Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,645
Wakuu habari za Jumapili. Najua mada hii ninayoianzisha nitapata upinzani mkubwa sana na matusi mengi mno. Lakini kabla hamjanitukana nawaomba mfikiri sana na muweke pembeni ushabiki.
Ni kwamba kwa muda mrefu sana Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh. Paul Makonda amekuwa midomoni mwa watu wengi wakimsema kwa mabaya mengi. Tena utakuta mtu anayeonesha chuki kwa mkuu huyu wa Mkoa wa Dar Es Salaam ukimuuliza sababu hataweza kukueleza ni kwa nini anamchukia. Wengi wanafuata mkumbo tu baada ya kuona watu wenye ushawishi na uwezo wa kupanga maneno wanamsema vibaya.
Hebu kaeni chini mjiulize na mfanye uchunguzi kwa kujiuliza kosa la Mh Makonda ni lipi? Kuweni wakweli wakati mkitafakari hayo kama nilivyosema hapo juu kwamba muweke ushabiki pembeni.......!!!
Tulipokuwa chuoni tulikuwa tukiandamana kwenda kudai posho wizarani. Wakati huo usipoandamana wanafunzi wenzako wanakuona mbaya na utapata taabu sana kama hukuhudhuria ama kuungana nao kwenye maandamano. Ndicho kinachotokea kwa Mh Paul Makonda. Ukimuuliza mtu kwa nini anamsema vibaya Mheshimiwa huyu utakuta hata yeye hajui!!!
Wana Dar Es Salaam mjiulize sana ubaya wa Makonda. Hivi kosa lake ni kuwaletea maendeleo? Ina maana ninyi hampendi au hamtaki maendeleo?
Eti mnadai Mh Paul Makonda hana vyeti.....na kwamba eti alifeli......pia eti jina lake si hili la Paul Makonda bali analo jina lingine.........!!!
Mimi nashangaa sana.....
Hivi mlikuwa wapi toka Mh Paul Makonda bado mvulana mdogo kabisa kufichua hilo jina lake? Mmesubiri mpaka amekuwa Mkuu wa Mkoa ndio mnaibuka na kudai hana vyeti na jina lake analotumia si lake? Miaka yote mlikuwa wapi??? Acheni ubabaishaji!!
Yaani unasubiri mtu amepata mafanikio ndio mnaibuka ili mumharibie? Kama ni hivyo basi ninyi ni watu wabaya sana!!! Hamfai..........!!
Nirudi kwenye hili la vyeti.
Kwamba kama ni kweli watu wanayoyasema (kitu ambacho mimi siamini kabisa maana nchi hii ina vyombo vingi sana vya upelelezi vilishindwa kujua hili? Eti mtu mwingine asiye na taaluma ya upelelezi aje atuaminishe na sisi kwa kufuata mkumbo tumeamini uzushi!!!) basi Mh Paul Makonda is a hero!!!
He is a fighter! Badala ya kubezwa angepewa hongera kwa juhudi za ku struggle kutafuta maisha!!! Wangapi wamerudia kusoma darasa la saba bwana na leo hii ni maprofesa? Yaani ku fight kuondoa ujinga ni kosa?
Lakini hoja ya msingi hapa ni madai yanayotolewa na watu eti Mh Makonda jina lake sahihi ni Bashite. Huu ni ujuha wa hali ya juu. Hivi unaamini vipi jina la Bashite na kuacha la Paul Makonda? Yaani jina analotumiia mwenyewe hulikubali bali unakubali jina linalozushwa mitandaoni? Huo ni usomi gani Watanzania mnauonyesha?
Lengo langu si kumtetea Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam bali nasema ukweli mtupu. Tuacheni ubabaishaji!!
Eti kuna madai Mh Makonda alivamia studio za Clouds.......mimi naomba niulize swali.....
Hivi hiyo Laptop na kile chumba alichokuwa akitumia hapo ofisi za Clouds nacho alikiteka? Na hicho chakula alichokuwa akiwekewa na uongozi wa Clouds kisha wanampigia simu chakula kipo tayari anakwenda kula nao meza moja napenyewe aliwateka?
