Wanaopigwa Chini CHADEMA Wamelostishwa na Mh. Lowassa

Hashpower7113

JF-Expert Member
Sep 26, 2011
1,353
2,137
C&P
“Piiiipooz..... pawaaa!”

Nikisikiaga hizi mambo nakumbuka mauchaguzi ya 2015 yaliyomuweka Anko Magu hapo kati Magogoni nini! Dah! Asikwambie mtu, zile mbishe za mauchaguzi kipindi kile zilikuwa noma sana!

Unakumbuka zile mitkasi za mafuriko ya mshua mamvi? Daah! Ilikuwa noma sana, unaambiwa kila mshua akihutubia mahali, hilo nyomi lake acha kabisa! Ni fact kwamba washua kibao kutokea upande wa pili waliopo mjengoni now, ni kwa sababu ya upepo wa mamvi!

Watu walipagawishwa kinoma na siasa zake! Unajua mshua aliwawini sana watu baada ya kutangaza kuhamia pipoz pawa alipokatwa ile kiroho mbaya chamani nini, akasepa na kijiji kuhamia upande wa pili. Amsha amsha zikawa za kufa mtu.

Alipoamua kusepa na kijiji, washua kibao nao walisepa naye, nao wakavua mbogamboga na kutinga gwanda ile kibabe, ikawa ni mwendo wa vidole viwili juu na kuonesha ile ishara ya kuzungusha mikono hewani!

Hata siku ya kugonga mavoti nini, wana kibao walijitokeza front, si unajua tena masela huwa wanapenda kwenda against na gavamenti, yaani ndiyo iko hivyo kila nchi, hata masteti kwa Trump pigo ni hizohizo.

Basi mshua mamvi akakomba makura kibao nini, sema Anko Magu akampiga gepu na mwisho ndiyo akawa presidaa ile kimagutumagutu! Wana waliomchagua mamvi, wakaona safari ya matumaini haijafika mwisho nini, 2020 inakuja hiyo.

Huku na kule mara paap, mamvi akawabadilikia masela, si akarudi chamani bwana! Unaambiwa wana walimaindi ile kinyama sema kwa sababu ya respect ya mshua nini, wakaamua kumvungia! Ila wakawa wamejifunza kwamba kuna masnichi kibao ambao walisepa na upepo wa mamvi.

Ishu inayotrendi kwa sasa, ni mchongo wa mauchaguzi ndani ya chama la wazee wa Pipoz Pawa! Juzikati hapo mauchaguzi ngazi ya ngazi ya kanda nini, yamemalizika. Sasa ishu ni nini? Unaambiwa wale washua waliohama na upepo wa mamvi, wamechezea za uso kinyama!

Wana si bado wana hasira za mamvi kuwachuuza? Wakaona aah, kumbe mnatuektia nini siyo? Sasa dawa yenu ni kuwapiga chini! Mwamba kule Kusini kachezea za uso, mshua Fred na yeye hapo kati wana wamemkazia, kapigiwa makura ya hapana kama yote akapagawa kinyama mwisho kasanda, kaamua kutundika daruga na kusema shit kibao, si unajua tena zile mitkas za sizitaki mbichi hizi!

Wamba wa Pipoz wana hasira mazee, ishu ya mamvi kuwabwaga bado inatembea kweye vichwa vyao na safari hii ni kama wameamua ile kama mbwai mbwai, hakuna kumsapoti snichi! Piga chini!

Hapo kati Desemba 18, wazee wa pipoz wanaenda kuhitimisha kwa kumchagua chairman wa chama nini! Unaambiwa mzee wa Bilicanas njia nyeupe, japo kuna wana wanamfanyia figisu asitoboe, lakini mpaka sasa ni kama mzee baba kakanyaga ganda la ndizi, yaani ile kiulaaiiiini, kama ananawa vile!

Ndiyo, masela wameona kama vipi aendelee kukaa front kuwaongoza maana mambo yashakorogeka haya! Sema mbogamboga wanamaaaaindi! Mzee wa Billz misheni tauni yule, anazijua figisu na anajua namna ya kuwakomesha ile kiroho mbaya nini, wanamhanya sema ndo watafanya nini sasa! Wana na chama lao washaamua.

Kwenye uvais chairman nini, namuona mwamba Tunduni akila shavu kutoka mamtoni kama ananawa vile! Kwa hiyo inakuwa huku mzee wa Billz, kule mwamba Tunduni, patamu hapo! Kama nawaona machizi wa Lumumbani nini!

Sema mshua Mamvi na wewe unawadisapoint kinyama masela, yaani nyomi yote ile uliyokuwa unakula, wana wakajitoa tag ubavu kukusapoti mwisho wa siku unarudfisha mpira kwa kipa? Umezingua mshua ndo maana watu wanamalizia ugwadu kwa kina Fred na kampani yake!

Mhuni Smart!
 
Siasa ya 2015 Mwakalebela alitengeneza tukio hili nakumbuka wana walimmaindi kinoma noma
tapatalk_1575432250202.jpeg
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom