio hali halisi

Kwa hiyo jamani wakati mwingine tusilaumiane maana kuna vitu pia huwa tunaangalia, atlist hawa wanaotoka kwenye other NGO's huwa wana uwezo wa kujieleza maana huwa wanafanya kazi practically na sio kwenye makaratasi kwa hiyo mara nyingi huwa wanaeleza kitu wanachokifahamu ila hawa wa serikalini wanafanya kazi kwenye makaratasi ukimwambia aelezee uhalisia wa kazi anayoifanya hawezi

Sent using Jamii Forums mobile app
Ikiwa tayar ulishakiri kuwa kuna kufill nafas ambazo hata watu wake hawakutakiwa kuwa pale na bado ukaita interview
Haya yote uliyosema hayana maana
Kwa kuwa anawez fika qualifications zote na akajitetea kwa interviews
Ila nafasi yake mshampa mwingjne
Nonsense !!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nachofaham MAHR mpo humu
Na NGOs staff mpo wengi humu..

Naombeni mnisaidie

Status : job seeker,Internships& volunteering hunter
Education : Bachelor degree(2022)
Field : community economic development (SOCIAL WORKER )
Experience : Fresh graduate (1 month of field-out of NGO)
Location (currently): kigoma urban .
Scope of work: Everywhere .

Mtende Akili 2 Tutor B
Msaada!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu HR mtende kasema vitu vya ukweli niliomba post kampuni ya jti(japan international tobacco) HQ ipo Geneva-Uswisi. Post zao una apply kwa portal CV zinaenda Geneva wana sort candidate wanasend Tz HQ Dar TCC(Tanzania Cigarrete Company),TCC wana sort wanatuma branch ya Tabora ndo mnaitwa interviwe mnakuwa mmeitwa watu wachache kweli.ila Mungu mkubwa.
 
Habari zenu,

Kama unatafuta kazi kwenye hizi NGO's ziwe za Local au International kuna usanii mkubwa sana kwenye kuajili au kwenye ajira zao.

Yani wanajifanya wanatangaza kazi na kuita watu kwenye usaili kumbe wana Mtu wao mapema yupo na kazi ashaanza wanaita na kukufanyia usaili wakiwa wanakuenjoy tuu.

Mfano mimi.

1. Niliitwa kwenye usaili Morogoro kwenye NGO moja hivi tukiwa wanne tuu wakatufanyia usaili ila kabla ya usaili walitupatia chai kumbe aliyekuwa anatusavia chai ndio mwenye nafasi hiyo akawa anatuenjoy tuu

2. Niliitwa kwenye usaili Mbeya nako tukawa tunafanya usaili na anayetufanyia usaili ndio mwenye nafasi wajinga sana wale jamaa harafu ni shirika la dini

3. Kwenye shirika ninalofanya kazi japo ni international nako tumewafanyia watu usaili jana tarehe 7 wakati watu wameajiliwa toka tarehe 2/1/2019 yani mwendo ni ule ule tuu mie nimeumia kweli

N.B .
Wasaka ajili kwenye haya mashirika eleweni hivyo japo siyo mashirika yote yana upumbavu huo ila mengi ndio mtindo wao.

OMBI LANGU KWA MA HR na Ma-Director General

1. Acheni kusumbuwa watu kama mnavindugu vyenu au wapenzi wenu mnavipachika tuu basi sio manajifanya mnatangaza harafu mnnawapotezea watu mda na nauli zao

2. Acheni unafiki wa kuwafanyisha watu usaili wakati mshaajili na mkiulizwa mshaajili mnajibu bado tuta tuma email kumbe unafiki mtupu

3. Kama mnajuwa mshawaweka jamaa zenu jengeni utaratibu wa kuwarudishia watu nauli,, yani mtu anatoka kigoma anakuja kwenye usaili hewa hapa dar, mngejuwa safari ya dar to kigoma ni noma

ASANTENI

By. Akili Mbili
Ni sheria kutangaza ajira ili na wao wwaon
 
Kwanza nikujuze kama nafasi ya kazi ni moja hatuwezi kuita watu 18 kwenye usaili, tutaita watu watatu, kama nafasi ni kumi tutaita watu ishirini, policy yetu inaturuhusu kwenda kwa ratio ya moja kwa mbili unles kama nafasi ni very competent lets say tunatafuta country director basi tutawafanyie interview watu wanne mpaka watano lakini kwa nafasi ya kawaida huo muda wa kuita watu wengi hatuna na sijawahi katika experience yangu as HR kwenye NGO