Hiyo Laptop ya Mh Makonda iliyokuwa hapo ofisini kisha baada ya muda wa kazi wanamkaribisha kufanya kazi zake binafsi napo aliwalazimisha kwa nguvu ikae hapo? Mbona haya yote sijasikia mkiyatafakari bali mnatafakari vyeti tu na jina?
Jambo usilolijua huna haki ya kulizungumzia. Hivi mtakuja kupata mkuu wa mkoa mchapa kazi kama Paul Makonda? Kosa lake ni lipi hili la kupambana na maharamia wa madawa ya kulevya? Kwa hiyo mnatakaje sasa? Mnataka Dar Es Salaam na nchi kwa ujumla iwe na mazezeta wabwia unga ndio mnaona sawa?
Hii haikubaliki!!! Msitumie vyombo vya habari na uhuru wa habari kupakazia watu. Kama ni vyeti mbona watoto wenu hawana kabisa mbona hamsemi!!
Huo ugomvi wa Clouds na Makonda ni wa kibinadsi zaidi.
Wanajua ni kipi makonda alikuwa anakifanya. Walimkaribisha wenyewe studio na wala hakuvamia. Wasitake kudhani sisi ni wajinga kiasi hicho.
Makonda ni mchapa kazi.
1. Anataka Dar Es Salaam wanafunzi wafaulu.
2. Anataka Dar Es Salaam iwe ni jiji safi
3. Anataka barabara zote ziwe nzuri
4. Anataka kuwepo amani ya nchi
5. Hataki uonevu kwa raia
6.Ni mtu wa watu
7. Anataka watu wapate ajira
8. Anataka vijana wapewe nafasi za kuongoza nchi
9. Anataka watu walipe kodi
10. Anapiga vita madawa ya kulevya na ufisadi
Sasa huyu mtu ubaya wake ni upi?
Kwa hiyo nimegundua watu wamekuwa overwhelmed na mwangi tu yaani mkumbo wa watu. Hana kosa. Weka ushabiki pembeni kisha waza mwenyewe kwa makini utagundua Dar ina Mkuu wa Mkoa madhubuti sana.
Nampongeza sana Mh Makonda kwa kukaa kimya bila kujibizana na watu maana anajua ni kitu gani wananchi tunataka.
Nasubiri matusi na upinzani mkali kutoka kwa wachangiaji lakini sitajali.......
Mh Makonda chapa kazi!
Ni kwamba kwa muda mrefu sana Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh. Paul Makonda amekuwa midomoni mwa watu wengi wakimsema kwa mabaya mengi. Tena utakuta mtu anayeonesha chuki kwa mkuu huyu wa Mkoa wa Dar Es Salaam ukimuuliza sababu hataweza kukueleza ni kwa nini anamchukia. Wengi wanafuata mkumbo tu baada ya kuona watu wenye ushawishi na uwezo wa kupanga maneno wanamsema vibaya.
Hebu kaeni chini mjiulize na mfanye uchunguzi kwa kujiuliza kosa la Mh Makonda ni lipi? Kuweni wakweli wakati mkitafakari hayo kama nilivyosema hapo juu kwamba muweke ushabiki pembeni.......!!!
Tulipokuwa chuoni tulikuwa tukiandamana kwenda kudai posho wizarani. Wakati huo usipoandamana wanafunzi wenzako wanakuona mbaya na utapata taabu sana kama hukuhudhuria ama kuungana nao kwenye maandamano. Ndicho kinachotokea kwa Mh Paul Makonda. Ukimuuliza mtu kwa nini anamsema vibaya Mheshimiwa huyu utakuta hata yeye hajui!!!
Wana Dar Es Salaam mjiulize sana ubaya wa Makonda. Hivi kosa lake ni kuwaletea maendeleo? Ina maana ninyi hampendi au hamtaki maendeleo?
Eti mnadai Mh Paul Makonda hana vyeti.....na kwamba eti alifeli......pia eti jina lake si hili la Paul Makonda bali analo jina lingine.........!!!
Mimi nashangaa sana.....
Hivi mlikuwa wapi toka Mh Paul Makonda bado mvulana mdogo kabisa kufichua hilo jina lake? Mmesubiri mpaka amekuwa Mkuu wa Mkoa ndio mnaibuka na kudai hana vyeti na jina lake analotumia si lake? Miaka yote mlikuwa wapi??? Acheni ubabaishaji!!