Pili kwa sehemu ambazo nimeshafanya kazi, hatujawahi kufanyisha watu interview zaidi ya mbili, mara nyingi interview inakua ni moja ya oral lakini kwa baadhi ya nafasi kama communications officer lazima wafanye na written au atupatie sample ya writting ambayo amewahi kuifanya, watu wa research kwa senior positions pia lazima wafanye practical kwa maana ya tools au programs wanazotumia kutengeneza reports na watu position za director and deputy director ambapo interview zao mara nyingi wanafanyiwa moja kwa moja kutoka marekani through skype then baada ya hapo ndio wanakuja for final intervieew kwetu sisi

Pia kama mtu amequalify huwa tunawasiliana na referees wake kwanza baada ya referee kutoa feedback ndio tunaamua kumuajiri mtu kutokana na feedback tuliyoipokea, kuna referees wengine huwa wanatoa feedback inayotia mashaka na sisi huwa tunapima kama kuna feedback zinazotia mashaka hatuwezi kukupa mkataba wala kukutaarifu kwamba umequalify we will go to the next candidate

Sasa sijajua kwa swali lako kwamba kwa nini mtu anakua ameshafanyiwa interview zaidi ya moja na reference check imeshafanyika bado haajiriwi hilo ntashindwa kukujibu, either feedback ya reference zako haikua clear au kuna other internal reasons lakini kwa mimi sijawahi kukutana nayo

Mara nyingi tukishapata reference feedback tunachofanya ni kumnotify candidate na kukubaliana mshahara pamoja na tarehe ambayo atakua available kuanza kazi then tunamuandalia mkataba

Kama kuna ambalo sijakujibu uwe huru kuuliza

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu,hakuna nafasi huko na Mimi niombe kazi
 
Ni kweli kabisa.Nilipomaliza chuo nilibahatika kupata internship mwenye international NGOs.
HR aliniambia niandae Tangazo la ajira Kisha nirushe kwenye mitandao nikiwa naliandaa watu walishaajiriwa nikiwemo mimi niliduwaa lakini HR akaniambia zungusha bongo dogo.Nilipost lile Tangazo kwenye mitandao watu walikuja interview lakini hakuna aliyepata.

Kufanya kazi kwenye NGOs raha lakini uchumi wa mabeberu ukiyumba hatari.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu heshima yako. Bado umekaba nafasi kwenye hiyo NGO?

Nimegraduate November 2022 na bachelor's degree in management of social development, I'm 24 years old na ninaishi Kigamboni.

Unaweza kunisaidia kupata internship?
 
Akili 2, Mimi ni mmoja wa HR kwenye international NGO na sio NGO ya kwanza kufanya kazi, niseme tu ukweli labda eirher hujui au huna uhakika na unachokisema, hakuna sehemu zenye kutenda haki kwenye utoaji wa ajira kama NGO' s especially za wamarekani, sina uhakika na NGO zingine maana sina uoefu nazo ila zilizopo chini ya mmarekani ajira inapatikana kwa haki kwa kuzingatia vigezo vinavyohitajika kwa nafasi husika na ndio maana unakuta NGO huwezi kukutana na watendaji wavivu kama serikalini maana hakuna kujuana wala undugu ni haki bin haki

Labda wewe umekutana na usanii kwenye local NGO ot somewhere else ila usipotoshe

Sent using Jamii Forums mobile app

Greetings sir.

Me ni fresh graduate na nina bachelor's degree in management of social development granted by MNMA November, 2022.

I am a 24 years old male resident of Kigamboni. Kuna internship vacancies kwa sasa kwenye taasisi yenu?
 
Greetings sir.

Me ni fresh graduate na nina bachelor's degree in management of social development granted by MNMA November, 2022.

I am a 24 years old male resident of Kigamboni. Kuna internship vacancies kwa sasa kwenye taasisi yenu?
Hapa ulipomfata obvious atakujibu hakuna , ungemfata chemba

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
 
Hapa ulipomfata obvious atakujibu hakuna , ungemfata chemba

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app

Dooh! umenena vyema mkuu ila sasa hali yangu ni taabani kiasi kwamba hata simu nnayotumia (microsoft) haikubali ku'install app ya JF wala ku'update browser kwahiyo siwezi ku'access PM yangu.

Ila all in all nimejaribu bahati tu mkuu, let's wait and see how it'll play out.
 
Back
Top Bottom