Yaani unasubiri mtu amepata mafanikio ndio mnaibuka ili mumharibie? Kama ni hivyo basi ninyi ni watu wabaya sana!!! Hamfai..........!!
Nirudi kwenye hili la vyeti.
Kwamba kama ni kweli watu wanayoyasema (kitu ambacho mimi siamini kabisa maana nchi hii ina vyombo vingi sana vya upelelezi vilishindwa kujua hili? Eti mtu mwingine asiye na taaluma ya upelelezi aje atuaminishe na sisi kwa kufuata mkumbo tumeamini uzushi!!!) basi Mh Paul Makonda is a hero!!!
He is a fighter! Badala ya kubezwa angepewa hongera kwa juhudi za ku struggle kutafuta maisha!!! Wangapi wamerudia kusoma darasa la saba bwana na leo hii ni maprofesa? Yaani ku fight kuondoa ujinga ni kosa?
Lakini hoja ya msingi hapa ni madai yanayotolewa na watu eti Mh Makonda jina lake sahihi ni Bashite. Huu ni ujuha wa hali ya juu. Hivi unaamini vipi jina la Bashite na kuacha la Paul Makonda? Yaani jina analotumiia mwenyewe hulikubali bali unakubali jina linalozushwa mitandaoni? Huo ni usomi gani Watanzania mnauonyesha?
Lengo langu si kumtetea Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam bali nasema ukweli mtupu. Tuacheni ubabaishaji!!
Eti kuna madai Mh Makonda alivamia studio za Clouds.......mimi naomba niulize swali.....
Hivi hiyo Laptop na kile chumba alichokuwa akitumia hapo ofisi za Clouds nacho alikiteka? Na hicho chakula alichokuwa akiwekewa na uongozi wa Clouds kisha wanampigia simu chakula kipo tayari anakwenda kula nao meza moja napenyewe aliwateka?
Hiyo Laptop ya Mh Makonda iliyokuwa hapo ofisini kisha baada ya muda wa kazi wanamkaribisha kufanya kazi zake binafsi napo aliwalazimisha kwa nguvu ikae hapo? Mbona haya yote sijasikia mkiyatafakari bali mnatafakari vyeti tu na jina?
Jambo usilolijua huna haki ya kulizungumzia. Hivi mtakuja kupata mkuu wa mkoa mchapa kazi kama Paul Makonda? Kosa lake ni lipi hili la kupambana na maharamia wa madawa ya kulevya? Kwa hiyo mnatakaje sasa? Mnataka Dar Es Salaam na nchi kwa ujumla iwe na mazezeta wabwia unga ndio mnaona sawa?
Hii haikubaliki!!! Msitumie vyombo vya habari na uhuru wa habari kupakazia watu. Kama ni vyeti mbona watoto wenu hawana kabisa mbona hamsemi!!
Huo ugomvi wa Clouds na Makonda ni wa kibinadsi zaidi.
Wanajua ni kipi makonda alikuwa anakifanya. Walimkaribisha wenyewe studio na wala hakuvamia. Wasitake kudhani sisi ni wajinga kiasi hicho.
Makonda ni mchapa kazi.
1. Anataka Dar Es Salaam wanafunzi wafaulu.
2. Anataka Dar Es Salaam iwe ni jiji safi
3. Anataka barabara zote ziwe nzuri
4. Anataka kuwepo amani ya nchi
5. Hataki uonevu kwa raia
6.Ni mtu wa watu
7. Anataka watu wapate ajira
8. Anataka vijana wapewe nafasi za kuongoza nchi
9. Anataka watu walipe kodi
10. Anapiga vita madawa ya kulevya na ufisadi
Sasa huyu mtu ubaya wake ni upi?
Kwa hiyo nimegundua watu wamekuwa overwhelmed na mwangi tu yaani mkumbo wa watu. Hana kosa. Weka ushabiki pembeni kisha waza mwenyewe kwa makini utagundua Dar ina Mkuu wa Mkoa madhubuti sana.
Nampongeza sana Mh Makonda kwa kukaa kimya bila kujibizana na watu maana anajua ni kitu gani wananchi tunataka.
Nasubiri matusi na upinzani mkali kutoka kwa wachangiaji lakini sitajali.......
Mh Makonda chapa kazi!